Tuesday, June 28, 2011

MIichezo ya leo

WEKUNDU wa MSIMBAZI SIMBA katika michuano ya kombe la KAGAME, lazima kieleweke watakapocheza na ZANZIBAR OCEAN VIEW.

SIMBA walioko kwenye kundi A wana pointi MOJA tu bila goli, wakati ZANZIBAR OCEAN VIEW wao ndo vinara wa kundi hili wakiwa na pointi SITA na magoli MATANO ya kufunga na wamefungwa magoli MAWILI tu, na kama watashinda leo ama kutoka sare watakuwa wamekata tiketi ya kucheza hatua ya robo fainali.

SIMBA ni watanzania, ZANZIBAR OCEAN VIEW ni watanzania pia, sasa hapa sijui kutakuwa na udugu ama tikiwa uwanjani hakuna udugu?

= = =

Jana kulikuwa na mechi mbili za Kombe la KAGAME na kule MOROGORO klabu ya soka ya ST.GEORGE ya ETHIOPIA imecheza na ULINZI ya KENYA.

Timu hizi zimefungana goli MOJA kwa MOJA.

Walianza ST.GEORGE kufunga na ndipo wakasawazisha ULINZI na habari zinasema ULINZI walizembea wenyewe katika kipindi cha pili cha mchezo kwasababu walipata nafasi za kufunga wakashindwa kuzitumia.

Jijini DSM BUNAMWAYA ya UGANDA imeionesha kazi ELMAN FC ya SOMALIA kwa kuinyuka kwa magoli MANNE kwa BILA, na hii ni mechi ya kundi Be ambapo hapo kesho ELMAN itakutana na YANGA.

YANGA nao wanakazi ya kufanya kwa kweli kwasababu walitoka sare ya magoli MAWILI kwa MAWILI na klabu tya EL MEREIKH ya SUDAN, klabu inayotajwa kwamba mpaka sasa ndio iliyoonesha soka safi na la kuvutia na ukomavu wa uwanjani.

Wapachikaji wa magoli wa YANGA JERY TEGETE, na KENETH ASAMOAH ni majeruhi mpaka sasa, hivyo kabaki DAVIS MWAPE peke yake japokuwa kuna habari zinazodai mpachika magoli wa YANGA mpya KIZZA HAMIS kutoka UGANDA angefika nchini jana.

= = =

Leo katika jambo SPORTS tunaipongeza KANDA YA NYANDA ZA JUU KUSINI ya UMISETA, Umoja wa Michezo Shule za Sekondari kwa kuchaguliwa kuunda timu itakayowakilisha TANZANIA kwenye michezo ya Umoja wa shule za sekondari AFRIKA MASHARIKI itakayofanyika nchini UGANDA mwezi JULAI mwaka huu.

Wachezaji hawa chipukizi wa mikoa ya MBEYA, IRINGA na SONGEA wanaunda timu ya wachezaji 20 wa kandanda na wachezaji WATANO wanariadha.

HOSEA CHEYO kutoka MBEYA amekutana na kikosi hiki kilichorejea nyumbani baada ya kumalizika kwa mashindano pale KIBAHA mkoani PWANI.

= = =

Mama ASHA BARAKA mdau mkubwa wa muziki wa dansi hapa nchini ambaye kwa sasa anaratibu shindano la MALIKIA wa TWANGA PEPETA maarufu kama KIMWANA WA MANYWELE ametangaza neema wa washiriki wa shindano hili akisema mshindi wanataka wamfanye mjasiriamali, na hapa watakuwa wameondoa tatizo la ajira.

Mama ASHA BARAKA ambaye pia ni Mkurungezi wa AFICANS STARS ENTERTAINMENT ameyasema haya alipokuwa akiwatambulisha washindanaji KUMI wa shindano hili la MALIKIA wa TWANGA PEPETA.

Mshindi wa shindano hili la MALIKIA wa TWANGA atapata zawadi ya Duka la kuunza bidhaa mbalimbali za masuala ya UREMBO, na duka lenyewe lina thamani ya shilingi MILIONI TANO.

Mshindi wa pili atapata shilingi LAKI TANO, mshindi wa tatu atapata shilingi LAKI TATU na washiriki wengine watapata kifuta cha shilingi LAKI MOJA kila moja.

= = =

Katika habari za kimataifa kama ulifuatilia kwa uzuri michuano ya WIMBLEDON tenesi ni kwamba kina dada ndugu MOJA, THE WILLIAMS SISTERS, VENUS na SERANA wameondolewa.

