Tuesday, August 31, 2010



washiriki wa big brother all stars wakipeyana moyo

Habari za michezo za kimataifa za leo

ALGERIA yaamini itafanya vizuri mchezo dhidi ya TAIFA STARS
WAKATI timu ya taifa, TAIFA STARS ikiwa njiani kuelekea ALGIERS kwaajili ya mchezo wa kombe la mataifa ya Afrika dhidi ya timu ya ALGERIA, kocha wa timu ya taifa ya ALGERIA RABAH SAADANE amesema kufungwa na GABON katika mchezo wa kirafiki haimaanishi kuanza vibaya katika mchezo dhidi ya TAIFA STARS.
Kauli ya kocha huyo imeungwa mkono na beki wa kimataifa wa ALGERIA, MADJID BOUGHERRA ambaye naye anaamini kuwa kushindwa kwao nyumbani kwa magoli MAWILI kwa MOJA sio ishara ya kufungwa na STARS.
Miongoni mwa sababu alizozitaja zilizosababisha kufungwa na GABON ni kutokana na kwanza wachezaji wengi walikuwa hawana mazoezi na ni mwanzo wa msimu .
ALGERIA ambayo ilishiriki mashindano ya kombe la dunia ya mwaka huu nchini AFRIKA KUSINI inaanza kibarua chake kwa kucheza na TAIFA STARS mchezo wa kutafuta tiketi ya kucheza mashindano ya kombe la mataifa ya Afrika AFCON ya mwaka 2012.
==
FRANCISCO VARALLO afariki dunia
KATI ya wachezaji wachache wakongwe ambao walicheza katika mashindano ya kwanza ya kombe la dunia akiwemo FRANCISCO VARALLO wa ARGENTINA amefariki dunia akiwa na umri wa miaka MIA MOJA.
Picha ya VIDEO ya VARALLO ni kwa hisani ya mtandao kupitia YOU TUBE ambapo aliichezea timu yake ya taifa ya ARGENTINA katika mchezo wa fainali dhidi ya timu ya URUGUAY, mchezo uliochezwa URUGUAY mwaka 1930 na timu yake kufungwa magoli MANNE kwa MAWILI.
Wakati wa uchezaji wake VARALLO aliweza kuifungia timu yake ya BOCA JUNIORS magoli 194 rekodi ambayo imevunjwa mwaka huu na mshambuliaji wa timu hiyo MARTIN PALERMO.
Wakati wa mahojiano mwaka huu kabla ya kifo chake na FIFA , kuadhimisha miaka 100, VARALLO alisema anakumbuka vilivyo mchezo wa fainali wa mwaka 1930 na kubainisha kuwa ulimnyong`onyesha na hata kulia kwa kufungwa na URUGUAY.
VARALLO aliachana na masuala ya soka baada ya kuumia akiwa na umri wa miaka THELATHINI na kuanza kufanya kazi ya ukocha na timu za vijana za BOCA JUNIOR.
==
BOB BRADLEY asaini kuifundisha Marekani
KOCHA wa timu ya taifa ya MAREKANI, BOB BRADLEY amesaini makataba wa miaka MINNE kuendelea kuifundisha timu ya taifa ya MAREKANI kwa kipindi cha miaka MINNE ijayo.
Kutia saini kwa kocha huyo kunamaliza tetesi kuwa kocha huyo anakwenda kuifundisha timu ya ASTON VILLA.
BRADLEY ambaye aliipeleka MAREKANI raundi ya pili ya mashindano ya kombe la dunia ya Afrika kusini sasa atakaa katika timu hiyo hadi mwaka 2014.
BRADLEY alichukua jukumu la kuifundisha MAREKANI mwaka 2006 kutoka kwa BRUCE ARENA na BRADLEY ameisaidia MAREKANI kutoka sare na timu za ENGLAND na SLOVENIA kabla ya kuifunga ALGERIA goli MOJA kwa SIFURI na kuwa timu ya kwanza katika kundi lake la C na iliondolewa na GHANA kwa kuifungwa magoli MAWILI kwa MOJA.
==
Manyota wa TENNIS washinda raundi ya kwanza
Mchezaji ELENA BALTACHA amefanikiwa kuanza vizuri mashindano ya TENNIS ya wazi ya MAREKANI baada ya kumrarua PETRA MARTIC kwa seti 6-2 6-2 katika mchezo wa kwanza wa mashindano hayo.
BALTACHA, ambaye ni mchezaji bora wa 57 ulimwenguni anatarajia kupanda chati hiyo na kufikia namba 50.
Baada ya ushondi huo sasa BALTACHA atapambana na Kvitova baada ya KVITOVA naye kumfunga mwenzake LUCIE HRADECKA kwa seti 6-4 7-5.
Huku VENUS WILLIAMS naye akifanikiwa kumfunga ROBERTA VINCI kwa seti 6-4na 6-1.
Naye bingwa wa mara tano katika mashindano hayo ya MAREKANI upande wa wanaume ROGER FEDERER amefanikiwa kushinda mchezo wake wa awali kwa kumchakaza muajentina BRIAN DABUL kwa ushindi wa seti 6-1 6-4 6-2.
Ushindi wa FEDERER unamfanya sasa apambane na mjeruman, ANDREAS BECK katika raundi ya pili.
Wengine walioshinda michezo yao ni pamoja na MARIN CILIC na JUAN CARLOS FERRERO.
==
Timu za Afrika zafanya vibaya mashindano ya kikapu ya dunia.
Wawakilishi wa bara la Afrika katika mashindano ya dunia ya mchezo wa kikapu , TUNISIA na ALGERIA zimefanya vibaya katika michezo yao.
TUNISIA imefungwa na IRAN kwa vikapu 58 kwa 71, huku ARGERNTINA ikiigaragaza vikapu 91 kwa 70 timu ya Angola.
Huku BRAZIL ikichapwa na Marekani kwa vikapu 70 kwa 68, na AUSTRALIA ikirarua timu ya UJERUMAN kwa vikapu 78 kwa 43, CROATIA nayo ikachapwa na SLOVENIA kwa vikapu 91 kwa 84.
==

