Thursday, February 24, 2011

MICHEZO LEO


Kuelekea pambano la ngumi la uzito wa juu TAMIMU atamba kuchapa ASHIRAFU.

Bondia AWADHI TAMIM ambaye amerejea kutoka nchini SWEDEN amesema anaendelea kujifua vilivyo kwa ajili ya pambano la uzito wa juu kuwania ubingwa wa AFRIKA MASHAIRIKI dhidi ya ASHRAF SULEIMAN litakalofanyika MACHI 11.

Akizungumza na TBC ONE, TAMIM amesema kuwa ana uhakika kuwa atamtwanga mpinzani wake katika hatua za mwanzo .

TAMIM amesema kuwa kwa sasa anajifua chini ya kocha wake SHOMARI KIMBAU ambapo amesema kabla ya kurejea hapa nchini alicheza mechi za kujipika nguvu .

Kwa upande wake mratibu wa pambano hilo ALLY SULUEIMAN,amesema mshindi wa pambano hilo atakwenda nchini MAREKANI kupigana na bondia mwingine ambaye anatafutwa .
= =

Ligi daraja la pili netiboli kumalizika leo.

Mashindano ya netiboli ligi daraja la pili yamefungwa leo hii katika uwanja wa JAMHURI mkoani MOROGORO na tayari timu tatu zimeshapanda daraja.


Baadhi ya viongozi wa timu zinazoshiriki mashindano hayo kocha wa timu ya LINDI ALICE CHIWAJI pamoja na kocha wa BLACK SISTER ya PWANI FARAJA JUMA wamesema mashindano ni mazuri lakini kunamapungufu ambayo yameweza kujitokeza katika mashindano hayo

Timu ambazo zimeshuka ni MINGA MOROGORO, TUPENDANE LINDI na BLACK SISTER ya PWANI.

Mashindano hayo ya ligi daraja la pili yanashirikisha timu kumi na moja kutoka mikoa tofauti ya TANZANIA BARA.

====.
KIFA yashindwa kuandaa mashindano ya soka la wanawake.

Katibu mkuu wa soka wilaya ya KINONDONI FRANK MCHAKI amesema Wilaya ya KINONDONI haitaweza kuandaa mashindano ya soka la wanawake kama ilivyokuwa zamani kutoka na ukukata wa fedha katika chama hicho.

Akizumgumza Jijini DSM FRANK MCHAKI amesema KIFA ilikuwa akiandaa mashindano ya soka la wanawake kwa lengo la kukuza soka hilo na kupata wachezaji watakaounda timu ya TAIFA lakini kwa kipindi hiki haitawezekana.

MCHAKI amesema sasa mashindano ya soka la wanawake yatakuwa yansimamiwa na chama cha soka la wanawake mkoa wa DSM .

Mpaka sasa mashindano ya soka la wanawake ya kutafuta timu ya bingwa ya mkoa .

=====
BAYEN MUNCHEN yaichapa INTER MILAN ulaya.

Ligi ya mabingwa barani ulaya imeendelea jana ambapo kule nchini ITALIA katika uwanja wa SAAN SIRO kulikua na mchezo kati ya wenyeji INTER MILAN dhidi ya BAYEN MUNCHEN ya nchini UJERUMANI.

Katika mchezo huo BAYEN imeibuka kidedea kwa kushinda bao moja kwa bila ikiwa ugenini.

INTER ndio walioanza kulerta kashikashi langoni mwa BAYEN MUNICH kabla ya BAYEN kujibu mapigo haraka kwa krosi iliyopigwa na ARJEN ROBBEN kupigwa kichwa na FRANK RIBERY kilichokwenda kugonga mwamba wa juu.

Kwenye dakika ya 62 ARJEN ROBBEN aliwatoka mabeki wa INTER MILAN na kupiga mpira uliokwenda kugonga mwamba wa pembeni na kutoka nje.

