Tuesday, August 2, 2011

Baada ya TWIGA STARS kufanya vizuri sasa COSAFA yaialika NGORONGORO HEROES katika michuano ya VIJANA.






Baada ya TWIGA STARS kufanya vizuri sasa COSAFA yaialika NGORONGORO HEROES katika michuano ya VIJANA.
Baada ya kufanya vizuri kwa timu ya taifa ya wanawake ya TANZANIA, TWIGA STARS katika michuano ya COSAFA na kushika nafasi ya tatu, Timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 20, NGORONGORO HEROES nayo imealikwa katika michuano ya vijana ya ukanda huo wa kusini mwa AFRIKA yatakayoanza DECEMBER MOJA hadi KUMI NA MBILI mwaka huu.
Afisa Habari wa TFF , BONIFACE WAMBURA amesema timu hiyo ambayo inaendelea na mazoezi chini ya kocha KIM POULSEN akisaidiwa na ADOLF RISHARD huku gharama zote zikitolewa na COSAFA.
NGORONGORO HEROES hivi karibuni iliweza kufanya vizuri dhidi ya USHELISHELI katika mechi mbili za kirafiki jijini ARUSHA ambapo iliweza kushinda mechi zote.
=== ==
TFF yatoa ratiba ya VPL
Wakati huo huo ,Shirikisho la soka nchini TFF , limetoa ratiba ya ligi kuu soka ya Vodacom raundi ya kwanza ambapo jumla ya timu zote KUMI na NNE zitashuka dimbani ambapo ratiba inaonyesha timu hasimu za SIMBA na YANGA zitakutaka OCTOBER 29 katika mzunguko wa kwanza na APRIL MOSI katika mzunguko wa pili.
Katika za raundi ya kwanza ya Ligi hiyo inayoanza AUGUST 20 na 21, JKT OLJORO watakuwa wenyeji wa SIMBA mjini ARUSHA , ilhali YANGA watakuwa wenyeji wa JKT RUVU katika mechi ambayo itachezwa katika uwanja wa TAIFA jijini DAR ES SALAAM AUGUST,21.
Katika siku ya ufunguzi AUGUST 20, TOTO AFRICANS ya MWANZA itafungua dimba katika UWANJA WA CCM KIRUMBA dhidi ya VILLA SQUAD,COASTAL UNION ikichuana na MTIBWA SUGAR,KAGERA SUGAR itaialika RUVU SHOOTING,nao maafande wa POLISI DODOMA wakiikaribisha AFRICAN LYON katika uwanja wa JAMHURI mjini DODOMA.
Mechi nyingine ya ufunguzi itakuwa ni baina ya AZAM FC ambayo itaikaribisha JKT RUVU katika UWANJA WA CHAMAZI.
= =
Baada ya TWIGA STARS kufanya vizuri sasa COSAFA yaialika NGORONGORO HEROES katika michuano ya VIJANA.
Baada ya kufanya vizuri kwa timu ya taifa ya wanawake ya TANZANIA, TWIGA STARS katika michuano ya COSAFA na kushika nafasi ya tatu, Timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 20, NGORONGORO HEROES nayo imealikwa katika michuano ya vijana ya ukanda huo wa kusini mwa AFRIKA yatakayoanza DECEMBER MOJA hadi KUMI NA MBILI mwaka huu.
Afisa Habari wa TFF , BONIFACE WAMBURA amesema timu hiyo ambayo inaendelea na mazoezi chini ya kocha KIM POULSEN akisaidiwa na ADOLF RISHARD huku gharama zote zikitolewa na COSAFA.
NGORONGORO HEROES hivi karibuni iliweza kufanya vizuri dhidi ya USHELISHELI katika mechi mbili za kirafiki jijini ARUSHA ambapo iliweza kushinda mechi zote.
=== ==
TFF yatoa ratiba ya VPL
Wakati huo huo ,Shirikisho la soka nchini TFF , limetoa ratiba ya ligi kuu soka ya Vodacom raundi ya kwanza ambapo jumla ya timu zote KUMI na NNE zitashuka dimbani ambapo ratiba inaonyesha timu hasimu za SIMBA na YANGA zitakutaka OCTOBER 29 katika mzunguko wa kwanza na APRIL MOSI katika mzunguko wa pili.
Katika za raundi ya kwanza ya Ligi hiyo inayoanza AUGUST 20 na 21, JKT OLJORO watakuwa wenyeji wa SIMBA mjini ARUSHA , ilhali YANGA watakuwa wenyeji wa JKT RUVU katika mechi ambayo itachezwa katika uwanja wa TAIFA jijini DAR ES SALAAM AUGUST,21.
Katika siku ya ufunguzi AUGUST 20, TOTO AFRICANS ya MWANZA itafungua dimba katika UWANJA WA CCM KIRUMBA dhidi ya VILLA SQUAD,COASTAL UNION ikichuana na MTIBWA SUGAR,KAGERA SUGAR itaialika RUVU SHOOTING,nao maafande wa POLISI DODOMA wakiikaribisha AFRICAN LYON katika uwanja wa JAMHURI mjini DODOMA.
Mechi nyingine ya ufunguzi itakuwa ni baina ya AZAM FC ambayo itaikaribisha JKT RUVU katika UWANJA WA CHAMAZI.
= =

Vilabu vinane vya gofu kuchuana Arusha


Vilabu vinane vya mchezo wa gofu vinatarajiwa kushiriki katika mashindano ya kutafuta klabu bingwa ya taifa ambayo yanatarajiwa kufanyika jijini ARUSHA siku ya jumamosi na jumapili ijayo.
Akizungumza na TBC Afisa Tawala wa chama cha gofu Tanzania (TGU) SOFIA NYANJERE amesema lengo la mashindano hayo ni kuchangua timu ya taifa ya gofu ambayo itashiriki mashindano ya CHALENGE kwa nchi za Afrika Mashariki na kati yatakayo fanyika mwezi NOVEMBA jijini ARUSHA.

Vilabu vitakavyo shiriki katika michuano hiyo ni LUGALO, MFINDI, ARUSHA, MOROGORO, DSM GYMKHANA, TPC, MOSHI na KILOMBERO.
== ==

Timu ya taifa ya Kuogelea yarudi mikono mitupu


Ukosefu wa uzoefu na vifaa vya kisasa vya michezo pamoja na maandalizi duni , imetajwa kama sababu ya kushindwa kufanya vizuri kwa Timu ya taifa ya mchezo wa kuogelea ambayo imewasili leo ikitokea CHINA ambapo ilikuwa ikishiriki katika mashindano ya KUMI NA NNE ya mchezo huo duniani .
Mmoja wa wachezaji wa timu hiyo AMAR GHADIARI pamoja na kocha wa timu hiyo RAMADHAN KHAMIS wamesema ili TANZANIA iweze kufanya vizuri katika michuano ya kimataifa ya kuogelea katika siku za usoni , serikali inabidi itilie mkazo katika michezo mingine ukiwamo mchezo wa kuogelea , huku akieleza changamoto alizozipata katika michunao hiyo.
Timu ya taifa ya TANZANIA haikuwerza kupata medali hata MOJA katika michuano hiyo ambapo kwa upande wa nchini za AFRIKA , AFRIKA YA KUSINI , TUNISIA na MISRI ndio nchi pekee zilizonyakua medali huku wenyeji CHINA na MAREKANI zikifanya vizuri.
==