Tuesday, September 28, 2010

Big Brother Africa



It’s day 69 on M-Net’s Big Brother All Stars --- and Big Brother is having and engagement party for Meryl and Mwisho. The party was attended by Meryl's aunt and uncle as well as Mwisho's brother

Marefa

Hao ndio marefa baada ya mafunzo ya FIFA yaliyofanyika kabla ya Ligi kuu Tanzania Bara kuanza, lakini baadhi yao wameaza kuboronga na kufungiwa na kamati ya mashindano ya TFF

Makocha kazini



Makocha Charles Mkwasa na Adolf Rishad wakiwanoa wachezaji wa Twiga Stars katika viwanja vya Karume jijini DSM hii leo

Twiga Stars



Twiga Stars mazoezini wakijiandaa na michuano ya kombe la mataifa ya Afrika yatakayofanyika Afrika kusini mwezi ujao

GYM ya TFF ipo kazini

Wachezaji wa TSA wakifanya mazoezi katika gym ya TFF

AMERIKANI FOOTBALL TANZANIA



Tanzania kwa mara ya kwanza itakuwa mwenyeji wa mchezo wa kirafiki wa kimataifa wa AMERICAN FOOTBALL kati ya DRAKE UNIVERSITY ya MAREKANI dhidi ya CANADEIP ALL STARS ya MEXICO mchezo utakochezwa mjini MOSHI MAI 21 mwakani.
Akizungumza na TBC jijini DSM mratibu wa mchezo huo mwenyekiti wa GLOBALL FOOTBALL PATRICK STEENBERGE kutoka MAREKANI amesema lego la mchezo huo ni kueneza mchezo huo hapa nchini pamoja na kujifunza tamaduni mbalimbali za kitanzania.
Kwa upande wake kaimu Afisa masoko Mkuu wa bodi ya utalii Tanzania DEVOTE MDACHI amesema mchezo huo utasasaidi kuutangaza utalii wa Tanzania kimataifa.
Wachezji wa timu hizo mbili za DRAKE UNIVERSITY ya MAREKANI na CANADEIP ALL STARS licha ya mchezo huo pia wataendesha kliniki za mcezo huo kwa watoto wa shule za sekondari na msingi mkoani Kilimanjaro kabla ya kupanda mlima kilimanjaro

Miss Tanzania



Miss Tanzania 2010 GENEVIEVA EMMANUEL ameonyesha matumaini kwamba atafanye vema katika mashindano ya kumtafuta mrembo wa dunia MISS WOLRL ambayo yanatarajiwa kufanyika mjini SANYA nchini china OCTOBA 31 mwaka huu.
GENEVIEVA amesema maadalizi aliyofanya ya kujenga kujiamini,kujieleza na maadalizi ya mwisho mwisho atakayofanya atakapo wasili nchini china yatamsaidia kupata ushindi katika mashindano hayo lakini akakiri kwamba kutakuwa na ushindani mkubwa
Mwenyekiti wa kamati ya miss Tanzania HASHIM LUDENGA amesema Tanzania imefika katika hatua zuri katika jukwaa la urembo kimataifa ingawa wamekuwa hawapati taji la DUNIA kutokana na wasichana wengi kukosa kujiamini.
Miss Tanzania 2010 GENEVIEVA EMMANUEL anaagwa kesho jijini dsm na ataondoka kwenda CHINA keshokutwa siku ya ALHAMIS tayari kwa kinyanganyiro hicho kitakachofanyika CHINA, OCTOBA 31

TFF yaonyesha makali yake

Rungu la kamati ya mashindano ya shirikisho la soka nchini TFF limewashukia waamuzi wanne wa ligi kuu Tanzania bara baada ya kuwafungia kwa kipindi cha miezi sita kuchezesha michezo ya ligi hiyo baada ya kushindwa kutafsiri sheria 17 za soka katika michezo kazaa iliyopita.
Akizungumza na waadishi habari jijini DSM hii leo Afisa habari wa TFF, FOLRIAN KAIJAGE, aliwataja wamuzi walifungiwa kuwa ni METHEW AKRAMA na FRANK KOMBA waliochezesha mchezo kati ya mabingwa watetezi Simba dhidi ya AZAM FC mchezo ulichezwa kwenye uwanja wa mkwakwani mkoani Tanga septemba 11 na Simba kuibuka kidedea kwa ushindi wa mabao mawili kwa moja
KAIJAGE pia akawataja wamuzi wengine waliofungiwa na kamati hiyo kuwa ni RONALD SWAI na Msaidizi wake SAMUEL PENZU waliochezesha mchezo kati ya YANGA na KAGERA SUKARI kwenye uwanja wa JAMHURI MKOANI MOROGORO na wamuzi hao kushindwa kutafrisi kwa usahihi sheria za soka na kuasababisha YANGA kufunga bao la kwanza,katika mchezo huo YANGA ilipata ushindi wa mabao MAWILI kwa BILA
KAIJAGE akayataja maamuzi mengie ambayo yamefikiwa na kamati ya mashindano kuwa ni kuipiga faini klabu ya majimaji ya Songea ya shilingi LAKI TATU kwa kile alichoeleza kuwa majimaji ilichelewa kuingia uwanjani kwa dakika 15 na kusababisha mchezo huo kati yake na AFRICAN LYON kuchelewa kuanza,Majimaji wamedaiwa kuchelewa kuingia uwanjani kutokana na imani za kishirikiana katika mchezo ulipigwa kwenye uwanja wa majimaji SEPTEMBA 28.KAIJAGE amesema kamisaa wa mchezo kati ya YANGA na KAGERA SUKARI yeye amefungiwa kwa mwaka mmoja kwa kushindwa kuandika taarifa sasahihi za mchezo huo