INTER nayo ikafanya mashambulizi ambapo SAMUEL ETOO alipiga shuti lililookolewa na kipa wwa BAYEN lakini ESTEBAN CAMBIASO alishindwa kumalizia mpira huo uliokua umeokolewa na kipa wa BAYEN.

Hata hivyo katika dakika ya 90 MARIO GOMES aliwanyanyua mashabiki wa BAYEN MUNCHEN kwa kufunga goli pekee la mchezo huo akimalizia shuti lililopigwa na ARJEN ROBBEN ambalo liliokolewa na kipa wa INTER CESAR na kushindwa kuudaka vizuri.

= = = = =

MARSEILLE sare na MANCHESTER UNITED.

Nchini UFARANSA MARSEILLE chini ya DIDIER DESCHAMP imeshindwa kuutumia uwanja wake vyema baaada ya kutoka suluhu ya sifuri bin sifuri dhidi ya MANCHESTER UNITED.

Timu zote mbili zilipiga mashuti ndani ya goli MAWILI TU katika dakika zote tisini.
Kocha wa MANCHESTER UNITED SIR ALEX FERGUSON amesema matokeo hayo ni mabaya lakini hakusita kuipigia upatu timu yake kuibuka na ushindi katika mchezo wa marudiano utakaochezwa kwenye uwanja wa OLD TRAFFORD majuma matatu yajayo.

FERGUSON amekubali pia kuwa haukuwa mchezo mzuri wa kuangalia kwa kuwa ulikua hauna masham masham mengi kutokana na kila timu kushindwa kutengeneza nafasi za wazi za kufunga.

FERIGE amesema matokeo kama hayo ni mabaya kama utafungwa goli hata moja nyumbani kwako lakini pia yatakua mazuri kama utashinda kwa kuwa utasonga mbele.

Aidha upande mwingine wa shilingi DIDIER DESCHAMP amewapongeza wachezaji wake kwa juhudi walizozifanya na kusema kuwa wageni hao ambao ni UNITED watakua wamefurahia matokeo hayo.

DESCHAMP amekubali kiwango kilichooneshwa na UNITED na kuongeza kuwa matokeo hayo ya suluhu so mabaya kwao lakini ni mazuri kwa upande wa MANCHESTER UNITED.

= = = =
PORTO yasonga mbele EUROPA LEAGUE
Katika UEFA ndogo ama EUROPA LEAGUE FC PORTO ikiwa nyumbani imefungwa bao MOJA kwa BILA lakini imefuzu kusonga mbele katika ligi hiyo kwa faida ya goli la ugenini.

Shuti lililopigwa na mchezaji wa PORTO lilikwwenda kugonga mwamba wwa pembeni kabla ya ALVARO kupiga shuti lililokwenda nje.

PORTO waliendelea kuliandama lango la SEVILLA safari hii tena mpira uligonga mwamba baada ya kupigwa kichwa na FALCAO.

Kwenye dakika ya 70 LUIS FABIANO mchezaji wa zamani wa PORTO aliipatia SEVILLA goli la pekee la mchezo huo.

Dakika chache baadaye PORTO walipunguzwa mchezaji mmoja baada ya ALVARO kucheza ndivyo sivyo.

SEVILLA nao wwakapunguzwa mchezaji mmoja baada ya ALEXIS kupewa kadi ya njano ya pili.

Sasa PORTO imefuzu kucheza hatua ya 16 bora ya ligi hiyo na itakutana na CSKA MOSCOW ya URUSI.

= = ==.
ARSENAL yaichapa STOKE EPL.

Wakati ligi ya mabingwa barani ulaya ikichezwa jana usiku, ligi kuu soka ya ENGLAND pia ilichezwa jana usiku kwa mchezo mmoja tu kati ya ARSENAL wakiwa EMIRATES dhidi ya STOKE CITY.

ARSENAL imeisogelea MANCHESTER UNITED sasa ikiwa nyuma kwa pointi moja baada ya kushinda goli MOJA kwa bila dhidi ya STOKE.

