Tuesday, October 26, 2010

Pweza matabiri afaraiki dunia

Yule pweza POUL aliyepata umaarufu kwa kutabiri katika fainali za kombe la dunia zilizomalizika AFRIKA KUSINI JULY 2010 amefariki dunia akiwa na umri wa miaka miwili

MEDALI kuongelea


Medali kuongelea wakionyesha dhahabu

SIMBA na YANGA viwanjani kesho

Ligi kuu Tanzania bara Yanga na Simba viwanjani kesho

Ligi kuu Tanzania bara kuendele kesho katika viwanja vinne kuwaka moto huku watani wa jadi SIMBA na YANGA wakisaka ALAMA mhimu ili kujikita kileleni mwa ligi hiyo.

Mabingwa watetezi SIMBA wao wamesafiri hadi mkoani kagera kuivaa KAGERA SUKARI katika dimba la KAITABA wakati YANGA wao watakuwa wenyeji wa AFRICAN LYON katika dimba la JAMHURI MKOANI MOROGORO.

MICHEZO MINGINE wauza lambalamba AZAM FC watakuwa wageni wa MAAFADE wa POLISI TANZANIA katika uwanja wa JAMHURI mkoani MOROGORO huku wakata miwa MTIBWA SUKARI wataikaribisha timu inayoburuza mkia katika ligi hiyo ARUSHA FC katika uwanja wa MANUNGU huko turiani mkoani MOROGORO.

YANGA ipo kileleni mwa ligi hiyo ikiwa na Alama 21 sawa na bingwa mtetezi SIMBA lakini YANGA inaogoza kwa sababu ya tofauti ya magoli ya kufunga na kufunga na SIMBA.

Timu ya taifa ya Gofu kutamba michuano ya dunia

Wachezaji watatu wa timu ya taifa ya GOFU ya TANZANIA wanaotarajiwa kuteremka dimbani kupeperusha bendera ya taifa katika michuano ya dunia ya GOFU inayofanyika kesho kutwa siku ya ALHAMISI huko ARGERTINA wanamatumaini ya kufanya vema katika michuano hiyo.

Akizungumza na TBC Afisa tawala wa chama cha GOFU Tanzania TGU, SOPHIA NYANJERA amesema wachezaji hao wamefika salama ARGERTINA na wamefanya mazoezi katika viwanja yatakapo fanyika mashindano hayo ya GOFU ya dunia ili kuzoea hali ya hewa kabla ya kuanza kinyang’anyiro cha kutafuta ubingwa wa Dunia.

Wakati timu ya taifa ya GOFU kwa wanaume ikijiandaa kucheza katika mashindano hayo wezao akina dada wametoka kapa baada ya kumaliza katika nafazi ya 51 katika nchi 52 zilizoshiriki mashindano ya GOFU ya dunia kwa wanawake yaliyomalizika mwishoni mwa wiki huku ARGERTINA.

====

Stingrays yatwaa medali sabini na nne nchini Malawi.

Klabu ya kuogelea ya STINGRAYS aliyoshiriki mashindano ya MWALIKO WA MALAWI Kuanzia October 22 hadi 23 nchini MALAWI imerudi na medali SABINI na Nne na kufanikiwa kuwakilishwa vyema TANZANIA katika mashindano hayo.

Akizungumza mara baada ya kuwasili wakitokea nchini MALAWI mkuu wa msafara wa timu hiyo RAMADHANI NAMKOVEKA amesema haikuwa kazi ngumu kutwaa medali hizo kwani waogeleaji kutoka nchini zilizoshiriki mashindano hayo zilikuwa zimejiandaa vizuri.

Mchezaji CHRISTIAN OPPERMAN amejinyakulia medali saba peke yake akishiriki katika staili tofauti katika mashindano hayo.

Kwa upande wake mkurugenzi wa ufundi wa chama cha kuogelea TSA MARCELINO NGALIOMA amesema kwa medali walizopata waogeleaji hao zimeiletea sifa TANZANIA hivyo ni jukumu la timu zingine kuiga mfano wa klabu ya STINGRAYS.

Kocha wa klbu hiyo LEILANI CORREIA amesema kiwango walichoonyesha wachezaji hao kinampa matumaini ya kufanya vizuri katika mashindno ya muungano nay a kimataifa yatakayofanyika nchini BOSTWAN.