Monday, September 27, 2010

Michezo leo

Yanga emeengelea kujikita kileleni mwa ligi kuu ya Tanzania bara baada ya hiyo jana kuibuka na ushinda wa mabao MAWILI kwa BILA dhidi ya RUVU SHOOTING STARS mchezo uliochezwa katika uwanja wa JAMHURI mkoani morogoro.

Kwa matokeo hayo YANGA imefikisha Alama 16 baada ya kushuka dimbani mara SITA ikifuatiwa na mabingwa watetezi SIMBA yenye Alama 12 baada ya kucheza michezo MITANO huku JKT RUVU ikishika nafasi ya tatu ikiwa na Alama 10.

Timu zilizopanda daraja msimu huu bado hazijafanya vyema na zinaendelea kushikilia nafasi za mwisho katika msimamo wa ligi kuu Tanzania bara, RUVU SHOOTING inashika nafasi ya 11 ikiwa na Alama 3 baada ya kushuka dimbani mara TANO wakati AFC ARUSHA inaendelea kushikilia mkia ikiwa na haina hata Alama yeyote baada ya kushuka dimbani mara nne na kupoteza michezo yote.

Ligi hiyo inaendelea jumatano ya wiki hii wakati mabingwa watetezi SIMBA watakuwa wageni wa MTIBWA SUKARI kwenye dimba la JAMHURI mjini morogoro,Azam fc watakuwa wenyeji wa JKT RUVU katika dimba la mkwakwani mkoani Tanga.

=== ==

MICHAEL OWEN alifunga goli lake la 200 katika ligi kuu ya ENGALAND na kuisaidia MANCHESTER UNITED kutoka sare ya kufungana mabao MAWILI kwa MAWILI na BOLTON ugenini katika mchezo uliochezwa kwenye uwanja REEBOK hiyo jana.

Kocha wa MANCHESTER UNITED SIR ALEX FERGUSON amesema ni vizuri kufunga mabao lakini haifurahishi kuona timu inashindwa kuondoka na Alama zote tatu.

Alipoulizwa juu ya timu yake kushindwa kuyatumia matokeo ya jumamosi ya kufungwa kwa wapinzani wao katika kufukuzia ubigwa ARSENALna CHELSE, FERGUSON amesema timu hupoteza Alama wakati hukutegemea matokeo yagekuwa hivyo.

Kwa sare hiyo Manchester imechupa hadi nafasi ya pili katika msimamo wa ligi ya ENGLAND ikiwa na Alama 12 huku ARSENAL wakiendelea kushika nafasi ya pili ikiwa na Alama 11 baada ya juzi kuchapwa kwa mabao tatu kwa mawili na WEST BROM, kuku mabingwa watetezi CHELSEA wakibaki kileleni mwa ligi hiyo ikiwa na ALAMA 15 igawa ilichapwa bao moja kwa bila ma MANCHESTER CITY mwishoni mwa wiki.

Kocha mpya wa ASTON VILLA GERARD HOULLIER akiwa kwenye benchi la timu hiyo kwa mara ya kwanza aliingoza VILLA kuibuka na ushindi wa mabao MAWILI kwa Moja dhidi ya BLACKBURN ROVERS.

Matokeo mengine yakushangazwa hiyo jana yameshuhudia NEW CASTLE wakichapwa nyumbani katika uwanja wa ST JAMES PARK kwa mabo mawili kwa moja na STOKE CITY.

=== ==

Ligi kuu ya Hispania maarufu kama LALIGA iliendelea mwsihoni mwa wiki huku BARCELONA wakibuka kidea kwa ushi wa mabo matutu kwa moja dhidi ya ATHLETIC BILIBAO.

