Wednesday, October 10, 2012


Klabu ya SIMBA yawasili jijini TANGA.
KATIKA hatua nyingine mabingwa wa soka nchini SIMBA ya DSM imewasili mjini TANGA tayari kwa mchezo wao wa ligi kuu soka Tanzania bara dhidi ya wenyeji wa COSTAL UNION mchezo utakaochezwa katika uwanja wa MKWAKWANI mjini humo siku ya jumamosi.
Msemaji wa klabu ya SIMBA, EZEKIEL KAMWAGA amewataka mashabiki wa klabu hiyo kutojiingiza katika vitendo vitakavyosababisha klabu hiyo kutozwa faini.
Kiungo wa simba RAMADHANI CHOMBO REDONDO hakuondoka na kikosi cha SIMBA kwenda TANGA kwa kuwa anasubuliwa na MALARIA,lakini akaeleza kurejea kwa mshambuliaji wa timu hiyo MRISHO NGASSA ambaye atacheza katika mchezo huo.
Michezo mingine itakayochezwa jumamosi ni katika uwanja wa JAMHURI mjini MOROGORO ambapo POLISI MORO itacheza na AZAM FC, TANZANIA PRISONS itacheza na JKT OLJORO.
Michezo mingine RUVU SHOOTING itacheza na AFRICA LYON na MTIBWA SUGAR itacheza na MGAMBO JKT.
====
Wagombea sita soka la wanawake wapingwa
WAGOMBEA sita wa nafasi mbalimbali za uongozi katika Chama cha Mpira wa Miguu wa Wanawake Tanzania (TWFA) wamewekewa pingamizi na wadau wa mchezo huo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TWFA, Ombeni Zavala, wagombea hao ni JOAN MINJA anayewania nafasi ya Mwenyekiti ambaye amewekwa pingamizi na wadau sita. Pia ISABELLAH KAPERA ambaye anagombea uenyekiti amewekewa pingamizi moja.

Wagombea watatu wa nafasi ya Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) nao wamewekewa pingamizi.

Wagombea hao ni JULLIET MNDEME ana pingamizi sita , Zena Chande ana pingamizi NNE na Jasmin Soud mwenye pingamizi tatu.

Naye Rahim Maguza anayewania ujumbe wa Kamati ya Utendaji amewekewa pingamizi moja.

Licha ya pingamizi hizo, wagombea wote wanatakiwa kuhudhuria usaili wakiwa na vyeti vyao halisi vya kitaaluma utakaofanyika Oktoba 12, 13 na 14 mwaka huu kwenye ofisi za TFF zilizopo Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam kuanzia saa 3 asubuhi.
 ===

JOKATE azindua ubunifu mpya wa mitindo.
MWANAMITINDO na MBUNIFU nchini JOKATE MWEGELO amezindua aina nyingine ya mitindo ya NYWELE inayokwenda sambamba na mitindo ya ubunifu wa nguo.
JOKETI ambaye pia aliwahi kuwa mshindi wa pili katika shindano la Taifa kwa mwaka 2006 amesema nia yake ni kutaka kutanua wigo wa ubunifu kwa kutumia fani ya urembo.
Akizundua kampuni hiyo JOKATE akaeleza kwa nini ameiita jina la KIDOTI.
Kisha akaeleza madhumuni  ya kuazisha kampuni  hiyo katika tasinia ya urembo,ubunifu na mitindo hapa nchini.
Baada ya hapo warembo wakajimwanga jukwaani kuonyesha mitindo ya nywele


CHEKA kuwania ubingwa wa DUNIA dhidi ya mjerumani.
BINGWA wa ngumi za kulipwa nchini anayetambuliwa na shirikisho la ngumi la dunia (UBO) FRANCIS CHEKA amesaini mkataba wa kucheza pambano la kuwania ubingwa unaotambuliwa na shirikisho la ngumi la IBF uzito wa kati.
Katika pambano hilo CHEKA ambaye hivi karibuni alimchakaza KARAMA NYILAWILA kwa KO na kupata ubingwa wa UBO sasa atacheza na bondia kutoka nchini JERUMAN, BENARD SIMON katika pambano litakalochezwa nchini UJERUMAN NOVEMBA 17 mwaka huu.
BONDIA, CHEKA anasaini mkataba kwaajili ya kucheza pambano dhidi ya mjerumani BERNARD SIMON.
Pambano hilo limetafutwa na promota mpya wa FRANCIS CHEKA, JUMA MABAKILA mwenyewe akisema anataka, kila baada ya miezi miwili bondia CHEKA kupanda ulingoni.
Rais wa shirikisho la ngumi, IBF AFRICA ONESMO NGOWI naye akazungumzia pambano jingine la OMAN ambalo FRANCIS CHEKA atazichapa baada ya pambano na MJERUMAN
Tayari FRANCIS CHEKA amejizolewa sifa nyingi katika masumbwi nchini baada ya kuwachapa mabondia mashuhuri kama KARAMA NYILAWILA, MADA MAUGO na RASHID MATUMLA.

