Saturday, March 28, 2015



Bondia MOHAMED MATUMLA, SNAKE BOY JUNIOR amewatoa watanzania kimasomaso baada ya kutandika bondia WANG XIN HUA kutoka CHINA na kuibuka na ubingwa wa WBF UZANI wa BANTAM katika pambano lilofanyika katika ukumbi wa DIAMOND JUBLIEE jijini DSM.
Katika pambano hilo ambalo lilikuwa na ushindani wa hali ya juu, MATUMLA, amemchapa WANG XIN HUA kwa ALAMA.
Kwa usindi huo MATUMLA amepata nafasi ya kucheza pambano la utangulizi wakati wa pambano kati ya FLOYD MAYWEATHER, dhidi ya MANNY PACQUIAO utakaochezwa MAY MBILI nchini MAREKANI.
=====
Wakati huo huo bondia MADA MAUGO ametoa kichapo cha mwaka baada ya kumtandika bila huruma kwa KO Mpizani wake JAPHET KASEMBA katika mzunguko wa NANE.

=====
Mkurugenzi wa Idara ya Utamaduni kutoka wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo HERMAN MWASOKO aliomba shirika la hifadhi ya jamii NSSF kubadili mfumo wa mashindano ya kuwania KOMBE LA NSSF kutoka kwenye mtindo wa mtoano hadi ligi ili kuongeza ushindani.
MWASOKO aliyasema hayo baada ya kukabidhi zawadi kwa washindi ,huku nahodha wa TBC WARRIORS, JAMES MAPEPELE na Habari Zanzibar AMRI MAKAME wamesema walijiandaa vyema ndio maana wakaibuka na ushindi

TIMU ya TBC WARRIORS imenyakua nafasi ya tatu, IPP MEDIA imeshika nafasi ya pili wakati HABARI ZANZIBAR ndio mabingwa michuano katika soka kwa mwaka huu.
====
TIMU ya taifa ya Tanzania TAIFA STARS kesho inashuka dimbani kuibili timu ya taifa ya Malawi the flames katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa utaochezwa katika uwanja wa CCM KIRUMBA mjini MWANZA.
TAYARI KIKOSI cha wachezaji wa timu ya Taifa ya MALAWI, THE FLAMES kimewasili jijini MWANZA  kwa mchezo dhidi ya TAIFA STARS.

Mbali na wachezaji walioitwa na kocha wa MALAWI wanaocheza soka la ndani ya nchi yao pia amewajumuisha wachezaji wanaocheza soka la kulipwa  katika nchi za AFRIKA KUSINI,  JAMHURI ya KIDEMOKRASIA ya CONGO,  MSUMBIJI na ZIMBABWE.
====
STARS TAYARI KUWAKABILI MALAWI KESHO CCM KIRUMBA
Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) leo asubuhi imefanya mazoezi ya mwisho tayari kwa kuwakabili timu ya taifa ya Malawi (The Flames) mchezo utakaochezwa kesho jumapili saa 10.30 jioni katika Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

Tiketi za mchezo tayari zimeshaanza kuuzwa katika vituo vya Uwanja wa Nyamagana na uwanja wa CCM Kirumba kwa bei za sh. 5,000 kwa mzunguko, sh. 12,000 kwa jukwaa kuu na sh.20,000 kwa viti vya jukwaa kuu maalum.

Taifa Stars inashika nafasi ya 100 katika msimamo wa viwango vya FIFA vilivyotolewa mwezi Machi, huku Malawi (The Flames) wakishika wakiwa nafasi ya 91 kwenye vinago hivyo.

Akiongea na waandishi wa habari leo kaika hoteli ya La Kairo iliyopo Kirumba jijini Mwanza, kocha msaidizi wa Taifa Stars Salum Mayanga amesema kikosi chao kipo katika hali nzuri , na sasa kilichobakia ni mchezo wenyewe wa kesho.

Mayanga amesema vijana wake wote 22 waliopo kambini wapo fiti, wamefanya mazoezi kwa siku tano katika Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza, wachezaji wapo kwenye ari na morali ya juu, kikubwa wanachosubiri ni kesho tu kushuka dimbani kusaka ushindi.

Aidha Mayanga amewaomba wapenzi wa mpira wa miguu waliopo jijini Mwanza na mikoa ya jirani ya kanda ya ziwa, kujitokeza kwa wingi kesho uwanjani kuja kuwapa sapoti vijana kwa kuwashangilia muda wote wa mchezo.