Sasa waliowaondoa nao wamepata wababe wao, wote wamefurushwa kwenye WIMBLEDON tenesi.

Mchezaji asiyekuwa amejulikana kama anheweza kusababisha matatizo makubwa kwenye michuano hii MJERUMANI SABINE LISICKI amemuondosha MARION BARTOLI wa UFARANSA.

SABINE amemundosha BARTOLI kwa seti 6-4 6-7 na 6-1.

Kumbuka BARTOLI ndiye aliyemuondosha SERANA WILLIAMS katika robo fainali.

Mwanadada huyu SABINE anasema kwa KIINGEREZA I'm SPEECHLESS, SINA hata cha kuongea kwa furaha niliyonayo.

= =

Kwenye mchezo mwingine TSVETANA PIRONKOVA aliyemuondosha VENUS WILLIAMS naye ameondoshwa na PETRA KVITOVA.

KVITOVA anafika nusu fainali yake ya pili kwenye michuano ya WIMBLEDON kwa kumchapa PIRONKOVA kwa seti 6-3 6-7 na 6-2.

KVITOVA mwishoni akasema nina furaha nimefika nusu fainali kwasababu kabla ya mechi nilikuwa na hofu sana.

= = =

Sasa nakuletea mama wa milio katika court za WIMBLEDON.

Huyu ni MARIA SHARAPOVA,mrembo na mwanamitindo wa URUSI aliyevuma sana mwaka 2000 mpaka 2006.

Sasa amerudi tena.

Amemchapa DOMINIKA CIBULKOVA kwa seti za moja kwa moja za 6-1 6-1 na sasa atakutana na SABINE LISICKI kwenye mechi ya nusu fainali.

CIBULKOVA alimuondosha mchezaji nambari moja kwa ubora duniani CAROLINE WOZNIACKI, lakini hapa kwa SHARAPOVA wala hakufurukuta.

Kwa hali inavyokwenda akiendelea hivi SHARAPOVA huenda akatwaa GRAND SLAM hii, na kwa kweli ndiye anayepewa nafasi kubwa.

= = =

Na mwisho ni VICTORIA AZARENKA ambaye naye amesonga mbele kwenye hatua ya nusu fainali.

AZARENKA amemchapa TAMIRA PASZEK kwa seti 6-3 6-1.

Huyu naye ni moja ya wachezaji ambao wanapewa nafasi ya kufanya vizuri.

AZARENKA atacheza nusu fainali na PETRA KVITOVA.

= = =

Na sasa ni kandanda ambapo wachezaji TISA wa timu ya taifa ya MEXICO,wametimuliwa kwenye kambi ya timu ya taifa inayojiandaa na michuano ya COPA AMERIKA.

Wachezaji hawa si tu kwamba wametimuliwa, lakini pia wamelimwa tozo(faini)na wamefungiwa miezi SITA katika timu ya taifa.

Sababu ya adhabu hii ni utovu wa nidhamu walipokuwa kambini.

Wao waliona ni halali kuingiza wasichana ambao ni madada poa, ama kwa majina ya kisasa TAKE AWAY,kwenye vyumba vyao kinyume na taratibu.

Wale wasichana kwa vile walikuwa kibiashara zaidi wakawaibia vito vya dhamani wachezaji hawa wa MEKIKO, na fedha pia wakakomba.

Shirikisho la soka ya MEKIKO likaamua liwaarudishe nyumbani haraka sana ili wafaidi hicho wanachokitaka.

Sasa cha ajabu kuna habari hata bwana mdogo wa MAN.UNITED CHICHARITO naye yumo kwenye mkumbo, hizi ni tetesi,tutazifuatilia tuwajuze jamani,lakini kama itakuwa ni kweli, bado RYAN GIGGS wa MAN.UNITED ambaye kwa sasa yuko kwa wataalamu wakumtibu tabia ya kupenda ngono sanaaaa!

Aibu kweli MEKIKO.

==

Kombe la dunia la FIFA kwa wanawake, linaendelea UJERUMANI.

Na timu nyota duniani kwa soka la wanawake MAREKANI jana wameshuka dimbani wakicheza na KOREA ya KASKAZINI.

Ilikuwa kazi kweli hapa kwasababu WAKOREA ni wabishi kweli.

