Tuesday, March 22, 2011

MICHEZO LEO

Kufutia kutokea kwa ajali iliyohusisha wasanii wa muziki wa taarabu wa kundi la FIVE STARS Mwanamichezo wetu JANE JOHN ametembelea ofisi za kundi hilo pamoja na nyumbani kwa mmoja wa wasanii ambaye amefariki dunia katika ajali hiyo ISSA HASSAN aliyekuwa akifahamika kwa jina maarufu la ISSA KIJOTI na baadae kupata fursa ya kuongea na baadhi ya wasanii na wapenzi wa muziki wa Taarabu.

Safari yangu ilianzia Katika ofisi ya kundi la FIVE STARS, katika ukumbi wa IKWETA GRIR ambapo nakutana na ndugu jamaa na marafiki waliofika katika ofisi hizo kwa lengo la kujua nini kinachoendelea baada ya kutokea kwa ajali hiyo.

Katika eneo hili nakuta huzuni ilitawala kwa wasanii waliokuwa kundi hilo ambao hawakusafirI na kundi hilo kutoka na kuumwa na wengine kuhama katika bendi.

Mwimbaji MARIAM HAMIS ambaye hivi karibuni alihama katika kundi hilo pamoja na mwimbaji HADIJA KOPA na mwimbaji JOHA KASSIM ambaye kutoka na kuumwa hakusafiri na kundi holi wanaelezea jinsi walivyopeka msimba huo.

Kwa upande wake mkurugenzi wa kundi la FIVE STARS FEROUZ JUMA alikuwa na haya ya kusema.

Baada ya hapo nikafika nyumbani kwao msanii ISSA HASSAN TEMEKE hali ya huzini ikitawala na hapa mama yake mzazi AMIN MAHAMOD anasema yote ni mipango ya mungu.

Nikipande kidogo alichoimba msanii ISS HASSAN


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Mheshimiwa Emmanuel Nchimbi kutokana na vifo vya wasanii 13 wa Kundi la Muziki wa Taarab la Five Star Modern Taarab.

Rais Kikwete amesema anamwomba Mwenyezi Mungu azilaze mahali pema peponi roho za Marehemu wote huku akiwaomba waliopoteza wapendwa wao katika ajali hiyo mbaya kuwa na moyo wa uvumilivu, ujasiri na subira katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo.
Wasanii hao waliokuwa kwenye gari la kukodi wakitokea Kyela, Mbeya, walipata ajali eneo la Doma, karibu na Mbuga ya Wanyama ya Mikumi, Mkoani Mororogoro usiku wa kuamkia leo tarehe 22 Machi, 2011 wakati gari hilo lilipogongana na gari lingine. Wasanii hao walikuwa wakirejea Dar es Salaam kutoka Mbeya ambako walikuwa wamefanya maonyesho.
==
SERIKALI KUTAFUTA MWEDESHAJI UWANJA WA TAIFA

Serikali imesema itafuta uwezekano wa kumtafuta wakala wa ndani ya nchi kuendesha uwanja wa taifa baada ya kushindwa kumpata mwendeshaji wa uwanja huo katika mchakato uliofanyika mwaka jana.

Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, EMMANUEL NCHIMBI ameyasema hayo katika Mkutano wake na Jukwaa la wahariri jijini DSM ambapo amesema nia ya serikali ni kuufanya uwanja huo uwe wa kisasa zaidi.

Pia NCHIMBI amesema serikali inatafuta uwezekano wa kupunguza makato ya viingilio ili kuviwezesha vilabu shindani kunufaika zaidi na viingilio hivyo.

Hata hivyo, akaonyeshwa kukerwa na tabia za baadhi ya watu wanaoharibu kwa makusudi baadhi ya samani ndani ya uwanja huo na kusema hiyo siyo tabia ya kizalendo.

====

Makamu M/Kiti wa kamati ya kudumu ya bunge ya maendeleo ya Jamii JUMA NKAMIA amelitaka shirikisho la soka nchini TFF kuhakikisha pesa zinazotolewa na FIFA zinatumika kama ilivyokusudiwa kuleta maendeleo ya soka hapa nchini.

NKAMIA amesema kwamba kwa sasa utaratibu unaotumika kuratibu matumizi ya fedha hizo haouko wazi jambo ambalo amedai linatoa mwanya wa matumizi ya pesa hizo kwa mkoa wa DSM pekee huku mikoa mingine ikiachwa bila kunufaika na pesa hizo. (PAUSE) JUMA NKAMIA - Makamu M/Kiti wa kamati ya kudumu ya bunge ya maendeleo ya Jamii.