Tayari waamuzi na kamishina wa mchezo wameshawasili jijini Mwanza, mwamuzi wa kati atakua ni Munyazinza Gervais kutoka nchini Rwanda, akisaidiwa na mshika kibendera wa kwanza Hakizimana Ambroise (Rwanda), mshika kibendera wa pili Niyitegeka Bosco (Rwanda), mwamuzi wa akiba  Martin Saanya kutoka Morogoro huku na Kamishina wa mchezo ni Afred Rwiza kutoka Mwanza.
Mshambuliaji wa TAIFA STARS ,MBWANA SAMATTA AKISHANGILIA BAO

Wednesday, July 9, 2014

SIMBA IMEANZA MAZOEZI



Katibu mkuu wa shirikisho la ngumi za ridhaa nchini BFT, MAKORE MASHANGA ametoa wito kwa wadau wa michezo kuisadia timu ya taifa ya ngumi  iliyopo kambini  KIBAHA  kujiandaa na mashindano ya JUMUIYA ya MADOLA yanayotarajiwa kuanza JULY 23 jijini GLASSGOW, SCONTLAND.
MASHANGA amesema wadau wengi wa michezo hujitokeza kupongeza timu wakati inaporejea kutoka kwenye michezo kwa kutafuta sifa na kuzisahau timu hizo wakati wa maadalizi yake.
Timu ya taifa ya ngumi  imeweka kambi KIBAHA na inanolewa na makocha HASSAN MZONGE na JONATHAN MWAKIPESILE baada kumaliza kambi ya mazoezi nchini CHINA na UTURUKI.
=====
Mkoa wa kimichezo wa TEMEKE umeandaa mashindano ya ngumi ya kimataifa yatakayoshirikisha  mabondia  kutoka nchi za ZAMBIA, KENYA na UGANDA,mashindano hayo yatafanyika mwezi SEPTEMBA jijini DSM.
Mwenyekiti wa chama cha ngumi mkoa wa kimichezo wa TEMEKE, SAID OMAR maarufu GOGO POA  na kocha wa ngumi kutoka Kenya , MUSSA BENJAMIN wamesema mashindano hayo yanalenga kuimarisha mchezo huo kwa nchi za Afrika mashariki.
Nao mabondia JOHN DAUDI na ALLEN FLEURY wamejigamba kufanya vyema katika mashindano hayo.
====


KLABU ya simba ya jijini DSM imeanza mazoezi yake leo katika GYM iliyoko TEMEKE jijini DSM.
Ofisa Habari wa SIMBA ,ASHA MUHAJI amsema kuwa wamejipanga kuhakikisha wanafanya vizuri katika msimu ujao ligi kuu ya VODACOM Tanzania Bara.PAUSE
kocha wa  simba  ZDRAVKO LOGARUSIC inatarajiwa kutua nchini siku ya ijumaa tayari kujiunga na timu hiyo kwa maandalizi ya msimu ujao wa ligi.
====

KIINGILIO MECHI YA TAIFA STARS, MSUMBIJI 7,000/-

KIINGILIO MECHI YA TAIFA STARS, MSUMBIJI 7,000/-
Kiingilio cha chini cha mechi kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Msumbiji (Mambas) itakayochezwa Julai 20 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kitakuwa sh. 7,000.

Tiketi zinapatikana kwa mfumo wa elektroniki kupitia M-PESA. Kiingilio hicho kwa ajili ya viti vya rangi ya rangi ya chungwa, kijani na bluu. Viingilio katika maeneo mengine vitatangazwa baadaye.

Mshabiki ili apate tiketi anatakiwa kutumia M-PESA kwa kupiga *150*00# kisha bonyeza 4, ingiza namba ya kampuni 173399 kisha weka 7000 kwenye namba ya kumbukumbu ya malipo, na weka 7000 kama kiasi cha bei ya tiketi na mwisho weka namba yao ya siri.

Baada ya hapo utapokea ujumbe wenye orodha ya vituo vya MaxMalipo kwa ajili ya kuchukulia tiketi ukiwa na namba ya uhakiki wa malipo yako.

Vituo vya kuchukulia tiketi ni mgahawa wa Steers uliopo mtaa wa Samora/Ohio, maduka makubwa ya Uchumi Supermarket (Quality Centre, Tabata Segerea na kituo cha daladala Makumbusho), Sheer Illutions (Millennium Tower na Mlimani City), maduka makubwa ya TSN Supermarket (City Centre, Kibo Tegeta na Upanga).