Goli la ARSENAL limepatikana katika dakika ya 7 mfungaji akiwa SEBASTIAN SQUILACHI aliyefunga kwa kichwa kufuatia kona iliyopigwa na JACK WILSHERE na NICKLAS BENDTNER kumtengenezea SQUILACHI.

Kwenye dakika ya 13 ARSENE WENGER alilazimika kumtoa nahodha CES FABREGAS ambaye alikua ameumia msuli wa mguu na kumwingiza ANDREI ASHARVIN.

STOKE ilijaribu kusaka bao la kusawazisha lakini ngome ya ARSENAL ilikua imara kuhakikisha inaokoa hatari zote zilizokua zinapelekwa langoni mwake.

ARSENAL ilipata pigo tena katika dakika ya 68 pale winga wake THEO WALCOT alipoumia kifundo cha mguu na kutolewa nje kwa machela.

Juhudi za STOKE kutaka kusawazisha bao hilo hazikuzaa matunda kwani mpaka dakika tisini zinamalizika bao hilo ndilo lilikua pekee katika mchezo huo.

Hata hivyo meneja wa ARSENAL ARSENE WENGER amesema kuwa winga wake THEO WALCOT ataukosa mchezo wa fainali ya kombe la CARLING siku ya Jumapili dhidi ya BIRMINGHAM kutokana na majeraha hao aliyoyapata.

Kuhusu nahodha wake CESC FABREGAS WENGER amesema ni ngumu kugundua mapema kuwa ameumia kiasi gani kwani wanatazamia kumfanyia uchunguzi leo.

= = =







Tenga atinga CAF


Rais wa TFF, Leodegar Tenga akipongezwa na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu la Uganda (FUFA) Lawrence Mulindwa mara baada ya kuchaguliwa Februari 23 mwaka huu kuwa mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Afrika (CAF) katika uchaguzi uliofanyika jijini Khartoum, Sudan.

Tuesday, February 22, 2011

BIG BROTHER AFRICA


ONE LAST CHANCE TO ENTER!
M-NET’S SEARCH FOR NEW HOUSEMATES FOR BIG BROTHER AFRICA 6 HEATS UP…
CAN YOU WIN USD 200 000?

February 2011

With the February 27 deadline looming and just a week left for wannabe entrants to submit their entries for BIG BROTHER AFRICA 6, M-Net has made an exciting announcement for all those people who have left it too late to enter!

With a vast amount of entries streaming in from across the 14 participating countries, M-Net has confirmed that it will also run open auditions in the different countries – so that those people who didn’t submit a paper entry, still get one last chance to try out for the new season.

“We’re extremely pleased with the response that this year’s call to entry has had,” says M-Net Africa Managing Director Biola Alabi. “Going into a 6th season, we knew that there would be interest but the scale of this interest has been quite phenomenal with over 5000 entries already received, certainly among the highest number of entries for any edition of Big Brother Africa.”

She goes on to say, “However, we’re aware that there are always people who leave it too late to enter and then arrive at the audition venues, where our teams are holding phase two audition sessions, to plead for a chance to try out. So this year, in addition to paper entries, we’ll also have open audition days. This way, if you submitted a paper entry, your entry has already been evaluated and successful candidates will be called and seen first at audition venues. But those people who didn’t do a paper entry will have one last chance to enter when our selection team is in the participating countries. They simply need to arrive at the audition venue on the relevant days.”

“But I would strongly suggest that people opt to submit a written entry. There’s still some time to do this! Your entry definitely gets priority with our selection teams who read through it in detail and are able to spend time working through the information. ”

To submit a written entry for the show, log on to www.mnetafrica.com/bigbrother and complete your entry form online. Or download an entry form from the website, complete and email it back to bba@endemol.co.za. The deadline for all written entries to be submitted is 27 February 2011 – so don’t delay.