Katika hatua nyingine NKAMIA ameitaka TFF kufikiria uamuzi wake wa kupunguza idadi ya wachezaji wa kigeni katika ligi kuu kutoka wachezaji watano hadi watatu, hatua ambayo amesema inaweza kuathiri maendeleo ya soka hapa nchini kutokana na mchango wa wachezaji hao katika ukuaji wa soka la Tanzania.

===
MANYARA STARS kuondoka Alhamisi tayari kuikabili CAMEROON
Timu ya taifa ya Tanzania chini ya umri wa miaka 23 MANYARA STARS kuondoka keshokutwa siku ya Alhmisi tayari kuikabili CAMEROON katika mchezo wa awali kuwani kucheza fainali ya OLYMPIKI itayofayika LONDON mwakani.
Akizunguza jijini DSM hii leo Afisa habari wa shirikisho la soka nchini TFF BONIFACE WAMBURA amesema msafara wa timu hiyo utakuwa na wachezeja 18 na viongozi watano.
Wakati huo huo WAMBURA amesema wachezaji wa timu ya taifa ya AFRIKA ya KATI wamewasili kwa mafungu usiku wa kuamkia leo tayari kwa mchezo wao dhidi ya TAIFA STARS mchezo uliopangwa kuchezwa jumamosi wiki hii na kuongeza kwamba idadi ya wachezaji wengine wanategemewa kuwasili mchana huu.
Jioni ya leo timu ya AFRIKA ya KATI inategemewa kufanya mazoezi yake katika uwanja wa KARUME wakati TAIFA STARS yenyewe itakuwa katika uwanja wa TAIFA jijini DSM.
===
TP MAZEMBE YACHONGEWA JENEZA DSM
Mashabiki wa soka wa SIMBA katika eneo la bandari jijini DSM wamechonga jeneza na kuliandika jina la TP MAZEMBE wakiashiria kuzikwa kwa timu hiyo itapocheza na mabingwa wa soka nchini SIMBA katika mchezo wa marundiano wa ligi ya mabingwa Afrika utakaoipigwa wiki mbili zijazo kwenye uwanja wa taifa jijini DSM.
Wakizungumza na TBC kwa niamba ya mashabiki wezao MOSSES AMBROSS na SAID MBEGA wamesema wametegeneza jeneza hili wakiashiria kwamba SIMBA itaibuka kidedea dhidi ya TP MAZEMBE katika mchezo wa marundiano.
Katika mchezo wa kwanza wa ligi ya mabingwa Afrika uliopigwa jumapili iliyopita katika uwanja wa KENYA mjini lumbumbashi SIMBA ililala kwa kufungwa mabao matatu kwa moja hiyo inatakiwa kushinda kwa mabao mawili kwa bila ili ishonge mbele.
==
RAGA YAANZA KUFUNDISHWA SHULE ZA MSINGA DSM.
Vijana 12 wa shule ya msingi Mapambanano jijini DSM wameanza mafunzo ya mchezo wa RAGA yanayotolewa na mkufunzi kutoka UINGEREZA RICHARD BENETT.
Akizungumza na TBC BENETT kutoka katika taasisi ya kimichezo ya BHUBESI PRIDE amesema wameamua kuazisha mchezo huo katika shule za msingi za Tanzania kwa lego la kukuza mchezo huo hapa nchini.