Usafi kinondoni


Gari la likizoa taka katika eneo la Mwembechai jijini DSM leo asubuhi,angalao manispaa ya kinondoni imeanza kungamala juu ya kuiweka manispaa hiyo katika hali ya usafi

TWIGA STARS Kambini

Timu ya taifa ya soka ya wanawake TWIGA STARS itacheza michezo minne ya kimataifa dhidi ya timu ya taifaya AFRIKA YA KUSINI Banyana Banyana na ZIMBABWE mwezi ujao kujiweka sawa na fainali za kombe la matifa ya Afrika kwa wanawake yanayotarajiwa kufanyika mwezi OCTOBA nchini Afrika ya kusini.
Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kutangaza kikosi cha wachezaji 25 wa timu hiyo wanaoanza kambi kesho, Kocha mkuu wa TWIGA STARS, CHARLESE MKWASA, amesema wameamua kuanza kambi mapema igawa hawajui tarehe ya kuanza kwa mashindano hayo ya Afrika kwa wanawake.
Mkwasa amesema TWIGA STARS,itacheza na Banyana Banyana septemba 29 na Oktoba 2 na pia itacheza dhidi ya ZIMBABWE Octoba 6 na 10 kwa lego la kuiweka sawa timu hiyo kabla ya mashindano hayo makubwa barani Afrika kwa wanawake na kwamba michezo hiyo itachezwa jijini DSM.Fainali za soka kwa mataifa ya Afrika kwa wanawake yatazishirikisha timu za taifa za Algeria,Ghana,Tunisia,Equitoria Gine,Tanzania,Cameroon na wenyeji Afrika ya Kusini na yanatarajiwa kutimua vumbi mwezi Okatoba

Simba kulishitaki mwanasport


Kamati ya utendaji wa klabu ya Simba imetishia kulishitaki gazeti la michezo la Mwanasport kwa kuandika makala inayoukashifu uongozi wa klabu hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini DSM hii leo, mwenyekiti wa klabu hiyo ISMAIL ADEN RAGE amesema kamati ya utendaji ya klabu ya Simba iliyokutana jana imetoa siku kumi na nne kwa gazeti hilo kuomba radhi vinginevyo watalishitaki mahakamani na pia kudai kulipwa fidia ya shilingi bilioni moja kama litashindwa kufanya hivyo
Wakati huo huo Rage amesema klabu ya Simba itacheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Ulizi ya Kenya siku ya jumamosi kwenye uwanja wa Taifa jijini DSM ikiwa ni maadalizi ya kuikabili Azam FC katika mchezo utakaopingwa Septemba 11 katika uwanja wa taifa.
RAGE ameongeza kusema kwamba baada ya mchezo huo wachezaji wa samba watasafiri kwenda jijini mwanza ambapo watautumia uwanja wa CCM KIRUMBA kwa michezo yake ijayo ya ligi kuu Tanzania bara baada ya uwanja wa Uhuru kufungwa kwa ajili ya mategenezo.
Simba imeanza vyema kuutetea ubingwa wake baada ya kuifunga African Lyon mabao mawili kwa bila katika mchezo wa ufunguzi uliofanyika katika uwanja wa Uhuru Augosti 21.

Kocha wa netball kuwasili kesho


Kocha wa timu ya taifa ya netiboli SIMONE MACKIMIS kutoka Australia anawasili nchini kesho tayari kwa kuinoa timu hiyo inayojiandaa kushiriki mashindano ya Afrika yatakayofanyika nchini Afrika ya Kusini mwezi ujao.
Kaimu Katibu mkuu wa CHANETA, ROSE MKISI, amesema kocha SIMONE MACKIMIS atakapo wasili atajiunga moja kwa moja na kambi ya timu hiyo ambayo ipo katika shule ya sekondari ya FILBERT BAYI KIBAHA, tayari kwa kuinoa kablya kuondoka kwenda Afrika ya Kusini.
MKISI amesema igawa kocha MACKIMIS atakua na muda mfupi wa kuinoa timu hiyo lakini wanamatumaini kwamba mafunzo atakayotoa yatasaidia timu hiyo kufanya vyema katika mashindano hayo ya Afrika.
Hii itakuwa nia mara ya kwanza kwa timu ya taifa ya netiboli kunolewa na kocha wa kingeni na kwamba kama walivyo makocha wa soka,ngumi na riadha kocha MACKIMIS pia atalipwa mshahara na serikali.


Sunday, August 29, 2010

Ramadhani karimu


Hili ni kumi la pili la mwezi mtukufu wa ramadhani,waislam tushikamane



Timu ya soka ya Filbert Bayi leo inateremka dimbani kuchuana na mabingwa watetezi ST.MERYS KITENDE ya Uganda katika nusu fainali ya kwanza mchezo utakaochezwa mjini Nakuru nchini Kenya.

Nusu fainali ya pili katika soka inazikutanisha timu za soka za ST.MARKS ya Kenya itakayoshuka dimbani kumenyana na PS BABTIST ya Rwanda.

Katika netiboli timu ya Filbert Bayi inashuka dimbani katika mchezo wa nusu fainali ya kwanza dhidi ya shule ya sekondari BLESSED SACRAMENT KIMAYA YA UGANDA huku nusu fainali ya pili ikizikutanisha ST.MERYS KITENDE ya Unganda dhidi ya SHIMBA HILL YA KENYA.

Timu za Tanzania katika michezo ya mpira wa kikapu,mikono na Voliboli zote zimeshindwa kutamba na kuitinga katika hatua ya nusu fainali ya mashindano hayo.

===


Timu za kriketi za klabu ya Gymkhana ya Tanzania na ile ya jeshi la wanamaji la India zimechuana katika mchezo maalumu wa kuendeleza uhusiano wa kimichezo kati ya Tanzania na India,mechi hiyo imechezwa hii leo katika viwanja vya Gymkhana jijini DSM

mwenyekiti wa kriketi wa klabu ya Gymkhana KULBIR CUPTA na Nahodha wa timu ya wanamaji India DINESH TRIPATHI wamesema michezo hujenga urafiki na uhusiano mwema kwa wachezaji na nchi kwa ujumla

Meli ya kivita ya wanamaji wa jeshi la india imewasili Dar es Salaam hiyo jana ikiwa na lengo la kulinda amani katika bahari ya hindi.

