Tuesday, November 9, 2010

Kili stars hadharani


Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania Bara Kilimanjaro Stars JAN PAULSEN ametangaza kikosi cha wachezaji 22 wa timu hiyo tayari kujiandaa na mashindano ya CECAFA TUSTER CHALLENGE CUP na kusema TANZANIA kuwakilishwa na timu mbili za KILIMANAJARO STARS na ZANZIBAR HEROES katika mashindano hayo kuna hasara.

Akizungumza wakati wa kutangaza kikosi hicho jijini dsm hii leo kocha wa KILIMANAJARO STARS ambaye pia ni kocha mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania TAIFA STARS JAN PAULSEN ametaja baadhi ya hasara ni kuwakosa wachezaji mahiri aliokwisha waandaa wakati wakitumikia TAIFA STARS hali inayopunguza nafasi ya Tanzania kunyakua kombe la CHALENGE.

Hata hiyo PAULSEN amekiri kuwa mfumo huo wa kuwa na timu mbili katika mashindano ya CECAFA TUSTER CHALLENGE CUP kunatoa fursa ya kuibua wachezaji wapya ambao ni faida kwa TAIFA STARS.

Katika kikosi cha KILIMANJARO STARS kilichotangazwa na kocha huyo kinachotarajiwa kujipima nguvu tarehe 17 mwezi huu na kati ya timu ya taifa ya ETHIOPIA au KENYA kina sura mpya ambazo ni pamoja na GAUDENCE MWAIKIMBA, JUMA NOYSO, KIGI MAKASI na THOMAS ULIMWENGU amayecheza soka la kulipwa huko SWEDEN.

KILIMANJARO STARS imepangwa katika katika kuindi A kwenye mashindano ya CECAFA TUSTER CHALLENGE CUP na itaanza kutupa karata yake ya kwanza dhidi ya ZAMBIA katika mchezo wa ufunguzi NOVEMBA 27 kabla ya kuzikabili SOMALI NOVEMBA 30 na BURUNDI DECEMBA 4.


No comments:

Post a Comment