Naye mkuu wa shule ya msingi Mapambano IDDA UISSO amesema mafunzo hayo yamekuja wakati mwafaka na yatasaidia kukuza vipaji kwa wachezaji chipukizi wa RAGA kwa faida ya timu ya taifa kwa siku za usoni.
Tanzania ni miongoni mwa nchi nyingine kumi za Afrika ambazo zitafaidika a mafunzo ya mchezo wa RAGA kutikakatika taasisi hiyo ya BHUBESI PRIDE ya UINGEREZA.
==
WASANII KUTUMBUIZA KATIKA Tuzo za Kili Music
Wasanii wa kizazi kipya na wale wa taarabu kutumbuiza wakati wa onyesho la Tuzo za Muziki za Kili ambazo zitafanyika katika ukumbi wa wa Diamond Jubilee Jumamosi ya MACHI 26.
Akizungumza wakati wa kutambulisha tuzo hizo jijini DSM hii leo Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Bia Tanzania TBL, David Minja amesema utoaji wa Tuzo za mwaka huu utapambwa na burudani tofauti kutoka kwa wasanii mbalimbali ili lionekane la kisasa zaidi mwaka huu tofauti na miaka mingine.
Minja akawataja wasanii watakaotumbuiza katika utoaji wa Tuzo hizo ni Ali Kiba, THT, Banana Zoro, Linah, Diamond, Joe Makini, C Pwaa, 20%, Mzee Yusuf pamoja na Mapacha Watatu na Stara Thomas.
Baadhi ya tuzo zinazoshindaniwa kwa mwaka 2010/ 2011 ni Msanii wa kike bora wa Muziki, Msanii wa Kiume Bora wa Muziki, Mwibaji bora wa Kike, Mwimbaji Bora wa Kiume, Wimbo Bora wa Taarab, Wimbo bora wa Mwaka.
===
BLACK STARS imewasili jana nchini Kenya kuweka kambi
Nayo timu ya GHANA, BLACK STARS imewasili nchini KENYA jana kuweka kambi ya siku NNE kabla ya kuelekea CONGO BRAZZAVILLE ambapo timu hiyo ya GHANA itakuwa mgeni katika mechi hiyo.
Hii ni mara ya NNE kwa BLACK STARS kuweka kambi huko NAIVASHA nchini KENYA, ambapo timu hiyo kabla ya kwenda nchini AFRIKA KUSINI kushiriki mashindano ya kombe la dunia iliweka kambi nchini KENYA.
Hata wakati wa mashindano ya wachezaji wanaocheza mashindano ya ndani yaani CHAN, timu ya GHANA iliweka kambi yake nchini KENYA na baadae kwenda kushiriki mashindano ya CHAN yaliyofanyika nchini SUDAN.
==
MOHAMED BIN HAMMAM aendelea kumpinga BLATTER
MGOMBEA wa kiti cha urais katika shirikisho la soka duniani FIFA, MOHAMED BIN HAMMAM ambaye anapinga sera za rais wa sasa wa shirikisho hilo , SEPPY BLATTER , amesema akichaguliwa ataweka mipango ya uwazi wakati wa kuchagua nchi itakayoandaa mashindano ya kombe la dunia.
Bin Hammam , amesema FIFA haitaki rushwa ila shirikisho hilo linahitaji kuwa na uwazi katika kiwango kikubwa katika kuamua mambo yake.
Rais wa sasa wa FIFA , SEPPY BLATTER alikuwa katika wakati mgumu baada ya wajumbe wa kamati ya utendaji wa shirikisho hilo mwaka jana kuchagua URUSI na QATAR kuandaa mashindano ya dunia ya mwaka 2018 na 2022.
Wakati ambapo kazi hiyo ikifanyika kulikuwa na tuhuma za rushwa kwa wajumbe wawili wa shirikisho hilo kwamba walitumiwa kutaka kuuza kura zao ili nchi fulani ifanikiwe kuandaa mashindano hayo ya dunia.
==
NOVAK afurahia kupata nafasi ya pili ya ubora duniani.
MCHEZAJI wa TENNIS, NOVAK DJOKOVIC ambaye amempiku ROGER FEDERER na kuchukua nafasi ya pili kwa ubora duniani amesema hajawahi kuwa katika kiwango cha juu kama hivi sasa tangu aanze kucheza mchezo huo.
DJOKOVIC, alimfunga RAFAEL NADAL katika fainali za mashindano ya INDIAN WELLS ATP na kunyakuwa ubingwa wa mashindano hayo.
Djokovic mwenye miaka 23, alimpiku ROGER FEDERER baada ya kupata ushindi wa 6-3 3-6 6-2 dhidi ya RAFAEL NADAL.
Nafasi ya NNE ya ubora ulimwenguni inashikiliwa na ROBIN SODERLING kutoka SWEDEN na ya TANO inashikiliwa na ANDY MURRY kutoka UINGEREZA.
==

Tuesday, March 15, 2011


Jengo la simba FC katika lililopo katika mitaa ya msimbazi na karikakoo jijini DSM ambalo limefanyiwa ukarabati.