Entry is open to would-be housemates who are 21-years or older, English speaking, have a valid passport and is a citizen of any one of the 14 participating countries (Angola, Botswana, Ethiopia, Ghana, Kenya, Malawi, Mozambique, Namibia, Nigeria, South Africa, Tanzania, Uganda, Zambia and Zimbabwe). Remember that all entrants must be tolerant of views and lifestyle choices other than their own and must have the social flexibility to live in close proximity with others.

BIG BROTHER AFRICA 6 begins on Sunday May 1 this year and once more, the dedicated DStv channel 198 will be providing 24/7 live coverage for the 91 day duration of the series.


Audition Dates and Venues:

COUNTRY

DATES

VENUE

Angola

3 - 5 March 2011

Skyna Hotel, Luanda

Botswana

28 February – March 1 2011

Grand Palm Hotel, Gaborone

Ethiopia

28 February - 2 March 2011

Hilton Addis Ababa Hotel

Ghana

28th February - 2 March 2011

Holiday Inn Hotel Accra Airport

Kenya

4 and 5 March 2011 (Nairobi)

6 March 2011 (Mombasa)

KICC, Nairobi

Little Theatre, Mombasa

Malawi

11 – 13 March 2011

Protea Ryalls Hotel, Blantyre

Mozambique

8 – 10 March 2011

Southern Sun Maputo

Namibia

28 February 2011 1 March 2011

The Playhouse, Windhoek

Nigeria

4 – 6 March 2011 (Lagos)


7th March 2011 (Abuja)

Protea Leadway Hotel Maryland Estate Ikeja, Lagos

Protea Hotel Asokoro, Abuja

South Africa

8th March 2011 DBN


9th March 2011 (CPT)


10 and 11 March 2011 (JHB)

Southern Sun Marine Parade (DBN)

Holiday Inn Express St. Georges Mall (CPT)

The Forum – Turbine Hall Newtown (JHB))

Tanzania

12 – 14 March 2011

Mövenpick Royal Palm Hotel,
Dar es Salaam

Uganda

8 – 10 March 2011

Sheraton Kampala

Zambia

7 and 8 March 2011

Golfview Hotel, Lusaka

Zimbabwe

4 – 6 March 2011

The Meikles Hotel, Harare



TIMU YA TAIFA YA VIJANA MIAKA 23 YATAGAZWA

Kikosi cha timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 23 cha kuivaa CAMEROON chatangazwa.

Kocha mkuu wa timu ya taifa vijana chini ya umri wa miaka 23 JAMHURI KIWELO (JULIO) ametangaza kikosi cha wa chezaji 25 wa kikosi hicho tayari kuikabili CAMEROON katika mchezo wa kuwani kufunzu kwa mashindano ya OLYMPIC jijini LONDON mwakani,mchezo huo wa awali utapigwa mjini YAOUNDE machi 26.

Akitangaza majini ya wachezaji wa kikosi hicho jijini dsm hii leo KIWELO amesema wachezaji wa kikosi hicho wamechanguliwa baada ya kuonyesha viwango vya hali ya juu katika mashindano mbalimbali yakiwemo yale ya timu za vijana chini ya umri wa miaka 20 za vilabu vya ligi kuu na fainali ya ligi daraja la kwanza yaliyomalizika jana jijini TANGA.

Kwa upande wake AFISA habari wa shirikisho la soka nchini TFF BONIFANCE WABURA amesema shirikisho lake linafanya kila jitihada kuhakikisha timu hiyo ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 23 inacheza michezo miwili ya kirafiki ya kimataifa ya kujipima nguvu kati ya MACHI 12 na 13 ama 19 na 20 kabla ya kuivaa timu ngumu ya CAMEROON.

Kikosi hicho kinaanza mazoezi kesho kabla ya kuweka kambi FEBRUARI 26 na kinatarajiwa kuondoka nchini kwenda CAMEROON Machi 22.