Yanga yang'aka


YANGA yakanusha kutimua wachezaji wake

Klabu ya YANGA imekanusha uvumi uliosambaa juu ya kutimuliwa kwa wachezaji wake wawili MOHAMED MBEGU na ERNEST BOAKYE huku usajili wa mshambuliaji KENETH ASAMOOH kufanyika mwezi ujao.

akizungumza na waandishi habari jijini DSM hii leo afisa habari wa YANGA LUIS SENDEU amesema kuwa MOHAMED MBEGU ameondolewa kambini kutokana na utovu wa nidhamu na suala lake linachunguzwa na kamati ya nidhamu ya YANGA, kwa upande wa ERNEST BOAKYE anasumbuliwa na maumivu ya tumbo yaliyomtokea kabla ya mechi yao dhidi ya AZAMU FC na yuko hospitali anaendelea na matibabu.

SENDEU amesema usajili wa mshambuliaji wa timu hiyo mghana KENETH ASAMOOH utafanyika katika dirisha dogo la usajili linaloanza NOVEMBA MOSI kwa kufuata kanuni na taratibu mpya za usajli za FIFA.

Kwa upande wa kocha wa YANGA KOSTADINI PAPIC, SENDEU amesema suala lake la mkataba mpya linakamilishwa na kwamba hajatimuliwa kuinoa klabu hiyo kama ilivovumishwa na baadhi ya VYOMBO vya habari, SIYO TBC.


Thursday, October 21, 2010

Wake wa viongozi kambini TWIGA STARS


Twiga Stars walipotembelewa na wake wa viongozi wiki iliyopita



Mitindo



SWAHILI FASHION 2010

mziki


Ally Kiba huyu marekani kurikodi nyimbo na wanamziki wengine wa 7 wataaunda kundi liitwalo ONE8

Supa PESA

Wednesday, October 20, 2010

habari za tz

WANAMITINDO chipukizi WANANE watakuwa miongoni mwa wanamitindo 32 kutoka katika nchi za AFRIKA ya MASHARIKA ambao watampambana katika shindano la maonyesho na ubunifu la SWAHILI FASHION 2010 .

Mratibu wa onyesho hilo MUSTAFA HASANALI amesema kati ya wanamitindo hao wanamitindo 24 ni wale wenye uzoefu katika fani ya ubunifu kutoka mataifa ya RWANDA , TANZANIA , BURUNDI , KENYA na UGANDA

Mbali na masuala ya ubunifu , pia onyesho hilo litahusisha utamaduni wa vyakula na mavazi ya makabila mbalimbali nchini.

=

MWANAMZIKI wa miondoko ya BONGO FLEVA, ALLY KIBA anaondoka nchini keshokutwa kwenda nchini MAREKANI ambapo anaungana na wanamuziki wengine SABA kutoka AFRIKA ambao wataimba na nyota wa MAREKANI.

Maratibu kutoka kampuni ya ROCKSTAR, CHRISTINE MOSHA amesema msanii KIBA na wenzake wa Afrika wataunda kundi linalojulikana kama ONE-EIGHT

Katika kundi kila msanii ataimba kwa lugha yake ambapo ALI KIBA yeye ataimba kwa lugha ya Kiswahili.

Wanamuziki wengine ni AMANI kutoka KENYA, NAVIO kutoka UGANDA , FALLY IPUPA kutoka DR CONGO , 2FACE kutoka NIGERIA, JK kutoka ZAMBIA, FOUR TIMES kutoka GHANA na MOVAIZHALEINE kutoka GABON.

==

Wakazi wawili wa jijini la DSM, GRACE BIKO na MUSA SULEIMAN kwa nyakati tofauti wameendelea kushinda katika shindano la bahati nasibu la SUPA PESA.

Mkazi GRACE BIKO yeye amejishindia kiasi cha shilingi MILIONI KUMI, wakati SELEMAN yeye akizoa kitita cha shilingi MILIONI MOJA.

GRACE BIKO anakua ni mshindi wa nne kujinyakulia kitita cha shilingi MILIONI KUMI katika bahati nasibu ya SUPA PESA.

