Saturday, December 11, 2010

michezo ya leo


Kilimanjaro Stars uso kwa uso na Ivory Coast fainali Cecafa.
Timu ya taifa ya TANZANIA BARA The KILIMANJARO STARS kesho inateremka dimbani kuikabili timu ya taifa ya IVORY COAST maarufu kama tembo katika mchezo wa fainali ya cecafa tusker challenge cup utakaofanyika katika dimba la taifa jijini DSM
Akizungumza na waandishi habari jijini dsm hii leo katibu mkuu CECAFA NICOLUS MSONYE amewataka wantazania kujitokeza kwa wingi kuishingilia STARS ili iibuke na ushindi na kulinyakua kombe ambapo pia amesema washindi wa zawadi mbali mbali waliofanya vyema katika michuano hiyo watazawadiwa huku mratibu wa michuano hiyo SAADI KAWEMBA akiombea dua timu ya IVORY COAST kumaliza matatizo yake ya kisiasa yamalizike na warejeee tena kama wataalikwa .
Kabla ya The KILIMANJARO STARS kuivaa IVORY COAST kutakua na mchezo wa kumtafuta mshindi wa tatu kati ya ETHIOPIA ambao walifungwa na IVORY COAST katika mchezo wa nusu fainali dhidi ya UGANDA ambao wao walitolewa na STARS katika mchezo wa nusu fainali kwa mikwaju MITANO YA PENATI dhidi ya minne.
= =
Michezo ya shule za msingi kuzinduliwa jumanne ijayo
Michezo kwa shule za msingi hapa nchini inatarajiwa kuzinduliwa tarehe 14 hadi 21 mwezi huu huko KIBAHA mkoani PWANI ambapo rais wa jamuhuri ya muuungano wa TANZANIA,JAKAYA MRISHO KIKWETE atakuwa mgeni rasmi.
Hayo yamesemwa na naibu waziri wan chi ofisi ya waziri mkuu TAMISEMI anayeshughulikia ELIMU KASSIM MAJALIWA amesema kuwa michezo inapoanaznia katika shule za msingi ni rahisi kupata wachezaji wenye vipaji kutokana na kufundishwa kuanzia wakiwa na umri mdogo.
MAJALIWA amesema kuwa mikoa kumi kwa kuanzia itashiriki katika michezo hiyo ambayo inatarajiwa kuleta hamasa katika hule mbali mbali za msingi kurejesha hali ya michezo ambayo ilitoweka tangu mwaka 2000.
Amesema michezo itakayochezwa ni pamonja na soka, mpira wa pete, mbio ambazo zitakuwa kuanzia za mita mia moja hadi elfu moja na mia tano.
= =
TARRICK kuwakilisha nchi majahazi MALAYSIA
Kijana TARRICK NIELSEN atakwenda nchini MALYSIA kuwakilisha TANZANIA katika michuano ya majahazi ya dunia itakayofanyika kuanzia terehe 28 mwezi dec hadi januari 12 mwakani.
Akizungumza na waandishi wa habari katika mazoezi yake ya msiho mchezji huyo amesema kuwa amefanya maaandalizi kabbambe ambapoa anaamini antaweza kufanya vyema.
Mchezaji huyo ambaye ana miaka 13 ameanza kujifunza mchezo huo akiwa na miaka saba ambapo ametumia muda wa mwaka mmoja kuajiandaa kwenda ksuhiriki katika amshindano hayo.
= =
SOLOMON aendelea vyema
Msanii wa nyimbo za injili wa nchini ZAIRE anayeishi nchini KENYA SOLOMONI MKUBWA amepata nafuu na amerushusiwa hospitali baada ya kulazwa kutokana na kupata ajali ya gari akiwa anaelekea mpakani mwa TANZANIA na KENYA SIRALI.
Mratibu wa msanii huyo hapa nchini , ALEX MSAMA amesema kuwa msaniii huyo amepata nafuuu na karibuni ataendeelea na huduma yake ya kutoa neon la mungu kupitia nyimbo za injili.
Katika hatua nyingine,MSAMA amesema kuwa kampuni yake kwa sasa inajiandaa na tamsha la injili la PASAKA na si CHRISTMAS kama ilivyozoeleka ambapo amewataka wapenzi wa muziki wa injili kuwa wavumilivu.

No comments:

Post a Comment