Wednesday, October 10, 2012



CHEKA kuwania ubingwa wa DUNIA dhidi ya mjerumani.
BINGWA wa ngumi za kulipwa nchini anayetambuliwa na shirikisho la ngumi la dunia (UBO) FRANCIS CHEKA amesaini mkataba wa kucheza pambano la kuwania ubingwa unaotambuliwa na shirikisho la ngumi la IBF uzito wa kati.
Katika pambano hilo CHEKA ambaye hivi karibuni alimchakaza KARAMA NYILAWILA kwa KO na kupata ubingwa wa UBO sasa atacheza na bondia kutoka nchini JERUMAN, BENARD SIMON katika pambano litakalochezwa nchini UJERUMAN NOVEMBA 17 mwaka huu.
BONDIA, CHEKA anasaini mkataba kwaajili ya kucheza pambano dhidi ya mjerumani BERNARD SIMON.
Pambano hilo limetafutwa na promota mpya wa FRANCIS CHEKA, JUMA MABAKILA mwenyewe akisema anataka, kila baada ya miezi miwili bondia CHEKA kupanda ulingoni.
Rais wa shirikisho la ngumi, IBF AFRICA ONESMO NGOWI naye akazungumzia pambano jingine la OMAN ambalo FRANCIS CHEKA atazichapa baada ya pambano na MJERUMAN
Tayari FRANCIS CHEKA amejizolewa sifa nyingi katika masumbwi nchini baada ya kuwachapa mabondia mashuhuri kama KARAMA NYILAWILA, MADA MAUGO na RASHID MATUMLA.

No comments:

Post a Comment