VALENCIA nayo ikaibuka na ushindi wa mabao mwawili kwa bila dhidi ya Sporting gijon,SEVILLA ikachapwa mabao 2 kwa bila na HERCULES huku DEPOTTIVO LA CORUNA ikiifungwa na ALMERIA kwa mabao 2-0.

Real Madrid wakabanwa bavu na LAVENTE na kutoka suluhu,real sociedad ikafungwa na MALLORCA kwa maabao mawili kwa sifuri,matokeo mengine ESPAANYOL ikapata ushindi wa goli moja kwa bila dhidi ya Osasuna.

Msimamo wa ligi unaonyesha,VALENCIA wanaogoza ligi hiyo wakiwa na Alama 13 na inafuatiwa na mabingwa watetezi BARCELONA wakiwa na Alama 12 real Madrid wanashika nafasi ya tatu wakiwa na Alama 11

== ==

Mkenya PATRICK MAKAU ashinda BERLIN MARATHON

Mkenya PATRICK MAKAU ashinda BERLIN MARATHON ameshinda mashindano ya marathon ya Berlin lakini akashindwa kuvunja rekondi ya mwiethiopia GEBERSELASSLES aliyoweka mwaka 2008.

Makau amemaliza mbio hizo kwa muda wa dakika moja zaidi ya rekondi inayoshikiliwa na GEBERSELASSLES kwani alitumia muda wa saa mbili,dakika TANO na sekunde 8 huku MKENYA mwezake GEOFFREY MUTAI akimaliza katika nafasi ya pili kwa sekunde mbili nyuma ya MAKAU.

Nafasi ya tatu ilinyakuliwa na mwiethiopia BAZU WORK baada ya kutumia muda wa saa mbili,dakika tano na sekunde 25.

Kwa upande wa wanawake ABERU KEBEDE wa ETHIOPIA amemaliza wa kwanza mbele ya BEZUNESH BEKELE kwa muda wa masaa 2 na dakika 23 na sekunde 58.

== ===

Katika mbio za magari mwendesha magari wa timu ya FERRARI FERNANDO ALONSO ameibuka kideda baada ya kushinga mashindano ya SINGAPORE GRAND PRIX hiyo jana na kuufanya ubingwa wa dunia uwe wazi na unaweza kunyakuliwa na dereva yeyote.

SEBASTIAN vettel akamaliza katika nafasi ya pili nafasi ya tatu ikamyakuliwa na dereva wa timu ya RED BULL MARK WEBBER,nafasi ya nne ikanyakuliwa na JENSON BUTTON.

Lewis Hamilton wa timu ya MACLAREN alishindwa kumaliza mbio hizo kwa mara ya pili mfululuzo baada ya hiyo jana kukwaruzana na WEBBER katika mzunguko wa 36.

Msimamo wa mbio hizo unaonyesha MARK WEBBER anongoza Madera wezake akiwa na Alama 202,huku ALONSO akiwa wa pili na Alama 191,LEWIS HAMILTON yeye NASHIKA nafasi ya tatu akiwa na Alama 182 huku VETTEL akiwa katika nafasi ya nne na Alamaa 177.

Madereva hao watachuana katika mashindano manne yaliyobaki ya GRAND PRIX ili kumpata bingwa WA DUNIA ambayo ni JAPAN,KOREA ya KUSINI,BRAZIL na fainali itakuwa ABU DHABI.

====

squish akina mama

squish dar yarindima


BRUCE CHIKABUKA ameibuka kidedea katika mashindano ya ya BELL SQUISH ambayo yamefika tamati hiyo jana katika viwanja vya GYHKHANA jijin DSM baada ya kumfunga ALLY REMTULLA kwa Alama 27 kwa 16.

Kwa upande wa akina dada, VICKY CHUWA emanyakua ubingwa baada ya kumchapa mpinzania wake SARAH EMERSON kwa Alama 32 kwa 10

Nahodha wa KLABU ya GYHKHANA MARWA BUSIGARA amesema igawa mashindano ya mwezi huo yamekua na ushindani mkubwa lakini amesikitishwa na uchache wa ushiriki wa akina DADA

Kwa upande wao wadhamini wa mashindano hayo kampuni ya DEAUTO GROUP kupitia kwa SIBTAIN REMTULLA wamesema Tanzania ina wachezaji wengi wenye vipaji vya kucheza Squish lakini wanakosa kuendelezwa ili wacheze katika kiwango cha kimataifa.

