Katibu mkuu wa shirikisho la ngumi za ridhaa nchini
BFT, MAKORE MASHANGA ametoa wito kwa wadau wa michezo kuisadia timu ya taifa ya
ngumi iliyopo kambini KIBAHA kujiandaa na mashindano ya JUMUIYA ya MADOLA
yanayotarajiwa kuanza JULY 23 jijini GLASSGOW, SCONTLAND.
MASHANGA amesema wadau wengi wa michezo hujitokeza
kupongeza timu wakati inaporejea kutoka kwenye michezo kwa kutafuta sifa na kuzisahau
timu hizo wakati wa maadalizi yake.
Timu ya taifa ya ngumi imeweka kambi KIBAHA na inanolewa na makocha HASSAN
MZONGE na JONATHAN MWAKIPESILE baada kumaliza kambi ya mazoezi nchini CHINA na
UTURUKI.
=====
Mkoa wa kimichezo wa TEMEKE umeandaa mashindano ya
ngumi ya kimataifa yatakayoshirikisha mabondia
kutoka nchi za ZAMBIA, KENYA na UGANDA,mashindano hayo yatafanyika mwezi
SEPTEMBA jijini DSM.
Mwenyekiti wa chama cha ngumi mkoa wa kimichezo wa TEMEKE,
SAID OMAR maarufu GOGO POA na kocha wa
ngumi kutoka Kenya , MUSSA BENJAMIN wamesema mashindano hayo yanalenga kuimarisha
mchezo huo kwa nchi za Afrika mashariki.
Nao mabondia JOHN DAUDI na ALLEN FLEURY wamejigamba
kufanya vyema katika mashindano hayo.
====
KLABU ya simba ya jijini DSM imeanza mazoezi yake
leo katika GYM iliyoko TEMEKE jijini DSM.
Ofisa Habari wa SIMBA ,ASHA MUHAJI amsema kuwa wamejipanga
kuhakikisha wanafanya vizuri katika msimu ujao ligi kuu ya VODACOM Tanzania
Bara.PAUSE
kocha wa
simba ZDRAVKO LOGARUSIC inatarajiwa
kutua nchini siku ya ijumaa tayari kujiunga na timu hiyo kwa maandalizi ya
msimu ujao wa ligi.
====
No comments:
Post a Comment