MAREKAN walisoteswa mpaka dakika ya 54 ndipo walipopata goli la kuongoza kwa kichwa kilichopigwa kwa ustadi wa hali ya juu.

Kwenye dakika ya SABINI MAREKANI wakafunga goli la pili na wakatoka kifua mbele kwa magoli hayo MAWILI kwa BILA.

= =

SWEDEN nao walikuwa dimbani wakicheza na COLOMBIA.

Kwa kweli SWEDEN wanaonekana wamepikwa kwelikweli safari hii.

Lakini na wao walitolewa jasho na COLOMBIA.

Baada ya kusumbuka sana walifanikiwa kupata goli MOJA tu.

Kwa hiyo sasa katika kundi Che,MAREKANI wanaongoza wakiwa na pointi TATU na magoli MAWILI, SWEDEN wao wana pointi TATU na GOLI MOJA.

= =

Katika masumbwi bila shaka jumamosi hii kuna pambano la kufa mtu ulingoni kati VLADIMIR KLITSCHKO na DAVID HAYE,pambano la uzito wa juu la WBA.

Hapa patachimbika ama mtu atapigwa kirahisi sana.

Lakini sasa mwezi wa TISA mwaka huu mzee wa mapesa asiyepigika, FLOYD MAYWEATHER JUNIR atazichapa na

Alipokutana na wanahabari kwa mara ya kwanza FLOYD akaulizwa mbona una mkwepa MANNY PACQUIO?

Akawajibu uzuri.

Kwa kifupi tu FLOYD anasema hamwogopi MAN PACQUIO wala nani,yuko tayari ili mradi sharti lake la kutolewa damu apimwe kuhusu dawa za kuongeza nguvu kwanza.

= =

Unajua TUSKER PROJECT FAME imerejea na Tanzania tuna wawakilishi wawili, HEMED na MSECHU.

Hili ni shindano linalowakutanisha wale nyota wa miaka miwili iliyopita.

MSECHU aliyaaga mashindano haya mwaka jana kwa kilio kwa JULIANA, moja ya majaji wa shindano hili.

Sasa MSECHU amerudi tena na wimbo wa kwanza alioimba jumapili iliyopita bado anamuota JULIANA.

Kifaa kipya cha Man United


The Spanish goalkeeper is all set to complete a switch from Atletico Madrid, with the Red Devils in the market for a successor to the recently retired Edwin van der Sar.

1990: Born in Madrid on November 7.

2007: Helps Spain to victory in the 2007 Under-17 European Championship, and then to a runners-up spot in the Under-17 World Cup.

2008: Spends his first professional season with the Atletico Madrid reserves, in the Segunda Division B.

2009: September - De Gea makes his senior Atletico debut as a substitute in the Champions League against Porto, coming on for the injured Roberto.

October: Starts his first Primera Division match at home to Real Zaragoza. In the first 20 minutes he gives away a penalty but then saves the spot-kick.

2010: Towards the end of the 2009-10 season he becomes the first-choice goalkeeper under new coach Quique Sanchez Flores, twice earning man-of-the-match awards towards the end of the season.

May - Plays in the Europa League final victory over Fulham in Hamburg. Named in Vicente Del Bosque's 30-man provisional World Cup squad but does not make the final squad.

August - Helps Atletico win the European Super Cup in a 2-0 victory over Inter Milan, saving a penalty during the game.

2011: May - Ends the season as an ever-present in La Liga for Atletico. Manchester United manager Sir Alex Ferguson claims that the clubs are close to completing a deal to sign De Gea, though De Gea denies the claims. Included in Spain's 23-man under-21 squad for the European Championship in Denmark.


Monday, June 27, 2011

Serikali kurekebisha sera ya michezo

Serikali kurekebisha sera ya michezo

Wizara ya habari utamaduni vijana na michezo imekamilisha rasmu ya marekebisho ya sera ya maendeleo ya michezo nchini ambayo itatoa mwelekeo wa maendeleo ya michezo nchini.

Akijibu swali Bungeni mjini DODOMA hii Leo Naibu Waziri Wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo DKT FENELLA MKANGARA amesema serikali inaandaa mkakati maalumu wa uendeshaji wa michezo kuanzia ngazi za vijini ambao utashirikisha watoto,vijana na wazee.

DKT MKANGARA amasema Tanzania imekuwa ikifanya vyema katika mashindano mbalimbali ya kiamataifa hasa katika mchezo wa soka pamoja na sekta ya michezo kukubwa na matatizo mbalimbali ikiwepo ufinyu wa banjeti ya serikali katika kuendesha michezo nchini.