===

Wachezaji kutoka katika vilabu sita vya gofu wamechuana hii leo kwa lengo la kuchangua wachezaji wa akiba wa timu ya taifa ya GOFU ya Tanzania.

Afisa tawala wa Chama cha gofu Tanzania TGU, SOPHIE NYANJERA, amesema wameamua kuwashindanisha wachezaji wa timu ya taifa ya Gofu na wale ambao hawapo katika timu hiyo kwa madhumuni ya kupima viwango vyao

Kwa upande wake kocha wa timu ya taifa ya GOFU FARAYI CHITENGWA amesema amefurahishwa na kiwango cha uchezaji kilicho onyeshwa na wachezaji walio nje ya timu ya taifa na ni hazina kwa timu ya taifa

Wachezaji kutoka klabu za Gymkhana DSM, ARUSHA, MFINDI na Morogoro,TPC na LUGALO wamechuana katika mashindano hayo.

===

Katika klabu bingwa Afrika timu ya Heartland ya Nigeria imenashuka dimbani kuchuana na Ismaili ya Misri mchezo utakaopingwa kwenye uwanja wa Dan Anyiam wakati katika mchezo mwingine wa kundi B Al Ahly ya MISRI itaonyeshana kazi na JS Kabylie

Msimamo kabla ya mchezo wa leo JS Kabylie inaongoza ikiwa na pointi 9 kibindoni ikifuatiwa na Al Ahly yenye pointi 4, Ismaili inashika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 3 wakati Heartland inaburuza mkia ikiwa na pointi 1

Katika kundi A Entente Setif imeinyuka Dynamos ya Zimbabwe kwa mabao matutu kwa bila huku mabingwa watetezi TP Mazembe wanateremka dimbani kumenyana na Esperance

Msimamo katika kundi A mabingwa watetezi TP Mazembe inaongoza kundi hilo ikiwa imejikusanyia pointi 7 wakati Esperance inashika nafasi ya pili ikiwa na pointi 4, E. Setif inashika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 4 wakati Dynamos inaburura mkia ikiwa na pointi zake 3.

====

Ligi kuu ya ENGLAND imeendelea hii leo kwa michezo minne kutimua vumbi katika viwanja mbalimbali,Aston Villa wamewakaribisha Everton katika uwanja wao wa nyumbani wa Villa Park huku Bolton wakimenya na Birmingham katika dimba la Reebok.

Michezo mingine majogoo wa jiji Liverpool wameshuka dimbani dhidi ya West Brom katika uwanja wake wa nyumbani wa AN FIELD huku Sunderland wakiwakaribisha Man City.

Katika michezo iliyochezwa jana ARSENAL ilichapa Black BURN kwa mabao 2-1huku mashetani wekundu MANCHESTER UNITED wakatumia vyema uwanja wao wa nyumbani wa OLD TRAFORD na kuichapa WEST HAM UNITED kwa mabao matatu kwa bila.

Michezo mingine iliyochezwa jana mabingwa watetezi CHESLEA walitoka kifua mbele baada ya kuinyuka STOKE CITY kwa mabao MAWILI kwa sifuri huku BLACK POOL ikitoka sare ya kufungana mabao mawili kwa mawili na FULHAM wakati WOLVESHAMPTON ikakabana koo na NEWCASTLE na kutoka sare ya kufungana bao moja kwa moja.

===


Thursday, August 26, 2010


Shirikisho la mpira wa miguu nchini limebadili kanunu zake za ligi na saa Ligi kuu Tanzaniza Bara itakuwa na timu kumi na nne badala ya 12 katika msimu wa 2011 /2012.
Afisa habari wa TFF Florian Kaijage amesema lego la mabadiliko hayo ya kanuni ya nne ya ligi kuu ni kuogeza ushindani kwa timu zinazoshiriki ligi hiyo kwa lego la kukuza soka hapa nchini.
Kaijage amesema katika mabadiliko hayo timu nne zitapanda daraja kutoka ligi daraja la kwanza hadi ligi kuu huku timu mbili zikireka daraja.
Ligi kuu Tanzania bara kwa sasa imekuwa na timu 12 na timu mbili zimekuwa sikishuka daraja huku timu tatu zikipanda daraja kutoka ligi daraja la kwanza hadi ligi kuu.
==
Uwanja wa UHURU tayari umeanza kufanyiwa ukarabati baada ya kufungwa kwa muda wa miezi mitatu na kuzifanya timu za ligi kuu Tanzania Bara zilizokuwa zinatumia uwanja huo kutafuta viwanja vingine.
Akizungumza na TBC mfanyakazi mmojawapo katika uwanja huo TUGE SHEMU aliyataja maaeneo yanayofanyiwa ukarabati kuwa ni mifereji ya kupitishia maji kwenye sehemu ya kuchezea yaani (pitch).
SHEMU ameyataja maeneo mengine kuwa ni kujenga uzio upande wa mashariki mwa uwanja huo na eneo la geti la upende wa kazikazini,kuezua paa la jukwaa kuu na kuweka paa jingine pamoja na kufunga viti vipya na kupaka rangi.
Timu zilizoathirika na ukarabati wa uwanja wa UHURU ni mabingwa watetezi wa ligi kuu Tanzania Bara SIMBA,mabingwa wa Ngao ya Hisani YANGA,AZAM FC,AFRICAL LYON na RUVU JKT.
==
Shirikisho la mpira wa miguu nchini limebadili kanunu zake za ligi na saa Ligi kuu Tanzaniza Bara itakuwa na timu kumi na nne badala ya 12 katika msimu wa 2011 /2012.
Afisa habari wa TFF Florian Kaijage amesema lego la mabadiliko hayo ya kanuni ya nne ya ligi kuu ni kuogeza ushindani kwa timu zinazoshiriki ligi hiyo kwa lego la kukuza soka hapa nchini.
Kaijage amesema katika mabadiliko hayo timu nne zitapanda daraja kutoka ligi daraja la kwanza hadi ligi kuu huku timu mbili zikireka daraja.
Ligi kuu Tanzania bara kwa sasa imekuwa na timu 12 na timu mbili zimekuwa sikishuka daraja huku timu tatu zikipanda daraja kutoka ligi daraja la kwanza hadi ligi kuu.
==
Uwanja wa UHURU tayari umeanza kufanyiwa ukarabati baada ya kufungwa kwa muda wa miezi mitatu na kuzifanya timu za ligi kuu Tanzania Bara zilizokuwa zinatumia uwanja huo kutafuta viwanja vingine.
Akizungumza na TBC mfanyakazi mmojawapo katika uwanja huo TUGE SHEMU aliyataja maaeneo yanayofanyiwa ukarabati kuwa ni mifereji ya kupitishia maji kwenye sehemu ya kuchezea yaani (pitch).
SHEMU ameyataja maeneo mengine kuwa ni kujenga uzio upande wa mashariki mwa uwanja huo na eneo la geti la upende wa kazikazini,kuezua paa la jukwaa kuu na kuweka paa jingine pamoja na kufunga viti vipya na kupaka rangi.
Timu zilizoathirika na ukarabati wa uwanja wa UHURU ni mabingwa watetezi wa ligi kuu Tanzania Bara SIMBA,mabingwa wa Ngao ya Hisani YANGA,AZAM FC,AFRICAL LYON na RUVU JKT.
==

