Klabu ya SIMBA yawasili jijini TANGA.
KATIKA hatua nyingine mabingwa
wa soka nchini SIMBA ya DSM imewasili mjini TANGA tayari kwa mchezo wao wa ligi
kuu soka Tanzania bara dhidi ya wenyeji wa COSTAL UNION mchezo utakaochezwa
katika uwanja wa MKWAKWANI mjini humo siku ya jumamosi.
Msemaji wa klabu ya SIMBA,
EZEKIEL KAMWAGA amewataka mashabiki wa klabu hiyo kutojiingiza katika vitendo
vitakavyosababisha klabu hiyo kutozwa faini.
Kiungo wa simba RAMADHANI
CHOMBO REDONDO hakuondoka na kikosi cha SIMBA kwenda TANGA kwa kuwa anasubuliwa
na MALARIA,lakini akaeleza kurejea kwa mshambuliaji wa timu hiyo MRISHO NGASSA ambaye
atacheza katika mchezo huo.
Michezo mingine itakayochezwa
jumamosi ni katika uwanja wa JAMHURI mjini MOROGORO ambapo POLISI MORO itacheza
na AZAM FC, TANZANIA PRISONS itacheza na JKT OLJORO.
Michezo mingine RUVU
SHOOTING itacheza na AFRICA LYON na MTIBWA SUGAR itacheza na MGAMBO JKT.
====
Wagombea
sita soka la wanawake wapingwa
WAGOMBEA sita wa nafasi mbalimbali za uongozi
katika Chama cha Mpira wa Miguu wa Wanawake Tanzania (TWFA) wamewekewa
pingamizi na wadau wa mchezo huo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TWFA, Ombeni
Zavala, wagombea hao ni JOAN MINJA anayewania nafasi ya Mwenyekiti ambaye
amewekwa pingamizi na wadau sita. Pia ISABELLAH KAPERA ambaye anagombea
uenyekiti amewekewa pingamizi moja.
Wagombea watatu wa nafasi ya Mjumbe wa Mkutano
Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) nao wamewekewa pingamizi.
Wagombea hao ni JULLIET MNDEME ana pingamizi
sita , Zena Chande ana pingamizi NNE na Jasmin Soud mwenye pingamizi tatu.
Naye Rahim Maguza anayewania ujumbe wa Kamati ya
Utendaji amewekewa pingamizi moja.
Licha ya pingamizi hizo, wagombea wote
wanatakiwa kuhudhuria usaili wakiwa na vyeti vyao halisi vya kitaaluma
utakaofanyika Oktoba 12, 13 na 14 mwaka huu kwenye ofisi za TFF zilizopo Uwanja
wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam kuanzia saa 3 asubuhi.
===