===
TFF yavitaka vilabu vilivyopanda daraja kujiandaa kwa ligi kuu

Shirikisho la soka nchini TFF limevitaka vilabu vya vinne vilivyopanda daraja hadi ligi kuu Tanzania bara kujiandaa vilivyo ili kukabili ushindani katika ligi hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini DSM Afisa Habari wa TFF, BONIFANCE WABURA amesema baada ya kupanda daraja hadi ligi kuu na kujipongeza kwa viongozi,wachezeja na mashabiki wa timu hizo kazi kwao sasa ni kujipanga vizuri ikiwa ni pamoja na kusajili wachezaji watakamudu heka heka za ligi kuu Tanzania bara msimu ujao.

Timu zilizopanda daraja kutoka ligi daraja la kwanza katika fainali zilizomalizika jana jijini tanga ni VILA SQUAD na MORO UNITED zote za DSM, COASTAL UNION ya TANGA na JKT OLJORO.

===
TIGO YAKABIDHI ZAWADI KWA WASHINDI
Kapuni ya simu za mkononi ya TIGO leo imekabidhi zawadi ya pessa taslimu zenye thamani ya shilingi miloni 22 kwa washindi 22 walioshinda katika promosheni ya bahatisha na tigo.
Akikabidhi zawadi hizo jijini DSM hii leo mwakilisho wa TIGO MASANJA REDEMPTUS amewataka wateja wa tigo kuendelea kushiriki katika bahati na sibu hiyo kwani zawadi bado ni nyingi.

Kwa upande wao washindi wa zawadi hizo LULU MOHAMED na PIUS MABULA hawakusita kuelezea furaha zao baada ya kukabidhiwa zawadi zao.

Hii ni mara ya nne kwa TIGO kukabidhi zawadi ya fedha taslimu tangu bahati na sibu hiyo ianze kuchezeshwa na inamalizika MACHI 28.
===

COSOTA Rukwa kufanya msako kusaka wezi wa kazi za wasanii.

Katika kuhakikisha kuwa wasanii wa muziki wananufaika na mauzo ya kazi zai chama cha haki miliki Tanzania (COSOTA)mkoani Rukwa kimeanza msako kwa wenye maduka ya kanda pamoja na wale wanaotembeza mitaani ikiwa pamoja na kuwapa elimu kutokana na wengi wao kutojua sheria za hati miliki.
Akizungumza na TBC mwakilishi wa COSOTA mkoa wa Rukwa Abuu Majeki amesema zoezi hilo limeshafanyika wilaya ya Mpanda huku wengi wa wafanyabiasahara wa kanda wakionyesha mwitikio mkubwa katika kutunza kazi za wasanii ikiwa pamoja na kuzigundua kazi feki wanazoletewa
Kwa upande wake moja ya mfanyabiashara wa kanda katika maduka ya Sumbawanga Godfrey Enock anasena bado wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwapo ya baadhi ya machinga kudurufu kazi na kuuza kwa bei ya chini tofauti na wao

===

ANCELOTTI ana matumaini na CHELSEA kufanya vizuri

TUANZE na ligi ya mabingwa Ulaya ambapo kocha wa CHELSEA, CARLO ANCELOTTI amesema timu bado ina uwezo mkubwa wa kufanya vizuri katika mashindano ya ULAYA ijapokuwa timu yake ipo katika wakati mgumu kimchezo kwa sasa.

Kombe la ligi ya mabingwa barani ULAYA ndio kimbilio la CHELSEA kwa sasa kwani imeondolewa katika mashindano ya kuwania kombe la FA na kwa sasa ipo katika nafasi ya tano kwenye msimamo wa ligi kuu nchini humo.

CHELSEA leo ipo ugenini kucheza na timu ya FC COPENHAGEN ya DENMARK katika mashindano ya ligi ya mabingwa barani ULAYA.