Wednesday, August 25, 2010


MWILI wa aliyekuwa mwenyekiti wa shirikisho la mpira wa mikono kwa nchi za Afrika mashariki na kati (ECAHF) CECILIUS FUSI na Kanali wa jeshi la kujenga taifa kikosi cha TAU MGULANI umezikwa katika makaburi ya KINONDONI Jijini DSM.
Wakati wa mazishi yake FUSI alizikwa kwa taratibu zote za kijeshi
Marehemu atakumbukwa kwa kuhimiza michezo ambapo kabla ya kifo chake alikuwa mwenyekiti wa Shirikisho la Mpira wa Mikono Afrika Mashariki na Kati.Marehemu amecha mke DORIS FUSI pamoja na watoto TISA

MKAZI anayeishi jijini DSM, DORAH TEMU amebahatika kuibuka mshindi wa kitita cha shilingi MILIONI MIA MOJA katika shindano la kubahatisha linaloendeshwa na kampuni ya simu ya mkononi ya TIGO.

Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi fedha hizo, afisa uhusiano wa kampuni ya TIGO, JACKON MMBANDO amesema katika shindano hilo la JIKOKI jumla ya zawadi zenye thamani ya shilingi MILIONI 338, zilitolewa na kati ya hizo mshindi DORAH TEMU alifanikiwa kuwashinda washiriki wengine kwa kuwa na pointi nyingi zaidi.

Mbali na zawadi hiyo, TEMU aliwahi kunyakuwa zawadi ya fedha MILIONI MBILI na MILIONI TANO.
==

WAANDAAJI wa shindano la kutafuta nyota wa muziki katika shindano la BONGO STAR SEARCH (BSS) wamepatiwa kiasi cha shilingi MILIONI MIA MOJA na kampuni ya bia TANZANIA (TBL).
Wakati wa hafla hiyo meneja wa kinywaji cha KILIMANJARO, GEORGE KAVISHE na mratibu wa mashindano hayo RITA PAULSEN kwa nyakati tofauti wamesema mashindano ya mwaka huu yatakuwa na mabidiliko tofauti na miaka ya nyuma.
Mashindano ya kutafuta nyota wa muziki ya BONGO STAR SEARCH hufanyika kila mwaka na mshindi wa mwaka jana ni PASCHAL CASIAN kutoka MWANZA.
== == =

SHIRIKISHO la Kimataifa linalojihusisha na mazoezi ya mwili, viungo na utoaji wa elimu ya michezo la TAFISA linakusudia kutekeleza miradi ya ushirikiano na TANZANIA kupitia chuo cha Maendeleo ya michezo cha MALYA kilichopo mkoani MWANZA.

Katibu mkuu wa shirikisho la michezo kwa wote duniani, WOLFGANG BAUMANN ambaye alitembelea chuo hicho wakati wa ziara yake nchini, ambapo pia kikao cha bodi ya shirikisho hilo kilifanyika jijini DSM.

Aidha , BAUMANN amesema ndani ya chuo hicho cha MALYA kutakuwa na taasisi maalum ya utoaji wa mafunzo kwa vijana, mpango ambao utaanza mwanzoni mwa mwaka ujao na utakuwa na faida kwa nchi zilizopo katika ukanda wa nchi za Afrika mashariki na Afrika kwa ujumla.
==


MABARAZA ya michezo ya BMT na BMZ yametakiwa kufanya jitihada za kusuluhisha mgogoro wa vyama vya mchezo wa NETIBOLI visiwani ZANZIBAR na ule wa TANZANIA BARA.

Katibu Mkuu wa wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, SETH KAMUHANDA ametaka mgogoro huo umalizwe kwa faida ya mchezo huo

Katika kambi ya mazoezi inayojiandaa na mashindano ya kimataifa nchini AFRIKA KUSINI mwezi ujao , ni wachezaji wa TANZANIA BARA pekee ambao wapo katika kambi hiyo huku wachezaji kutoka ZANZIBAR wakiwa hawajaripoti katika kambi hiyo kutokana na madai yaliyochangiwa na mgogoro wa viongozi wa CHANEZA na CHANETA.

Katika hatua nyingine, katibu KAMUHANDA ametolea ufafanuzi kuwa timu ya soka ya wanawake ya TWIGA STARS wanaidai shirikisho la soka nchini TFF malimbikizo yao ya fedha ya nyuma na hayahusiani na msaada uliotolewa na rais JAKAYA KIKWETE kwa timu hiyo.

Fedha ambazo rais KIKWETE ametoa kama msaada kwa timu hiyo ni MILIONI HAMSINI fedha ambazo zitatumika kwa ajili ya kambi ya matayarisho ya timu hiyo inayojiandaa na mashindano ya kombe la mataifa ya Afrika yatakayofanyika nchini AFRIKA KUSINI mwezi OKTOBA mwaka huu.

Tuesday, August 24, 2010

Tanzanian artist, Witness has been nominated in the Most Gifted Female Video category with her song ‘Attention Please’.
May I kindly request that we give her all the support she needs.