Saturday, April 21, 2012

NGORONGORO HEROES yaichapa SUDAN

Katika michezo tuanzie na taarifa ya hapa nyumbani ambapo TIMU ya Taifa ya vijana NGORONGORO HEROES jana imefanikiwa kuanza vizuri hazma yake ya kutaka kucheza fainali za mashindano ya mataifa ya Afrika kwa kuichapa timu ya SUDAN mabao MATATU kwa MOJA katika mchezo wa awali uliochezwa kwenye uwanja wa Taifa Jijini DSM.

Mabao ya Ngorongoro Heroes yamefunga na THOMAS ULIMWENGU,RAMADHAN SINGANO MESSI na SAIMON MSUVA

===

ARSENAL yatoka suluhu na CHELSEA

LIGI kuu ya ENGLAND iliendelea jana ambapo michezo MITANO ilichezwa katika viwanja tofauti.

Katika uwanja wa EMIRATES, uwanja wa ARSENAL, Timu ya ARSENAL ililazimishwa suluhu na CHELSEA.

Katika mchezo huo timu zote zilikosa magoli katika nyakati tofauti ambapo VAN PERSIE alikosa nafasi TATU za kupachika magoli wakati mshambuliaji wa CHELSEA, DANIEL STURIDGE naye akikosa nafasi kadhaa za kupachika magoli.

Kocha DI MATTEO wa CHELSEA hakumchezesha DIDIER DROGBA na badala yake akamchezesha FERNANDO TORRES.

Kutokana na matokeo hayo, ARSENAL imesalia katika nafasi yake ya TATU ikiwa imebakiza michezo yake MITATU ikiwa na pointi 65.huku CHELSEA ikiwa katika nafasi ya SITA na pointi zao 58.

==

NEWCASTLE na FULHAM zashinda

Nayo NEWCASTLE UNITED imeicharaza STOKE CITY magoli MATATU kwa BILA katika mfululizo wa ligi hiyo.

Magoli ya NEWCASTLE UNITED yamepachikwa na YOHAN CABAYE ambaye aliipachikia timu yake magoli MAWILI na goli jingine likafungwa na PAPIS CISSE.

FULHAM ikiwa nyumbani nayo imefanikiwa kuchomoza na ushindi wa magoli MAWILI kwa MOJA dhidi ya timu ya WIGAN ATHELETIC.

NEWCASTLE imefikisha pointi 62, wakati FULHAM yenyewe ina pointi 46.

===

Leo MNCHESTER UNITED na EVERTON, MAN CITY na WOLVES

LIGI ya ENGLAND inaendelea leo kwa mchezo kati ya MANCHESTER UNITED itakayocheza na EVERTON.

MANCHESTER UNITED haina majeruhi wapya , na RIO FERDINAND anatarajia kucheza mchezo wa 450 katika historia yake ya kucheza michezo mbalimbali ya soka, huku ASHLEY YOUNG yeye ukiwa ni mchezo wa 200 tangu aanze kucheza soka la kulipwa.

Kwa upande wa EVERTON , wao watamkosa beki wake LEIGHTON BAINES kutokana na kuwa majeruhi aliopata wakati wa mchezo wa wiki iliyopita wa kombe la FA ambao walifungwa na LIVERPOOL .

Pia huenda mchezaji wa kimataifa wa Afrika Kusini STEVEN PIENAAR akacheza mchezo huo dhidi ya MANCHESTER UNITED utakaochezwa katika uwanja wa OLD TRAFFORD.

Michezo mingine LIVERPOOL itacheza na WEST BROM , WOLVES inaikaribisha MANCHESTER CITY.

Msimamo wa ligi ya ENGLAND, MANCHESTER UNITED inaongoza ikiwa na pointi 82 ikifuatiwa na MANCHESTER CITY ambayo nayo ina pointi 77 ikiwa katika nafasi ya pili.

==

Fainali ligi ya taifa ya kikapu ngazi ya vilabu kufanyika leo

LEO ni fainali ya mashindano ya ligi ya taifa , ambapo timu za kikapu za ABC na SAVIO zitaonyeshana kazi kutafuta bingwa wa mashindano hayo upande wa wanaume.

Wakati upande wa wanawake kutafanyika fainali kati ya JESHI STARS na RED LIONS katika michezo itakayochezwa kwenye uwanja wa ndani jijini DSM