==
MOURINHO na kibarua kigumu dhidi ya LYON
HUKO UFARANSA, kocha wa REAL MADRID ya HISPANIA, JOSE MOURINHO, ana kibarua cha kuikabili timu ya UFARANSA ya OLYMPIC LYON.
Yenyewe REAL MADRID ina lengo la kucheza robo fainali ya mashindano hayo kwa msimu huu.
Katika kikosi cha MOURINHO amemjumuisha SERGIO CANALES na PEDRO LEON.
Lakini kuna mjadala kuwa ni nani atachezeshwa katika kambi ya ushambuliaji kati ya EMANUEL ADEBAYOR au KARIM BENZEMA.
Huku mlinda mlango IKER CASILLAS, akitarajia kurudi katika mchezo wa leo kuchukua nafasi ya ANTONIO ADAN, ambaye alikaa langoni jumamosi iliyopita baada ya CASILLAS kutumikia adhabu.
Michezo mingine itachezwa kesho kati ya INTER MILAN ya ITALIA itaikaribisha BAYERN MUNICH ya UJERUMAN na MARSEILLE ya UFARANSA itacheza na MANCHESTER UNITED ya UINGEREZA.
==
GATTUSO afungiwa mechi NNE

MCHEZAJI wa AC MILAN, GENNARO GATTUSO amefungiwa kutocheza michezo MINNE baada ya kuzozana na kumpiga kocha msaidizi wa timu ya TOTTENHAM, Joe Jordan wakati wa mchezo wao wa raundi ya kwanza ambapo AC MILAN ilifungwa.

Kiungo huyo alimpiga kichwa kocha huyo baada ya kipigo cha kufungwa goli MOJA kwa Sifuri katika uwanja wa SAN SIRO.

UEFA imepotoa adhabu hiyo jana , na tayari GATUSSO amekiri kosa lake na AC MILAN imesema haitakata rufaa kupinga maamuzi ya UEFA.
==
MONTELLA ateuliwa kocha wa muda ROMA

TIMU ya ROMA imemteua VINCENZO MONTELLA kuwa kocha wa timu hiyo hadi mwisho wa msimu huu baada ya kocha CLAUDIO RANIERI kujiuzulu.

MONTELLA, awali alikuwa ni kocha wa klabu hiyo upande wa vijana ambapo kocha huyo ataanza kibarua chake kwa kucheza ugenini dhidi ya timu ya BOLOGNA kesho katika mchezo wa ligi kuu soka nchini ITALIA.
Kujiuzulu kwa RANIERI,kunatokana na timu hiyo kufungwa mechi nne mfululizo na hivyo kuifanya timu hiyo kushikilia nafasi ya NANE katika msimamo wa ligi nchini humo.
MONTELLA amewahi kucheza katika klabu za FULHAM ya UINGEREZA.

==
WEST HAM yairarua BURNLEY

WEST HAM UNITED imeicharaza BURNLEY magoli MATANO kwa MOJA katika mashindano ya kombe la FA ya UINGEREZA.

Lakini leo kutakuwa na michezo miwili ya ligi kuu nchini UINGEREZA kati ya BLACKPOOL ambayo itacheza na TOTTENHAM.

Mchezo mwingine utakuwa ni kati ya ARSENAL ambayo itacheza na STOKE CITY.

==

Thursday, February 17, 2011

Michezo mbalimbali duniani

YANGA uso kwa uso na KAGERA.

YANGA leo inajarabu kutoa machungu ya kuondolea katika kombe la shirikisho barani Afrika na DEDEBET ya ETHIPIOA itakapo teremka dimbani kumenyana KAGERA SUKARI katika dimba la KAITABA jioni ya leo.

Iwapo YANGA itaibuka kidedea dhidi ya KAGERA itareja kileleni mwa ligi kuu Tanzania bara kwani itakuwa imejikusanyia ALAMA 35 nyuma ya SIMBA ambayo inaongoza ligi hiyo kwa sasa ikiwa na Alama 34.

Mabingwa wa kandanda WEKUNDU wa MSIMBAZI SIMBA wamepunguzwa kasi ya kuongeza ligi kuu ya kandanda Tanzania Bara baada ya sare ya magoli MAWILI kwa MAWILI na TOTO AFRIKA ya MWANZA.