Zaidi ya wachezaji AROBAINI wameshiriki katika mashindano hayo kutoka katika mikoa ya ARUSHA, TANGA,DSM na ZANZIBAR

Kuongelea madola


Wachezaji wa kuongelea wakiwa uwanja wa ndege wa mwl Nyerere kabla ya kukwea pipa kwenda india kushiriki mashindano ya juimuiya ya madola

eid el fitry


Waumini wa dini ya kislam wakitoka katika mskiti wa kichangani magomeni jijini dsm baada ya swala ya EID EL FIRTY

Wednesday, September 22, 2010

MDSSS

Stand up 2010 start off point for procession at Dagoretti Nairobi KenyaIn procession children holding posters on MDGSStand up 2010 procession in Dagoretti NairobiMaking Noise for the MDGs
Stand up walk on 17th September 2010Stand up walk on 17th September 2010District Administrator Dagoretti giving a speechPersons with disabilities representatives handing over the petition to the District Administration Dagoretti – looking on is ABC Executive Director Mr MainaDistrict Administrators planting commemorative trees at DCs compound

Tuesday, September 21, 2010

Vijana waliochanguliwa kwenda Marekani


Hao ndio vijana watatu wakiwa na Smith mchezaji nyota wa NBA vijana hao wanaunda timu ya Afrika

Timu ya taifa ya meza


Timu ya taifa ya mpira wa Meza kabla ya kucheza mchezo wa kirafiki na Zambia mwishoni mwa wiki,Tanzania ilichapa Zambia

Mashindano ya gofu

Project fame

Wanamziki chipukizi wakijiandikisha kabla ya kushiriki katika shindano la Project fame wiki iliyopita

Project fame yaanza


Mshiriki wa project fame akijingamba kabla ya kinyang'anyiro

BMT wapewa gari


Hatimaye neema katika sekta ya michezo imeenza kujidhihirisha hapa nchini baada ya leo hii shirika la UK SPORT kwa kushirikiana na Tanzania kuzindua kituo cha nne maalumu cha kimataifa cha uongozi wa michezo kwa vijana.

Uzinduzi huo umehudhuriwa na naibu waziri wa habari, utamaduni na michezo JOEL BENDERA ambaye ametoa wito wa kutumia furasa hiyo kwa maendeleao ya michezo nchini.

Waweza kuona ni suluhisho la tatizo kubwa la michezo hapa nchini na hii yawezekana endapo tu makusudi na malengo ya kituo hiki yakifanyiwa kazi ipasavyo.

Michezo ni muhimu sana katika maendeleo ya taifa lakini kwa Tanzania hali hiyo bado haijaonekana dhahiri shahir kutokana na kukosa msingi imara wa kukuza wanamichezo chipukizi kwa ajili ya ujenzi wa timu za taifa za michezo mbalimbali za siku za usoni.

Naibu waziri wa habari utamaduni na michezo, JOEL BENDERA amekiri kufa kwa michezo hapa nchini hasa ngazi za chini vijijini , ilayani hadi mikoani hali inayomfanya sasa avae kibwebwe kwa kuwataka viongozi wa maeneo hayo kuwa watendaji na si wasemaji tu.


Awali NICK DIMKY mwakilisi wa michezo wa shirika la UK SPORT, ameitaka Tanzania kutumia vema fursa hii ili kupata walimu vijana watakaojenga misingi imara ya michezo na hatimaye jina la Tanzania kujulikana katika ulimwengu wa michezo

Hiki ni kituo cha nne kwa Tanzania, miongoni mwa vituo vya Arusha, Songea na Malya na kinasimamiwa na Baraza la Michezo nchini BMT na UK SPORT wametoa msaada wa gari jipya aina ya Toyota kwa ajili ya kurahishisha shughuli za utendaji wake.


MBIO ZA MAGARI


Tamasha kubwa la magari maarufu kama TANZANIA AUTOMOTIVE FESTIVAL linatarajia kufanyika OCTOBA 1-3 mwaka huu jijini DSM katika viwanja vya Posta.

Mratibu wa Tamasha hilo ALLY MTAAGA amesema hiyo inakuwa ni fursa ya kuhamasisha michezo ya mbio za magari inayokuwa kwa kasi hapa nchini na siku hiyo pia kutakuwa na michezo mbalimbali ya kuchezea magari na pikipiki .

Tamasha hilo linaloshirikisha wadau wa fani ya magari kutoka nchi mbalimbali Duniani, linadhaminiwa na makampuni ya SUPERDOL, SYNOVATE, AUDIO SENNSATION, INOCH na PETER GEORGE GARAGE pia litatoa fursa kwa watazamani kujionea aina mbalimmbali za magari ya kifahari , yale ya kale na yenye kasi kubwa yanayotumika katika mbio za magari za kimataifa.