Africa’s most gifted set to take flight with 2010 Channel O Music Video Awards
Africa’s most gifted musicians are set to take flight with the just-announced nominations for the 2010 Channel O Music Video Awards, sponsored by MTN.
Like the pan-African vision of the channel that spawned the awards the nominees in this year’s Channel O Music Video Awards are confirmation of the exceptional music talent that is being created in so many parts of Africa . From Hip-Hop to Dancehall; from Kwaito to Afro Pop; from Ghana to Angola ; from Namibia to Kenya - and so many other countries and music genres! - it’s impossible not to be impressed by the nominees in this year’s event and what they say about the healthy state of Africa’s contemporary music scene.

“What’s especially pleasing this year is the reach of the nominees,” says Yolisa Phahle, Channel Director of M-Net’s Special Interest Channels. “It’s great to see a country like Angola make its presence felt and there is a strong showing by artists from Ghana and Kenya as well. It’s now up to the artists and fans to mobilise in order to secure votes for the music videos that they believe deserve the honour of a Channel O Music Video Award. In the end, it’s the fans who decide who walks away with the statuette.”

In total, the 2010 Channel O Music Video Awards are spread across 14 categories – with five nominees in each category, except Most Gifted Video of the Year which features six nominees. After his high profile in the recent 2010 FIFA World Cup it’s no surprise that Somalian-born rapper, K’Naan, is one of the leading nominees this year with three nods. His video for “T.I.A.” has earned him a nomination in the Most Gifted Video of the Year category as well as for Most Gifted Hip-Hop Video and Most Gifted Male Video. The latter category is likely to be hard-fought and alongside K’Naan, it features Nigeria’s Wande Coal (“Bumper To Bumper”), Nigeria’s Banky W (“Strong Thing”), Botswana’s Zeus (“Champagne Music”) and South Africa’s Black Coffee (with the video for “Juju” featuring Bantwini).

Also notching up three nominations is Nigeria ’s M.I. whose video with Djinee – “Safe” – has ignited the continent-wide career of the rapper. Alongside Most Gifted Video of the Year, “Safe” sees M.I. in the running for Most Gifted Newcomer and Most Gifted Duo, Group or Featuring. Watch out too for Djinee, M.I.’s collaborator on the track, who is also a contender for Most Gifted Newcomer with the video “Overkilling”. Other nominees in this closely-watched category – designed to honour Africa’s emerging talent – is Mozambique’s Gabriela with “Mina Nawena”, and two new South African talents: Octave Couplet and Hydro with “Do Ur Thang” and L-Tido and T-P’s “Calling”.

Mozambique features strongly in this year’s nominees list with Gabriela and Dama Do Bling (“Casar Com Outra”) up for Most Gifted Southern Video. Their compatriot Lizha James represents Africa ’s gifted female artists in the Most Gifted Video of the Year nominees list and her song with Loyiso – “Vou Te Atacar’ – has also earned the Mozambican a nomination for Most Gifted Female Vide
Most Gifted Female Video additionally has Nigeria ’s Mo’Cheddah featuring Othello (“If You Want Me”), South Africa ’s Thembi Seete (“Free”), Kenya ’s Witness (“Attention Please”) and Nigeria ’s Kenny Saint Brown featuring Da Grin (Turn Me Around”). In a poignant confirmation of his rising talent, the late Nigerian rapper, Da Grin – who was tragically killed in a car accident in April this year – also features as a nominee in the Most Gifted West Video category with his hugely popular song “Pon Pon Pon
Ghana’s D-Black and Kwaku-T are another leading contender with their video “Breathe”. It’s up for Most Gifted Video of the Year and Most Gifted Hip Hop Video. Samini also represents the West African country in the category Most Gifted Ragga Dancehall Video with the video “Sweet Mistake” whilst Ghana ’s Jon Germain is in the running for a Most Gifted R&B Channel O Music Video Award with the video “In My Head”.
Another nominee for Most Gifted R&B is Anselmo Ralph whose “Domesticado” flies the flag for Angola along with Big Nelo whose “Hoje E Surra” is up for Most Gifted Dance Video.
Alongside these nominees, there are plenty of others who have earned multiple nods including Kenya ’s Nameless whose collaboration with Hadiba “Sunshine” is up for Most Gifted Afro Pop and Most Gifted East Video.
The 2010 Channel O Music Video Awards are set to take place on Thursday 4 November at the Sandton Convention Center , Johannesburg in South Africa .
Voters can have their say by voting via SMS [SMS the artist code to the number [+27 83 920 8406], on the web (www.mva.channelo.tv) or on their mobile phones [channelo.tv or on MXiT].
Aliyekuwa Kanali wa jeshi la kujenga taifa kikosi cha TAU MGULANI na mwenyekiti wa shirikisho la mpira wa mikono AFRIKA MASHARIKI NA KATI CECILIUS FUSI ambaye amefariki dunia jumapili iliyopita mwili wake unatarajiwa kuzikwa kesho katika makaburi ya kinondoni Jijini DSM.


Mkurungezi wa mtendaji wa TTB, ALOYCE NZUKI amesema bodi ya Utalii Tanzania katika harakati zake za kutangaza vivutio vya utalii vya Tanzania kimataifa imenunua nafasi ya kutangaza kwenye viwanja vya nyumbani vya timu sita zilizopo kwenye ligi kuu ya UINGEREZA kwa michezo 114 kuanzia AUGOSTI 14 hadi MAY 22 mwakani


Afisa habari wa Yanga LUIS SENDEU akiongea na waandishi wa habari hiyo jana,kushoto kwake ni Afisa habari wa Simba Clifford Ndimbo
Bondi ya Utalii Tanzania TTB imepanga kutumia shilingi milioni mia nane kutanganza vivutio vya utalii katika ligi kuu ya soka ya Uingereza.
Mkurungezi wa mtendaji wa TTB, ALOYCE NZUKI amesema bodi ya Utalii Tanzania katika harakati zake za kutangaza vivutio vya utalii vya Tanzania kimataifa imenunua nafasi ya kutangaza kwenye viwanja vya nyumbani vya timu sita zilizopo kwenye ligi kuu ya UINGEREZA kwa michezo 114 kuanzia AUGOSTI 14 hadi MAY 22 mwakani (PAUSE)

NZUKI alivitaja viwanja na timu hizo sita kuwa ni BLACKBURN ROVERS inayaotumia uwanja wa EWOOD PARK,NEWCASTLE UNITED inayotumia uwanja wa ST.JAMES PARK,STOKE CITY inayotumia dimba la BRITANIA,SUNDERLAND inayotumia uwanja wa LIGHT,WEST BROMWICH ALBION inayotumia uwanja wa THE HAWTHORNS na WOLVERTHAMTON inayotumia dimba la MALINEUX.