Mchezaji wa SIMBA VETERANS Madaraka Suleima "mzee wa kiminyio" akiongea na waandishi Habari juu ya pambano lao dhidi ya YANGA VETERANS litakalopigwa siku ya jumamosi katika uwanja wa taifa jijini DSM

Kocha wa timu ya taifa ya Tanzania TAIFA STARS,JAN POULSEN akitangaza kikosi cha timu hiyo jijini DSM hii leo

POULSEN ATANGAZA STARS KUIVAA JAMHURI YA KATI

Dihile Kazimoto Warejeshwa Stars kuikabili Jamhuri Ya Kati
Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Tanza nia TAIFA STARS JAN POULSEN amewarejesha kikosini mlinda mlango SHABANI DIHILE na kiungo mshambuliaji MWINYI KAZIMOTO wote wa JKT RUVU katika kikosi cha STARS kinachojiandaa na mchezo wa kuwania tiketi ya kucheza fainali za kombe la mataifa ya Africa CAN dhidi ya JAMHURUI YA KATI mchezo utakaopigwa MACHI 26 kwenye dimba la taaifa jijini DSM.

Akitangaza kikosi hicho chenye wachezaji 23 POULSEN amesema STARS inahitaji kupata pointi nne katika michezo miwili ijayo kama inataka kufufua matumaini ya kufunzu kucheza fainali za Afrika mwakani hivyo mchezo ujao dhidi ya JAMHURI YA KATI lazima STARS ishinde.

POULSEN amesema anajivunia nyota wake sita wanaosukuma soka la kulipwa ulaya ambao ni Danny Mrwanda na Abdi Kasim wanaocheza DT Long An ya Vietnam,Nizar Khalifan wa Vancouver White Caps ya Canada,ATHUMAN MACHUPA wa Vasolund Fc ya Sweden,Henry Joseph wa Kongsvinger Il ya Norway na Idrissa Rajab wa Sofapaka Kenya wakichanganyika na wale vyota wanaocheza lingi ya nyumbani anauhakika wa Stars kuibuka na ushindi.

STARS inashika nafasi ya tatu katika kundi la D ikiwa na Alama moja baada ya kutoka sare ya bao moja kwa moja na ALGERIA ugenini kabla ya kufungwa na MOROCCO bao moja kwa bila nyumbani,JAMHURI YA KATI ipo kileleni mwa kundi hilo ikiwa na ALAMA NNE.

===
Viingilio Simba na Yanga Kuchangia Gongo la Bonto hadharani.
Viingilio vya kuziona timu za veteran za SIMBA na YANGA zitakazocheza kuchangi wathirika wa mabumu ya Gongo La Mboto vyatagazwa cha juu ni 10,000/- na cha chini 1000/-,mchezo huo utapigwa kwenye dimba la taifa jijini DSM MACHI 19 siku ya jumamosi.

Wakizungumza wakati wa kutangaza viingilio hivyo Afisa habari wa SIMBA CLIFORD NDIMBO na wa YANGA LIUIS SENDEU wamesema mechi hiyo imepewa baraka zote na viongozi wa timu zote mbili na tayari maadalizi ya matanange huo yamekamilika.

Kwa upande wao wachezaji wa timu zote mbili wakiongea kwa niamba ya wezao MADARAKA SELEMAN wa Simba na BAKARI malima wa YANGA wamesema wamejiandaa vyema kutoa burundani ya kutosha kwa mashabiki watakohudhuria kushuhudia mchezo huo.

Viingilio katika mchezo huo vitakuwa kama ifuatavyo,VIP A 10,000/- VIP B,5000/- VIP C 3000/- viti vya bluu na kijani mzunguko ni shilingi 2000 na 1000/-

===

Wasaanii kutumbuiza tamasha la UZALENDO

katika burundani wasanii mbalimbali kutumbuiza katika tamasha lilopewa jina laTAMASHA LA UZALENDO,TANZANIA KWANZA,SOTE NI NDUGU litakalofanyika MACHI 26 katika viwanja vya biafra jijini DSM.

wakizungumza na tbc jijini DSMn hii leo waadaji wa tamasha hilo ERICK SHIGONGO na mwanamziki wa rage INNOCENT GALINOMA wamesema tamasha hilo limeandaliwa ili kuwakumbusha watanzania kupitia mziki juu ya uzalendo wa kuipenda nchi yao na kuthamini amani.