Magoli ya SIMBA yamepachikwa wavuni na MBWANA SAMATA na goli la pili ni la kujifunga mwenyewe mlinda mlango wa TOTO AFRIKA WILBERT MWETA.

Magoli ya TOTO yamefungwa TETE KANG’ANG’A na goli la pili likifungwa na MOHAMED SUDI katika dakika ya lala na buriani.

AZAM FC jana nao waliendeleza ubabe wao wa kushinda michezo yake baada ya kuibungiza bila huruma AFRICAN LYON mabao matatu BILA.

Magoli ya AZAM yamefungwa na MRISHO NGASA, MAO MKAMI, na RAMADHANI CHOMBO RIDONDO

===

ARSENAL yaichapa BARCELONA

Ligi ya mabingwa barani ulaya imeendelea jana katika viwanja viwili tofauti jijini LONDON kwenye uwanja wa EMIRATES ambapo ARSENAL waliwakaribisha BARCELONA na kwenye uwanja wa STADIO OLIMPICO nchini ITALI kati ya AS ROMA na SHAKHTAR DONETSKY.

Tuanzie EMIRATES ambapo kulikua na mchezo wa kukata na shoka ARSENAL imewashangaza mashabiki wa BARCELONA baada ya kutoka nyuma goli moja na kuibuka na ushindi wa goli mbili kwa moja katika mchezo huo wa kwanza wa hatua ya 16 bora.

ARSENAL ndio waliokua wa kwanza kuanza kuleta kashikashi langoni mwa BARCA lakini shuti la ROBIN VAN PERSIE liliokolewa na kipa wa BARCA VICTOR VALDES.

LIONEL MESSI almanusura aipatie BARCA goli la kuongoza lakini mpira alioupiga ulikwenda nje sentimeta chache.

LIONEL MESSI tena aliendelea kuisumbua ngome ya ARSENAL safari hii akipenyeza pasi safi iliyomkuta DAVID VILLA ambaye hakufanya hajizi na kuandika goli la kuongoza kwa BARCA katika dakika ya 25.

BARCA tena wakapata goli la pili lakini mwamuzi wa pembeni alionesha kibendera juu kuashiria kuwa mfungaji alikua tayari ameshaotea.

Kipindi cha pili ARSENAL ilikuja juu kutaka kusawazisha goli hilo na juhudi zao zikazaa matunda katika dakika ya 77 pale GAEL CLISHY alipompa pasi ROBIN VAN PERSIE ambaye aliachia shuti kali lililokwenda moja kwa moja wavuni.

Dakika ya 82 ANDREI ASHARVIN aliwanyanyua tena mashabiki wa ARSENAL kwa kuandika goli la pili na la ushindi kwa timu yake baada ya kutokea shambulizi la kushitukiza ambapo NASRI alimpatia ASHARVIN pasi ya goli.

Hii ni mara ya kwanza kwa ARSENAL kushinda dhidi ya BARCELONA na timu hizi zitakutana tena katika mchezo wa pili wa hatua hii ya 16 bora baada ya wiki tatu CAMP NOU.
= = = = = = =

Kwenye uwanja wa STADIO OLIMPICO AS ROMA wakiwa nyumbani wameshindwa kuutumia vyema uwanja wao baada ya kupata kichapo cha goli 3 kwa 2 dhidi ya SHAKHTAR DONETSKY.

ROMA walianza walikosa goli kwenye dakika ya 20 baada ya mchezaji wake kupiga kichwa kilichokwenda nje.

Kwenye dakika ya 28 ROMA walipata goli la kuongoza baada ya mchezaji wa SHAKHTAR RAZVAN RAT kujifunga.

SHAKHTAR walisawazisha goli hilo kwenye dakika ya 29 ikiwa ni dakika moja tu mfungaji akiwa ni JADSON.

Wageni hao hawakutosheka kwani walipata goli la pili kwenye dakika ya 36 mfungaji akiwa DOUGLAS COSTA kabla ya LUIS ADRIANO kufunga goli la tatu kwenye dakika ya 41.

