Tuesday, May 10, 2011

Kareti mafunzoni

Wachezaji mia moja wa mchezo wa karete wapata mafunzo ya kimataifa

Zaidi ya wachezaji mia moja kutoka katika klabu za karete za jijini DSM wanahudhuria mafunzo ya siku mbili yayoendeshwa na mkufunzi wa shirikisho la karete dunia kutoka Japan MANABU MURAKAMI, mafunzo hayo yanafanyika katika uwanja wa ndani wa taifa jijini DSM.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo kocha wa Shotokan Karete Tanzania Phillipo Chikoko amesema mafunzo hayo yameadaliwa kwa ajili ya kunyanyua kiwangao cha mchezo huo nchini.

Chikoko amesema mafunzo hayo pia yatasaidia pia kupata timu ya taifa ambayo itashiriki katika mashindano ya dunia yatakayofanyika mwakani nchini AUSTRALIA.

No comments:

Post a Comment