NZUKI mesema vivutio vya utalii vinavotangazwa katika viwanja hivyo ni Mlima KILIMANJARO, ZANZIBAR na SERENGETI na tayari matangazo hayo yameonekana katika mchezo kati ya BLACKBURN ROVERS dhidi ya EVERTON uliochezwa kwenye dimba la EWOOD PARK AUGOSTI 14.

==

Watani wa jadi,klabu za Simba na Yanga zimegomea mgao wa shilingi milioni THELATHINI NA MBILI kwa kila timu uliotokana na mechi ya Ngao ya Hisani na kudai hauendani na gharama za maandalizi ya mchezo huo.

Afisa Habari wa Simba CLIFORD NDIMBO na yule wa Yanga LUIS SENDEU wamesema timu zao haziko tayari kuchukua mgawanyo huo na endapo TFF haitachukua uamuzi wa kuuboresha uendane na kusudiao lao kuna uwezekano mkubwa wa timu hizo kugoma kuendelea kushiriki ligi kuu Tanzania Bara.
Klabu hizo zimedai kutokuwa na imani na shirikisho la soka nchini TFF, kufuatia kuendelea kutotendewa haki katika mapato hasa michezo inayozikutanisha timu hizo mbili ambayo huingiza mapato mengi kutokana na idadi kubwa ya mashabiki wa soka wanaojitokeza uwanjani kushuhudia mpambano kila timu hizo zinapoteremka dimbani kuchuana.
katika mchezo wa Ngao ya Hisani uliopigwa Jumatano iliyopita katika uwanja wa taifa jijini DSM jumla ya shilingi milioni MIA MBILI NA ISHIRINI NA MBILI zilipatikana lakini klabu hizo zimeambulia mgao wa shilingi milioni 32 kila moja.

====
Aliyekuwa Kanali wa jeshi la kujenga taifa kikosi cha TAU MGULANI na mwenyekiti wa shirikisho la mpira wa mikono AFRIKA MASHARIKI NA KATI CECILIUS FUSI ambaye amefariki dunia jumapili iliyopita mwili wake unatarajiwa kuzikwa kesho katika makaburi ya kinondoni Jijini DSM.

Wakizungumza katika msiba huo baba wa marehemu EDWARD FUSI na MARIETA FUSI wamesema msiba huo ni pigo kwa familia pamoja na watu wa करिबू
Baba wa marehemu FUSI amesema wanatarajia kuzika mwili wa marehemu CECILIUS FUSI kesho baada ya watoto wa marehemu ambao wanaishi nje ya nchi kuwasili nchini hii leo lakini iwapo hawatowasili mazishi yatafanyika na baadaye msiba utahamishiwa mjini Songea kwa wazazi wa marehemu.
Marehemu atakumbukwa kwa kuhimiza michezo ambapo kabla ya kifo chake alikuwa mwenyekiti wa Shirikisho la Mpira wa Mikono Afrika Mashariki na Kati.
Marehemu amecha mke DORIS FUSI pamoja na watoto tisa.

=====

MASHINDANO ya kimataifa ngumi za ridha maarufu kama mabingwa wa mabingwa yanaanza mchana huu katika ukumbi wa DDC MLIMANI CITY jijini DSM huku mashindano hayo yakiwa yanakabiliwa na ukata mkubwa ngumi kifedha.
Mashindano hayo yanashirikisha nchi SITA, zikiwemo, KENYA, UGANDA, RWANDA, BOTSWANA, MAURITIUS na wenyeji TANZANIA.
Ukata wa fedha unatokana na mabondia kutoka nchini KENYA na UGANDA kutolewa katika Hotel waliokuwa wamefikia na kuhamishiwa Hotel ya bei rahisi.
==
BINGWA wa mchezo wa Golf duniani TIGER WOODS ametalikiana na mkewe ELIN NORDEGREN.
Hayo yamefahamika katika taarifa iliyotumwa kwenye mtandao wa mchezaji golf huyo namba moja duniani.
Kila mmoja alibainisha kwa kudai kuwa wanasikitika kuwa ndoa yao imefikia tamati na kutakiana kila la heri .
Hata hivyo wanasema watasaidiana majukumu ya kulea watoto wao wawili.
Suala la kugawana fedha bado halijawekwa wazi lakini taarifa katika vyombo vya habari nchini MAREKANI zinasema NORDEGREN huenda akaondoka na dola za kimarekani MILIONI 100.
WOODS amekuwa na matatizo kwenye ndoa yake baada ya kukiri kuwa na uhusiano wa kimapenzi nje ya ndoa.
==

NAIBU waziri mkuu wa ENGLAND, NICK CLEGG amewaambia wakaguzi wa viwanja wa FIFA kuwa ENGLAND ni zaidi ya nchi nyingine zilizoomba kuandaa mashindano ya kombe la dunia kwa mwaka 2018.
CLEGG, ameaysema hayo wakati maofisa hao wa FIFA wakiwa nchini humo kwa siku NNE kukagua baadhi ya viwanja na baadae kutoa ripoti kama ENGLAND wataweza kuandaa au la.
DESEMBA 2 mwaka huu waandaaji wa mashindano ya kombe la dunia kwa mwaka 2018 na 2022 watatajwa ambapo kwa mwaka 2014 nchi ya BRAZIL ndiyo itakayoandaa mashindano hayo baada ya mwaka huu kufanyika nchini AFRIKA KUSINI kwa mara ya kwanza katika bara la Afrika.
Katika kupambana na uandaaji wa mashindano hayo inaonekana ENGLAND imekuwa ikipata upinzani mkubwa kutoka kwa nchi ya URUSSI.
Ujumbe wa watu SITA ukiongozwa na rais wa chama chya soka nchini CHILE, HAROLD MAYNE-NICHOLLS ulipata fursa ya kutembea kutoka eneo la DOWNING STREET hadi uwanja wa WEMBLEY ambapo walikutana na kocha wa timu ya taifa ya ENGLAND, FABIO CAPELLO.
Viwanja ambavyo vinaangaliwa na wakaguzi hao ni pamoja na kile cha OLYMPIK, uwanja wa ARSENAL wa EMIRATES, WHITE HART LANE, MK, NOTTINGHAM FOREST.
==

