Wednesday, March 24, 2010

Stars na Ngorongoro Heroes kibaruani Afrika

Timu za taifa ile ya wakubwa Taifa Stars na timu ya taifa ya Vijana chini ya umri wa miaka 20 zinakibarua kingumu katika kutafuta tiketi ya kushiriki fainali za kombe la mataifa ya Afrika.

Taifa Stars yenyewe inashuka dimbani siku ya jumamosi kupepetana na Somalia kwenye uwanja wa Uhuru katika kutafuta tiketi ya kucheza katika fainali za Kombe la mataifa bingwa Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za nyumbani maarufu kama CHAN.

Wakatika kwa upande wa Ngorongoro Heroes wao wanajiandaa kumenyana na MALAWI April 17 ugenini katika kuwania kutafuta tiketi ya kucheza fainali za vijana wenye umri huo ambazo zitafanyika Libya mwakani

No comments:

Post a Comment