===

Tuesday, October 19, 2010

Washiriki wa BIG BROTHER


Michezo leo

TFF kuwapinga msasa makocha wa ligi kuu Tanzania bara.
Shirikisho la soka nchini TFF kuwapinga msasa makocha wa ligi kuu Tanzania bara na wakufunzi wa mikoa ili kuwaweze kufika viwango vya shirikisho la soka barani Afrika CAF mwezi ujao.
Akizungumza na waandishi habari katika ofisi za TFF kaimu katibu mkuu wa TFF SUNDAY KAYUNI amesema, kozi hiyo ni kutekeleza maagizo ya CAF yaliyotolewa wiki iliyopita katika mkutano wa CAF na FIFA nchini MISRI ambapo CAF imetoa miaka minne tu kwa makocha kuhakikisha wamefiki madaja ya A,B na C ili waendelea kufundisha soka hapa nchini.
KAYUNI ameasema FIFA na CAF makocha wa timu za taifa wametakiwa kuwajumuisha wachezaji chipukizi katika timu zao za taifa ili kufanya vema katika michuano mabalimbali na kutolea mfano kwa timu za GHANA na Ujerumani kwamba zilifika mbali katika fainali za kombe la dunia kutokana na kutumia wachezaji chipukizi.
Mkutano wa FIFA na CAF uliomalizaika jijini CAIRO MISRI wiki ilyopita ulikuwa wa kutathimini fainali za kombe la dunia zilizomalizika AFRIKA KUSINI mwezi JULY.
====
TFF kuendesha ligi ya soka kwa shule za sekondari DSM
Shirikisho la mpira wa mguu nchini TFF limeamua kuendesha ligi maalumu ya soka kwa shule za sekondari za mkoa wa DSM ikiwa ni jaribio lake la kukuza kiwango cha soka hapa chini na yataanza kutimu vumbi jumamosi ya wiki ijayo katika viwanja vitatu jijini dsm.
Akizungumza jijini DSM hii leo kaimu katibu mkuu wa TFF SUNDAY KAYUNI amesema,shirikisho hilo limeamua kufanya hivyo ili kuonyesha mfano wa kuibua na kundeleza vipaji vya wachezaji chipukizi hapa nchini.
Kayuni amesema michuano hiyo itachezeshwa na marefa chipukizi na wasoni kwa lego la kuinua viwango vyao ili kuwa na marefa wenye ujuzi kwa faida ya soka la tanzania.
Shule 12 za wanaume na sita za wasichana kutoka kutoka katika mikoa ya kisoka ya KINONDONI,ILALA na TEMEKE.
====
BFT yasema ukosefu wa michezo ya kimataifa chazo cha kuboronga Madola
Ukosefu wa michezo za kimataifa na matumizi ya kopyuta vyatajwa kama sababu zilizosababisha mabondia wa Tanzania kuboronga katika michezo ya Jumuiya ya Madola iliyomalizaka wiki iliyopita nchini INDIA.
Akizungumza jijini DSM hii leo, Makamu rais wa BFT MICHEAL CHANGARAWE amesema ukosefu wa michezo ya kimataifa na matumizi ya kopyuta wakati wa mazoezi ndio zimekua sababu kubwa za kushindwa kutamba kwa mabodia wa Tanzania katika michezo ya MADOLA.
Changarawe amesema uongozi uliopita wa BFT ulipewa kopyuta na shirikisho la ngumi la dunia AIBA lakini haijulikani ilipo mpaka sasa kwani uongozi mpya haujakabidhiwa.
Changarawe amesema ili kuondokana na aibu iliyotokea India isitokea katika mashindano yajayo ya OLMPIKI yatakayofanyika UINGEREZA mwaka 2012 watafanya michuano ya kitaifa ili kutafuta mabondia chipukizi.
Ni kukumbushe tu kwamba timu ya Tanzania iliyoshiriki katika michezo ya YUMUIYA ya MADOLA haikuabulia medali hata moja.

====
Mrembo YARA wa PURTO RICO angara na vazi la ufukweni
MREMBO wa PURTO RICO, YARA SANTIAGO ameibuka mshindi katika shindano la dunia la ufukwe lililofanyika katika mji wa SANYA nchini CHINA ikiwa ni mwelekeo wa kuelekea fainali ya shindano hilo la dunia mwisho wa mwezi huu.
YARA SANTIAGO, amewashinda warembo wengine ISHIRINI waliongia fainali na mshindi wa pili ni kutoka MAREKANI, ambapo mrembo ALEXADRIA MILLS alimfuata kwa karibu mrembo YARA.
Mshindi wa tatu katika shindano hilo ni MARIANN BIRKEDAL kutoka nchini NORWAY.
Mrembo wa Tanzania katika mashindano hayo GENEVIVE MPANGALA hakufanikiwa kuingia katika AROBAINI BORA kwani ni mrembo wa GHANA na CAPE VERDE walipata tiketi ya kuingia hatua ya AROBAINI BORA na kushindwa kufua dafu katika hatua ya nusu fainali.
Ushindani wa ufukwe ni moja ya vitu vinavyofuatiliwa na waandaaji hao kwani inatoa alama zinazoweza kusaidia hatua ya fainali.