Katika kipindi cha pili ROMA walifanikiwa kupata goli la pili JEREMY MENEZ akiachia shuti kali lililokwenda moja kwa moja wavuni.

Hadi mwisho wa mchezo SHAKHTAR 3 AS ROMA 2.
= = = = = = = =

FIFA yataka vilabu kutimiza vigezo ili kushiriki mashindano ya kimataifa

Vilabu vya soka hapa nchini vimetakiwa kuanza mchakato wa kutekeleza vigezo vinavyotakiwa na shirikisho la soka la kimataifa FIFA ili viweze kupewa leseni ya kushiriki kwenye mashindano mbalimbali ya kimataifa.

Moja ya wakufunzi wanaoendesha semina ya FIFA kwa viongozi wa vilabu hapa nchini HENRY TANDAU anasema FIFA imejiwekea malengo ya miaka michache ijayo ya kuhakikisha kila klabu inakidhi vigezo 13 vya FIFA ili vilabu hivyo viweze kutambuliwa na chombo hicho cha juu cha soka duniani.

TANDAU ametaja baadhi ya vigezo vinavyotakiwa kutekelezwa na vilabu kuwa ni pamoja na ukaguzi wa mahesabu, klabu itambuliwe kisheria, klabu iwe na ofisi inayotambulika, klabu iwe watendaji wa kuajiriwa, iwe na uwanja, shule ya kukuza vipaji na masuala mengine.

Baada ya somo hili baadhi ya wasemaji wa vilabu akiwemo ANDREW CHATWANGA wa MAJIMAJI na LEONARD KIJANGWA wa POLISI TANZANIA wanasema wana imani vilabu vyao vitatekeleza maagizo haya FIFA.

Hata hivyo cha ajabu ni kwamba kati ya vilabu 12 vinavyoshiriki ligi kuu, ni vilabu sita tu vya SIMBA, YANGA, MAJIMAJI, POLISI TANZANIA,AFRICAN LYON,na AZAM FC vinashiriki.
= = =

CONTADOR arejea kwenye mbio za baiskeli.

Bingwa wa mbio za TOUR DE FRANCE ALBERTO CONTADOR amerejea katika mashindano ya kuendesha baiskeli katika mbio za TOUR DE ALGARVE hapo jana baada ya kushinda rufaa yake dhidi ya kufungiwa mwaka mmoja kutokana na madawa.

CONTADOR alifungiwa kwa muda baada ya kugundulika ametumia madawa ya kuongeza nguvu katika mbio za TOUR DE FRANCE za mwaka jana.

CONTADOR amesema anafurahia kurejea tena katika mashindano hayo na kuongeza kuwa kurejea kwake kumeleta faraja sio tu kwake bali pia kwa timu pamoja na wadhamini wake.

CONTADOR mwenye miaka 28 amekua akisema kuwa hana hatia na kudai kuwa nyama aliyokula iliyokua imechanganywa na vitu ndio sababu ya kushindwa kwa kipimo chake.

= = = = == ===
MURRAY AJITOTA KUWANIA UBINGWA WA TENESI WA DUBAI

Mchezaji nambari moja wa tenesi wa UINGEREZA ANDY MURRAY amejitoa kushiriki katika mashindano ya wazi ya tenesi ya Dubai kutokana na maumivu ya kiuno.

Murray ambaye amecheza fainali mara moja ya US Open na mara mbili Australian Open alipanga kupumzika baada ya kushindwa katika mchezo wa fainali ya Australian Open mwezi uliopita lakini akaona ageweza kucheza mashindano hayo ya DUBAI lakini maumivu yamemzuia kufanya hivyo.

Murray ambaye ni mchezaji namba tano kwa ubora wa tenesi duniani alishiriki mashindano hayo ya DUBAI mwaka jana ikiwa ni baada ya kupoteza mchezo wake wa fainali ya mashindano ya wazi ya AUSTRALIA.

===