Wasanii watakao konga nyoyo za mashabiki ni Profesa J,Ay,H Baba,H.Mbizo wakati kwa uapande wa bendi zitakuwepo MSONDO NGOMA,DDC MLIMAN PARK,TOT BAND na African Stars.
==

MAN UNITED VS MARSEILLE, BAYERN VS MILAN

USIKU huu ligi ya mabingwa barani ulaya UEFA inaendelea kwa michezo miwili ambapo, MANCHESTER UNITED ikiwa nyumbani leo inaikaribisha timu ya MARSEILLE ya UFARANSA katika mchezo mgumu kwa timu zote kwani katika mchezo wa awali uliochezwa nchini UFARANSA timu hizo zilitoka suluhu.

Kocha wa MARSEILLE, DIDIER DESCHAMPS amesema kikosi chake leo kitaingia uwanjani katika dimba la OLD TRAFFORD ikiwa na lengo la kutafuta ushindi.

DESCHAMPS amesema anakiamini kikosi chake kitapata tiketi ya kwenda hatua nyingine ya mashindano ya UEFA ijapokuwa MAN UNITED haijawahi kufungwa na timu ya UFARANSA katika uwanja wa Old Trafford basi leo timu yake itavunja mwiko huo.

Nayo BAYERN MUNICH ya UJERUMAN itakuwa nyumbani kuikabili INTER MILAN ya ITALIA.

Kesho michezo hiyo itaendelea ambapo CHELSEA itakuwa katika uwanja wake wa nyumbani wa STANFORD BRIDGE kucheza na FC COPENHAGEN na REAL MADRID itacheza na LYON.

==
JOHN TERRY kurejeshewa Unahodha

KOCHA wa timu ya taifa ya UINGEREZA anafikiria kumrejeshea unahodha JOHN TERRY baada ya sasa RIO FERDINAND kuwa majeruhi.

FERDINAND atakosa mchezo wa kutafuta tiketi ya kucheza mashindano ya EURO 2012 dhidi ya WALES mchezo utakaochezwa machi 26 ambapo pia nahodha msaidi wa FERDINAND, STEVEN GERRALD naye hatokuwepo katika mchezo kufuatia kusumbuliwa na HERNIA.

katika hatua nyingine klabu ya ARSENAL ina mpango wa kumsaji golikipa wake wa zamani mwenye miaka 41 sasa JENS LEHMANN.

Hali hii inatokana na timu ya ARSENAL kukabiliwa na magolikipa wake ambao ni majeruhi kama WOJCIECH SZCZESNY, LUKASZ FABIANSKI na VITO MANNONE na hivyo kusalia na kipa mmoja tu MANUEL ALMUNIA.
Wakati akiwa ARSENAL kati ya mwaka 2003 na 2008, LEHMANN aliichezea timu yake michezo MIA TISINI na TISA.
Kama masuala ya kusainishwa kwa golikipa huyo hayatakuwa na utata , LEHMANN anaweza akawemo katika kikosi chqa ARSENAL kitakachocheza mchezo wa jumamosi dhidi ya WEST BROM.
==
NADAL aanza vizuri mashindano ya BNP PARIBAS

RAFAEL NADAL amefanikiwa kuanza vizuri mashindano ya wazi ya TENNIS ya BNP PARIBAS kwa kumfunga RYAN SWEETING kwa seti 6-3, 6-1.
NADAL ameweza kufanya vizuri katika mchezo huo baada ya kuanza vibaya kwenye mashindano hayo yanayofanyika nchini INDIA.
Matokeo mengine upande wa wanawake CAROLINE WOZNIACKI wa DENMARK amefanikiwa kumchapa 6-1, 6-3 mpinzani wake MARIA JOSE MARTINEZ SANCHEZ wa Hispania.
Naye DINARA SAFINA amemfunga SAMANTHA STOSUR kwa seti 7-6, 6-4, ushindi wa SAFINA umekuja baada ya mchezaji huyo kuwa nje ya ya mashindano kutokana na kuwa na maumivu ya mgongo.
==
Tiketi za Olympiki 2012 zaanza kuuzwa
TIKETI zinakazotumika kuingia katika mashindano ya OLYMPIKI ya LONDON mwakani zimeanza kuuzwa siku MIA TANO kabla ya mashindano hayo kuanza.
Zaidi ya tiketi milioni 6.6 zitanunuliwa kwa kipindi cha wiki SITA.
Bei za tiketi hizo ni kuanzia paundi ISHIRINI hadi paundi ELFU MBILI.
==