==
CHELSEA VS SPARTAK MOSCOW
MICHEZO ya ligi ya mabingwa barani Ulaya (UEFA) inaendelea leo ambapo CHELSEA ipo ugenini nchini URUSI kucheza na SPARTAK MOSCOW katika mchezo wa kundi F.
Kocha wa CHELSEA, CARLO ANCELOTTI amebainisha kuwakosa akina DIDIER DROGBA ambaye anaumwa pamoja na FRANK LAMPARD ambaye anasumbuliwa na HERNIA.
Huku ANCELOTTI, akisema washambuliaji wake DANIEL STURRIDGE na SOLOMON KALOU kuwa wapo tayari kwa mchezo wa leo.
==
ANCELOTTI akanusha kutaka kumsaini ROONEY
Katika hatua nyingine kocha ANCELOTTI amekanusha tetesi kuwa klabu yake inataka kumchukua mshmabuliaji wa MANCHESTER UNITED, WAYNE ROONEY.
Mkataba wa ROONEY ambaye ana miaka 24, unamalizika mwaka 2012 na imeripotiwa hakuna mazungumzo yoyote yaliyofanywa kati yake na mshambuliaji huyo wa MANCHESTER UNITED.
Mbali na CHELSEA ambayo ilikuwa ikidhaniwa kumnyemelea mshambuliaji huyo , pia MANCHESTER CITY na REAL MADRID ni vilabu ambavyo vimetajwa kuwa na nia ya kumnyakuwa mshambuliaji huyo, ijapokuwa kocha wa REAL MADRID , JOSE MOURINHO ametabiri kwa kusema kuwa hafikirii kama ROONEY ataiacha klabu yake.
==
FABREGAS yupo fiti mchezo wa leo
NAHODHA wa timu ya ARSENAL, CESC FABREGAS amerejea uwanjani na leo atakuwepo katika kikosi cha ARSENAL kitakaocheza na SHAKHTAR DONETSK katika uwanja wa nyumbani wa Emirates.
Kiungo huyo wa HISPANIA, hajacheza tangu awe majeruhi tangu septemba 18 pale alipoichezea timu yake na kuumia wakati wa mchezo dhidi ya SUNDERLAND.

Wachezaji wengine ambao wako fiti kwa mchezo wa leo ni pamoja na NICKLAS BENDTNER na THEO WALCOTT.

Huku ARSENAL ikiwa na majeruhi lukuki kama LAURENT KOSCIELNY, BACARY SAGNA na THOMAS VERMAELEN.

Wengine majeruhi ni AARON RAMSEY na ROBIN VAN PERSIE, ila kocha WENGER anategemea kumchezesha JACK WILSHERE.

==
RANIERI asema ana uhusiano mzuri na TOTTI
Naye Kocha wa timu ya AS Roma CLAUDIO RANIERI amemsifia nahodha wa timu yake FRANCESCO TOTTI kwamba bado ana umuhimu wake katika timu ijapokuwa TOTTI inaelezwa kuwa na umri mkubwa kwa kuwa kiwango chake kimekwisha.
RANIERI, ameyasema hayo wakati wa mkutano na waandishi wa habari ambpo timu yake leo inacheza na FC BASEL.
Pia amekanusha kutokuwa na uhusiano mzuri na mchezaji wake TOTTI pamoja na wachezaji wengine wa timu hiyo.
Michezo mingine ya kundi E, BAYERN MUNICH itacheza na CFJ CLUJ, MALSEILLE itacheza na ZILINA katika mchezo wa kundi F.
Kundi G, AJAX inaikaribirisha AUXERRE, REAL MADRID inacheza na AC MILAN na kundi H kutrakuwa na mchezo kati ya SPORTING BRAGA itacheza na PARTIZAN BELGRADE.
==
Mwanaridha LASHAWN MERRITT afungiwa
MWANARIADHA bingwa wa OLYMPIC na wa dunia wa mita 400, LASHAWN MERRITT amefungiwa kwa miaka miwili baada ya kukutwa akitumia dawa za kuongeza nguvu michezoni.
MERRITT, kutoka MAREKANI alipimwa mara tatu na kukutwa anatumia dawa hizo katika kipindi cha OKTOBA 2009 hadi JANUARI mwaka huu.
Kutokana na kufungiwa huko sasa, mwanariadha huyo huenda akarejea tena mwakani wakati wa mashindano ya dunia yatakayofanyika mwezi wa NANE.
MERRITT, alishinda mita 400 wakati wa mashindano ya OLYMPIC yaliyofanyika BEIJING.
==