MCHEZAJI wa TENNIS wa DENMARK, CAROLINE WOZNIACKI amefanikiwa kuibuka na ushindi katika mashindano ya kombe la ROGERS kwa kumshinda VERA ZVONAREVA kwa seti 6-3 6-2.
Kila upande uliweza kuanza vizuri kwa kushambuliana kabla ya WOZNIACKI kubadili mchezo na kuanza kupata pointi za mfululizo.
Kabla ya mchezo huo WOZNIACKI alifanikiwa kumfunga SVETLANA KUZNETSOVA katika mchezo uliocheleweshwa kutokana na mvua.
WOZNIACKI kwa sasa anashikilia namba MBILI kwa ubora wa kiwango cha TENNIS.
==

Monday, August 23, 2010


mchezaji wa gofu wa tanzania ikifanya vituvyake katika mashindano ya wazi ya gofu yaliyojulikana kama KCB TANZANIA OPEN yalimalizaika mwishoni mwa wiki katika viwanja vya GYHKHANA jijini DSM

STARS yaanza mazoezi kuivaa Algeria.

Kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania, taifa Stars kilichotangaza na kocha wake mkuu JAN POULSEN jijini Arusha hiyo jana kinaanza mozezi hii leo katika uwanja wa karume tayari kuikabili Algeria ungenini Septemba 4.

Katika kikosi kilichotangazwa jana hakina mabadiliko licha ya kocha huyo kushuhudia michezo miwili mikubwa,mchezo kati ya watani wa jadi Simba na Yanga uliopingwa siku ya jumatano kwania Ngao ya Hisani uliochezwa katika uwanja wa Taifa jijini DSM na ule wa uliopingwa katika uwanja wa Shekh Amr Abeid kati ya AFC na Azam FC.

POULSEN amerudisha kikosi kilekile kilichocheza mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Harambee Stars mchezo ulipingwa AUGOSTI 11 katika uwanja wa Taifa jijini DSM na timu hizo kufungana bao moja kwa moja ikiswa ni pamoja na mlinda mlango majeruhi JUMA KASEJA na kumuacha kiungo wa pembeni KIGI MAKASI.

Pia POULSEN amewateua katika timu yake wachezaji wanosukuma soka ya kulipwa Nizar Khalifan anayekipinga katika timu ya Vancouver White Caps ya Canada,Henry Josoph anayecheza Sweden, Danny Mrwanda anayecheza Veitnam na Idrisa Rajabu wa Sofapaka ya Kenya.

Star itashuka dimbani kuikabili Algeria ugenini Septemba 4 kabla ya kuikabili MORROCCO Octoba 9 jijini DSM.

Stars imepangwa kundi moja na Jamhuri ya Afrika ya Kati, Morocco na Algeria.

==

Ligi kuu ya Tanzania bara yasimama kuipisha Stars.

Ligi kuu Tanzania bara iliyoanza kutimua vumbi katika viwanja sita siku ya jumamosi imesimama hadi septemba 11 kuipisha Taifa Stars inayojianda kuteremka dimbani dhidi ya Algeria ugenini Septemba 3.

Katika michezo iliyochezwa juzi,Katika dimba la Uhuru mabingwa watetezi wa ligi hiyo timu ya Simba ukipenda waiti wekundu wa masimbazi wao waliibuka kidedea kwa ushindi wa mabao mawili kwa bila dhidi ya African Lyon.

Kwingineko mabingwa wa Ngao ya Hisani Yanga ilibuka kidedea baada ya kuichapa Polisi Tanzania kwa bao moja kwa bila.

Katika uwanja wa Shekh Amri Abeid jijini Arusha wanalambalamba AZAM FC iliibuka kidedea kwa ushindi wa mabao mawili kwa bila dhidi ya AFC.

Huko Mwanza wana kishamapanda Toto Africans ya Mwanza wakatumia vyema uwanja wao wa nyumbani wa CCM Kirumba na kuibuka kidedea kwa ushindi wa mabao mawili kwa bila dhidi timu iliyopanda daraja ya Ruvu Shooting.

Huko Kagera Ruvu JKT waliwachapa wenyeji wao KAGERA SUGAR bao moja kwa bila wakati Mtibwa Sugar waliifunga Majimaji ya Songea bao moja kwa bila,

== =

Mashindano ya ngumi ya Afrika ya Mashariki kuanza kesho

Mashindano ya ngumi za riadhaa ya Afrika ya Mashariki maarufu kama mabingwa wa mabingwa yanaanza kutimua vumbi hapo kesho jijini DSM huku mabondia wa Tanzania wakitamba kufanya vyema katika mashindano hayo.

Akizungumza na TBC kwa njia ya simu katibu mkuu wa shirikisho la ngumi za ridhaa nchini (BFT) MAKORE MASHANGA amesema maandalizi ya mashindano hayo yamekamilika huku nchi zitakazo shiriki zikitazamiwa kuwasili jioni ya leo

Mashindano hayo yanashirikisha mabondia kutoka katika nchi za Kenya,Uganda,Rwanda,Burundi ,Botwana na Morius na wenyeji Tanzania.

===

Mashindano ya UMISETA kwa timu za Afrika ya Mashariki yaanza nchini Kenya

Mashindano ya UMISETA kwa timu za Afrika Mashariki yameanza nchini Kenya huku timu za Tanzania zikianza kutupa karata zao za kwanza asubuhi ya leo.

Akiongea na TBC kwa njia ya simu mratibu wa UMISETA kwa timu za Tanzania SALUM SALUM amesema timu ya soka ya wasichana wa Tanzania imeteremka dimbani kuchuana na RWANDA.