===

Michuano ya KAGAME kuendelea leo DSM

Michuano ya kuwania kombe la KAGAME hatua ya makundi inaendelea leo kwa michezo miwili ya kundi A kuchezwa katika uwamja wa taifa jijini DSM.

Mchezo wa kwanza utazikutanisha RED SEA ya ERETRIA dhidi ya ZANZIBAR OCEAN VIEW ambayo inaongoza katika kundi la A ikiwa na Alama Tatu ilizojikusanyia baada ya kushinda katika mchezo wa kwanza ilipoifunga ETINCELLES ya RWANDA mabao MATATU kwa MAWILI katika mchezo wa ufunguzi.

Mchezo mwingine unazikutanisha mabingwa wa Burundi Vital O’ ambayo itateremka dimbani dhidi ya ETINCELLES ya RWANDA, Vital O’ ina ALAMA MOJA hadi hivi sasa baada ya kutoka sare ya bila ya kufungana na SIMBA katika mchezo wa ufunguzi wa kundi la A mchezo ulipingwa juzi kwenye uwanja wa Taifa.

Katika michezo iliyochezwa jana mechi za kundi la B, YANGA iligawana ALAMA na EL- Mereikh ya SUDAN baada ya kufunga mabao MAWILI kwa MAWILI wakati katika kundi la C mabingwa watetezi timu ya APR ya RWANDA imeanza vyema kutetea ubingwa wake baada ya kuichapa PORTS ya JIBUTI kwa mabao MANNE kwa BILA.

===

Mwanamuziki wa Jamaica akonga nyoyo za mashabiki DSM

Mwanamuziki nyota wa Jamaica -ELEPHANT MAN usiku wa kuamkia leo alikonga nyoyo za wapenzi wa burudani hapa nchini pale alipoongoza wanamuziki kutoka Jamaica , Kenya na Tanzania kutumbuiza katika tamasha la ufukweni la STRAIGHT MUSIC BEACH PARTY 2011 lililofanyika katika klabu ya MBALAMWEZI.(UPSOUND)

Wasanii kutoka nchi za Kenya na Tanzania kama vile Fid Q, Cpwa, Red San na P-Unit nao wakatumbuiza (UPSOUND)

==

Ecuador yaichapa Burkinabe kombe la dunia la vijana

Timu ya taifa ya ECUADOR imetinga katika hatua ya KUMI NA SITA BORA ya fainali ya kombe la FIFA la dunia kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 baada ya kuifunga mabingwa wa Afika BURKINA FASO kwa mabao MAWILI kwa BILA nchini MEXICO.

Katika mchezo mwingine wa kundi la E mabingwa watetezi wa fainali ya kombe la dunia kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 timu ya taifa ya UJERUMANI nayo imetinga katika hatua hiyo ya KUMI NA SITA BORA baada ya kuitandika PANAMA mabao MAWILI kwa BILA.

Matokeo mengine yanaonyesha timu ya taifa ya MAREKANI imelazimishwa sare ya bila kufungana na New Zealand na sasa itakutana na UJERUMANI katika hatua ya mtoano ya KUMI NA SITA BORA’

Katika mchezo mwingine, UZBEKISTAN imeibuka kidedea baada ya kuifunga JAMUHURI ya CZECH mabao MAWILI kwa MOJA.

LEO kutakuwa na mchezo mwingine wakati AUSTRALIA itavaa na DENMARK.

=====

Ujerumani Yaanza Vyema Kombe La Dunia Kwa Wanawake

Timu ya taifa ya wanawaka ya UJERUMANI imaanza vizuri fainali za kombe la dunia kwa wanawake baada ya kuichapa CANADA kwa mabao MAWILI kwa MOJA katika mchezo wa ufunguzi ulichezwa jana kwenye uwanja wa OLYMPIC nchini UJERUMANI.

Katika mchezo mwingine mabingwa wa Afrika timu ya taifa ya NIGERIA imeambulia kichapo baada ya kufungwa Bao moja kwa bila na UFARANSA.

Ratiba ya michuano hiyo inaonyesha hii leo JAPAN itamenyana na NEW ZEALAND katika mchezo wa kwanza wakati MEXICO itakutana na ENGLAND katika mchezo wa pili.

