Monday, March 15, 2010

NGORONGORO HEROES KAZINI DHIDI YA MALAWI

Timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 20 tayari imeanza kambi ya mazoezi ya mwezi mmoja kabla ya kuivaa timu ya taifa ya Malawi.

mchezo wa kwanza utakuwa ugenini nchini MALAWI kati ya tarehe 17 na kumi na nane mwezi wa April,na mchezo wa marudiano utafanyika May jijini Dar es Salaam na kama itashinda itaivaa Ivory Coast na iwapo itavuzu itakuwa imekata tiketi ya kushiriki michuano ya vijana wenye umri chini ya miaka ishirini zitakazofanyika nchini Libya mwaka 2011

No comments:

Post a Comment