SALUM amezitaja timu nyingine za Tanzania zitakazoshuka dimbani kuwa ni timu ya mpira wa kikapu itakayomenyana na Uganda, timu ya mpira wa wavu ya wasichana inaikabili timu ya SUDAN na timu ya mwisho kucheza itakuwa ni ya soka ya wanaume ya Tanzania itakayocheza na Kenya.

Mashindano hayo ya UMISETA ya Afrika Mashariki yanashirikisha timu kutoka nchi za Tanzania, Uganda, Sudan, Rwanda, Burundi na wenyeji Kenya,.

====

Liverpool uso kwa uso na Manchester city

Lgi kuu ya Uingereza itaendelea usiku wa leo kwa matajiri wapya wa ligi hiyo MANCHESTER CITY itakapowakatibisha majogoo wa jiji LIVERPOOL katika uwanja wa CITY OF MANCHESTER.

Kocha wa Liverpol ROY HOGSON anaamini vijana wake watacheza vizuri ugenini na kuibuka na ushndi katika mchezo huo huku kocha wa Man City ROBERTO MANSHINI akijigamba kuibuka kidedea katika uwanja wake wa nyumbani kwa usajili wa nguvu alioufanya msimu huu.

Katika michezo iliyochezwa jana Mashetani wekundu Manchester United walijikuta wakilazimishwa sare ya mabao mawili kwa mawili dhidi ya wenyehi wao FULHAM waliokua chini ya kocha wao mpya MARK HUGHES.

MANCHESTER ndio waliokuwa wa kwanza kujipatia bao lilofungwa na mgongwe PAUL SKOZI katika dakika ya 12 ya mchezo.

FULHAM wakaja juu katika kipindi cha pili na kusawazisha bao hilo kupita kwa DAVIS lakini MAN UNITED wakajipatia bao la pili baada ya beki wa FULHAM BREDE HANGALEND kujifunga wakati akijaribu kuokoa mpira wa kona

LUIS NANI akaikosesha MAN UNITED bao la tatu na pengine lingekua la ushindi lakini penati yake aliyopinga zikiwa zimesalia dakika sita mpira kumalizika ikaenda mikononi mwa kipa wa FULHAM, DAVID STOCKDALE.

Fulham wakafanya shambulizi la mwisho na kupata kona ambayo ilizaa bao lilofungwa na beki wake BREDE HANGALEND.

Katika mchezo mwingine ulichezwa jana ASTON VILLA ilipata kichapo cha mabao sita kwa bila kutoka kwa timu ya NEW CASTLE UNITED

== =

Federer Bibgwa wa Western and Southern Masters

ROGER FEDERER ameshinda taji lake kubwa la 17 la tenisi baada ya kumchapa Mmarekani MARDY FISH kwa ushindi wa seti 2-1 ya 6-7,7-6 na 6-4 katika mchezo wa fainali iliyokua ya kusisimua ya WESTERN AND SOUTHERN FINANCIL GROUP MASTERS iliyofanyika jana nchini MAREKANI.

FEDERER mchezaji nambari mbili kwa ubora wa tenisi duniani ilibidi afanye kazi ya ziada kumdhiibiti mpinzani wake FISH baada ya kufungwa katika seti ya kwanza kwa 7-6.

FEDERER alikuja juu na kucheza kwa ustadi mkubwa na kushinda katika seti ya pili na ya tatu baada ya kupata shindi kwa seti 7-6 na 6-4.

Hili ni taji la NNE la WESTERN AND SOUTHERN FINANCIL GROUP MASTERS kwa FEDERER na likiwa ni taji lake la 17 la mashindano makubwa akiwa nyuma ya Mmarekani ENDRE AGASS mwenye mataji 18.

===

Sunday, August 22, 2010


It’s day 32 on M-Net’s Big Brother All Stars ---and the housemates are hard at work on their latest task building a model version of their ideal Big Brother house. Pictured here: Paloma

Stay tuned to M-Net’s BIG BROTHER ALL STARS with 24/7 coverage on DStv channel 198 plus daily edited shows on M-Net and AfricaMagic. For more information on the series, log on to www.mnetafrica.com/bigbrother. Pictured here: Meryl


STARS ya kuivaa Al-geria yatangazwa

Kocha mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars JAN POULSEN anatangaza kikosi cha timu hiyo jijini Arusha hii leo kitakacho ivaa Algeria ugenini Septemba 4.

Kikosi hicho kitaingia kambini jijini DSM kesho tayari kwa mazoezi ya kujiweka sawa kwa ajili ya mchezo huo.

Katika kikosi kitakacho tangazwa leo haitarajiwi kama kocha huyo atafanya mabadiliko makubwa licha ya kushuhudia michezo miwili,mchezo kati ya watani wa jadi Simba na Yanga uliopingwa siku ya jumatano kwania Ngao ya Hisani uliochezwa katika uwanja wa Taifa jijini DSM na ule wa jana uliopingwa katika uwanja wa Shekhe Amur Abed kati ya AFC na Azam FC.

Wachambuzi wa mambo ya michezo wanasema kocha atarudisha wachezaji wale wale aliowaita kwa ajili ya mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Harambee Stars mchezo ulipingwa AUGOSTI 11 katika uwanja wa Taifa jijini DSM na timu hizo kufungana bao moja kwa moja.

Pia POULSEN anatarajiwa kuwateua katika timu yake wachezaji wanosukuama soka ya kulipwa ambao ni Nizar Khalifan anayekipinga katika timu ya Vacouvor White Camps ya Canada,Henry Josophy anayecheza Sweeden na mshambuliaji wa timu hiyo Danny Mrwanda anayecheza Veitnam na Idrisa Rajabu wa Sofapaka ya Kenya.

Star ikishashuka dimbani dhidi ya Algeria ugenini Septemba 4 itakabiliwa na mtihani mwingine mgumu nyumbani dhidi ya timu ngumu ya MORROCCO Octoba 9.

Timu ya taifa ya Tanzania,Taifa Stars imepangwa katika kundi lenye timu za Jamhuri ya Afrika ya Kati,Morocco na Algeria.