CHEKA kuwania ubingwa wa DUNIA dhidi ya mjerumani.
BINGWA wa ngumi za kulipwa
nchini anayetambuliwa na shirikisho la ngumi la dunia (UBO) FRANCIS CHEKA
amesaini mkataba wa kucheza pambano la kuwania ubingwa unaotambuliwa na
shirikisho la ngumi la IBF uzito wa kati.
Katika pambano hilo CHEKA
ambaye hivi karibuni alimchakaza KARAMA NYILAWILA kwa KO na kupata ubingwa wa
UBO sasa atacheza na bondia kutoka nchini JERUMAN, BENARD SIMON katika pambano
litakalochezwa nchini UJERUMAN NOVEMBA 17 mwaka huu.
BONDIA, CHEKA anasaini
mkataba kwaajili ya kucheza pambano dhidi ya mjerumani BERNARD SIMON.
Pambano hilo limetafutwa
na promota mpya wa FRANCIS CHEKA, JUMA MABAKILA mwenyewe akisema anataka, kila
baada ya miezi miwili bondia CHEKA kupanda ulingoni.
Rais wa shirikisho la
ngumi, IBF AFRICA ONESMO NGOWI naye akazungumzia pambano jingine la OMAN ambalo
FRANCIS CHEKA atazichapa baada ya pambano na MJERUMAN
Tayari FRANCIS CHEKA
amejizolewa sifa nyingi katika masumbwi nchini baada ya kuwachapa mabondia
mashuhuri kama KARAMA NYILAWILA, MADA MAUGO na RASHID MATUMLA.
No comments:
Post a Comment