Vodashop (Ubungo na Mill Pamba), Shop Mwenge (Born to Shine), Puma Petrol Station (Mwenge na Uwanja wa Ndege), Engen Petrol Station (Mbezi Beach), Big Bon Petrol Station (Kariakoo, Sinza Mori, Mbagala na Temeke), YMCA (Posta Mpya), City Sports Lounge (Posta), Uwanja wa Taifa) na ofisi za TFF (PPF Tower).  

BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

KIINGILIO MECHI YA TAIFA STARS, MSUMBIJI 7,000/-

KIINGILIO MECHI YA TAIFA STARS, MSUMBIJI 7,000/-
Kiingilio cha chini cha mechi kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Msumbiji (Mambas) itakayochezwa Julai 20 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kitakuwa sh. 7,000.

Tiketi zinapatikana kwa mfumo wa elektroniki kupitia M-PESA. Kiingilio hicho kwa ajili ya viti vya rangi ya rangi ya chungwa, kijani na bluu. Viingilio katika maeneo mengine vitatangazwa baadaye.

Mshabiki ili apate tiketi anatakiwa kutumia M-PESA kwa kupiga *150*00# kisha bonyeza 4, ingiza namba ya kampuni 173399 kisha weka 7000 kwenye namba ya kumbukumbu ya malipo, na weka 7000 kama kiasi cha bei ya tiketi na mwisho weka namba yao ya siri.

Baada ya hapo utapokea ujumbe wenye orodha ya vituo vya MaxMalipo kwa ajili ya kuchukulia tiketi ukiwa na namba ya uhakiki wa malipo yako.

Vituo vya kuchukulia tiketi ni mgahawa wa Steers uliopo mtaa wa Samora/Ohio, maduka makubwa ya Uchumi Supermarket (Quality Centre, Tabata Segerea na kituo cha daladala Makumbusho), Sheer Illutions (Millennium Tower na Mlimani City), maduka makubwa ya TSN Supermarket (City Centre, Kibo Tegeta na Upanga).

Vodashop (Ubungo na Mill Pamba), Shop Mwenge (Born to Shine), Puma Petrol Station (Mwenge na Uwanja wa Ndege), Engen Petrol Station (Mbezi Beach), Big Bon Petrol Station (Kariakoo, Sinza Mori, Mbagala na Temeke), YMCA (Posta Mpya), City Sports Lounge (Posta), Uwanja wa Taifa) na ofisi za TFF (PPF Tower).  

BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

KIINGILIO MECHI YA TAIFA STARS, MSUMBIJI 7,000/-

KIINGILIO MECHI YA TAIFA STARS, MSUMBIJI 7,000/-
Kiingilio cha chini cha mechi kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Msumbiji (Mambas) itakayochezwa Julai 20 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kitakuwa sh. 7,000.

Tiketi zinapatikana kwa mfumo wa elektroniki kupitia M-PESA. Kiingilio hicho kwa ajili ya viti vya rangi ya rangi ya chungwa, kijani na bluu. Viingilio katika maeneo mengine vitatangazwa baadaye.

Mshabiki ili apate tiketi anatakiwa kutumia M-PESA kwa kupiga *150*00# kisha bonyeza 4, ingiza namba ya kampuni 173399 kisha weka 7000 kwenye namba ya kumbukumbu ya malipo, na weka 7000 kama kiasi cha bei ya tiketi na mwisho weka namba yao ya siri.

Baada ya hapo utapokea ujumbe wenye orodha ya vituo vya MaxMalipo kwa ajili ya kuchukulia tiketi ukiwa na namba ya uhakiki wa malipo yako.

Vituo vya kuchukulia tiketi ni mgahawa wa Steers uliopo mtaa wa Samora/Ohio, maduka makubwa ya Uchumi Supermarket (Quality Centre, Tabata Segerea na kituo cha daladala Makumbusho), Sheer Illutions (Millennium Tower na Mlimani City), maduka makubwa ya TSN Supermarket (City Centre, Kibo Tegeta na Upanga).

Vodashop (Ubungo na Mill Pamba), Shop Mwenge (Born to Shine), Puma Petrol Station (Mwenge na Uwanja wa Ndege), Engen Petrol Station (Mbezi Beach), Big Bon Petrol Station (Kariakoo, Sinza Mori, Mbagala na Temeke), YMCA (Posta Mpya), City Sports Lounge (Posta), Uwanja wa Taifa) na ofisi za TFF (PPF Tower).  

BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

Tuesday, July 30, 2013



MTIHANI WA UWAKALA WA WACHEZAJI, MECHI SEPT 26
Mtihani wa uwakala wa wachezaji (players agent) na uwakala wa mechi (match agent) wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) utafanyika Alhamisi ya Septemba 26 mwaka huu saa 4 kamili asubuhi kwenye ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

Kutakuwa na jumla ya maswali 20 kwenye mtihani huo, 15 yanatoka FIFA kuhusiana na kanuni za kimataifa za mpira wa miguu na matano yatatoka TFF kuhusiana na kanuni mbalimbali zinazotawala mchezo huo nchini.

Kwa ambao wangependa kufanya mtihani huo utakaokuwa katika lugha ya Kiingereza ambayo ni moja kati ya lugha nne rasmi za FIFA wanatakiwa kujisajili TFF kwa ada ya dola 50 za Marekani ambapo watapewa utaratibu na maeneo ambapo mtihani huo unalenga.

Mtihani huo utafanyika saa 4 kamili asubuhi, na muda wa kufanya mtihani hautazidi dakika 90.

Mpaka sasa Tanzania ina mawakala watano wa wachezaji wanaotambuliwa na FIFA. Mawakala hao ni John Ndumbaro, Mehdi Remtulla, Ally Saleh, Yusuf Bakhresa na Said Tully.

WAAMUZI VPL KUFANYA MTIHANI WA UTIMAMU WA MWILI
Waamuzi wote wa daraja la kwanza (Class I) wanaotaka kuchezesha Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) msimu wa 2013/2014 wanatakiwa kuhudhuria mtihani wa utimamu wa mwili (physical fitness test) utakaofanyika katika vituo viwili.

Mtihani huo utafanyika Agosti 12,13 na14 mwaka huu katika vituo vya Dar es Salaam na Morogoro. Kituo cha Mwanza kitahusisha waamuzi kutoka mikoa ya Geita, Kagera, Katavi, Kigoma, Manyara, Mara, Mwanza, Shinyanga, Simiyu, Singida na Tabora.

Kituo cha Dar es Salaam kitahusisha waamuzi kutoka mikoa ya Arusha, Dar es Salaam, Dodoma, Iringa, Kilimanjaro, Lindi, Mbeya, Morogoro, Mtwara, Njombe, Pwani, Ruvuma na Tanga.

Washiriki wote wanakumbushwa kuwa ni lazima wafuate utaratibu huo wa vituo, na si vinginevyo. Pia waamuzi waliofungiwa (sio maisha) wanatakiwa kushiriki katika mtihani huo.

RATIBA LIGI DARAJA LA KWANZA AGOSTI 14
Ratiba ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu wa 2013/2014 inayoshirikisha timu 24 zilizo katika makundi matatu zikicheza kwa mikondo miwili (nyumbani na ugenini) inatarajiwa kutolewa Agosti 14 mwaka huu.

Kundi A linaundwa na timu za Burkina Moro ya Morogoro, JKT Mlale (Ruvuma), Kimondo SC (Mbeya), Kurugenzi Mufindi (Iringa), Majimaji (Ruvuma), Mkamba Rangers (Morogoro), Polisi (Iringa) na Polisi (Morogoro).

African Lyon (Dar es Salaam), Friends Rangers (Dar es Salaam), Green Warriors (Dar es Salaam), Ndanda (Mtwara), Polisi (Dar es Salaam), Tessema (Dar es Salaam), Transit Camp (Dar es Salaam) na Villa Squad (Dar es Salaam) zinaunda kundi B.

Timu za kundi C ni JKT Kanembwa (Kigoma), Mwadui (Shinyanga), Pamba (Mwanza), Polisi (Dodoma), Polisi (Mara), Polisi (Tabora), Stand United (Shinyanga) na Toto Africans (Mwanza).

Tunapenda kukumbusha kuwa dirisha la usajili kwa madaraja yote ni moja ambapo usajili wa hatua ya kwanza ni kuanzia Juni 15 hadi Agosti 3 mwaka huu wakati hatua ya pili ni Agosti 14 hadi 29 mwaka huu. Dirisha dogo litafunguliwa Novemba 15 hadi Desemba 15 mwaka huu.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)