Kesho kutakuwa na michezo mingine miwili wakati COLOMBIA itakapocheza na SWEDEN, MAREKANI itacheza na KOREA KUSINI huku NORWAY ikipepetana na wawakilishi wengine wa Afrika GUINEA YA ikweta.

===

River Plate ya ARGETINA imeteremka DARAJA

Mabingwa mara 33 wa ligi kuu ya ARGETINA timu ya RIVER PLATE imeshuka daraja baada ya kudumu katika ligi kwa miaka 110.

Ilikuwa ni kilio kwa mashabiki wa RIVER PLATE baada ya FILIBI ya mwisho kupulizwa katika uwanja wa MONUMENTAL jana huku ubao wa magoli ukisomeka RIVER PLATE MOJA na BELGRANO

Mashabiki walishindwa kuvumilia na kuanza kurusha vyuma na mawe kwa wezao na kusababisha watu 25 kujeruhiwa wakiwepo askari SITA wa vikosi vya usalama.

Katika mchezo wa kwanza RIVER PLATE ilichapwa mabao MAWILI kwa BILA na BELGRANO na hivyo kushushwa daraja kwa jumla ya MABAO MATATU kwa MOJA.

RIVER PLATE sasa itacheza katika ligi ya NACIONAL B msimu ujao.

===

KAGAME - CASTLE CUP 2011

KAGAME - CASTLE CUP 2011

25th June TO 10th July 2011, Tanzania

Team Fixture list

GROUP A SIMBA(TZ), VITAL O’(BUR), ETINCELLES (RWA), OCEAN VIEW (ZNZ), RED SEA (ETR)

GROUP B YANGA(TZ), EL MEREIKH (SN),BUNAMWAYA (UG), ELMAN F.C. (SM)

GROUP C APR (RWA), ST. GEORGE (ETH), ULINZI (KN), PORTS (DBT),

(CLASSIFICATION: GROUP A 1st 2nd & 3rd GROUP B, 1st and 2nd GROUP C 1st & 2nd PLUS BEST QUALIFIERS FROM B AND C QUALIFY TO QUARTER FINALS).

DATE

NO

TEAMS

GROUP

VENUE

TIME (EAT)

Sat 25th June

1

Etincelles Vs Ocean View

A

Dar

2 pm

2

Simba SC Vs Vital O’

A

Dar

4 pm

Sun 26th June

3

APR Vs Port

C

Moro

4 pm

4

Yanga Vs Mereikh

B

Dar

4 pm

Mon 27th June

5

Red Sea Vs Ocean View

A

Dar

2 pm

6

Vital O’ Vs Etincelles

A

Dar

4 pm

Tue 28th June

7

Bunamwaya Vs Elman

B

Dar

4 pm

8

St. George Vs Ulinzi

C

Moro

4 pm

Wed 29th June

9

Red Sea Vs Etincelles

A

Dar

2 pm

10

Ocean View Vs Simba

A

Dar

4 pm

Thur 30th June

11

Bunamwaya Vs Mereikh

B

Dar

2 pm

12

Elman Vs Yanga

B

Dar

4 pm

13

Ulinzi Vs Ports

C

Moro

2 pm

14

St. George Vs APR

C

Moro

4 pm

Fri 1st July

15

Red Sea Vs Vial O’

A

Dar

2 pm

16

Etincelles Vs Simba

A

Dar

4 pm

Sat 2nd July

17

Elman Vs El Mereikh

B

Dar

2 pm

18

Yanga Vs Bunamwaya

B

Dar

4 pm

19

St. George Vs Ports

C

Moro

2 pm

20

Ulinzi Vs APR

C

Moro

4 pm

Sun 3rd July

21

Ocean View Vs Vital O’

A

Dar

2 pm

22

Simba Vs Red Sea

A

Dar

4 pm

Mon 4th July

REST DAY

QUARTER FINALS

Tue 5th July

23

C2 Vs B2

(LIVE)

Dar

24

A1 Vs Best Qualifier

(Live)

Dar

Wed 6th July

25

C1 Vs A3

(LIVE)

Dar

26

B1 Vs A2

(LIVE)

Dar

SEMI FINALS

Thur 7th July

27

Winner 23 Vs Winner 24

(LIVE)

Dar

Fri 8th July

28

Winner 25 Vs Winner 26

(LIVE)

Dar

Sat 9th July

REST DAY

Sun 10th July

29

Loser 27 Vs Loser 28

(LIVE)

Dar

30

Winner 27 Vs Winner 28

(LIVE)

Dar