Wednesday, December 1, 2010

Uganda na Ethiopia,KENYA na Malawi michuano ya CECAFA.

Michuano ya CECAFA TUSKER CHALLENGE CUP inaendelea mchana wa leo katika kundi la C, kwa mabingwa watetezi UGANDA kupepetana na ETHIOPIA huku KENYA ikiteremka dimbani dhidi ya MALAWI meche zote mbili zinachezwa kwenye dimba la TAIFA jijini DSM.

Katika michezo ya jana ya kundi la B, ZANZIBAR HEROES ilianza vyema michuano hiyo baada ya kuichapa SUNDAN kwa mabao MAWILI kwa bila yote yakifungwa na mshambuliaji ALLY AHMED SHIBOLI.

Mchezo mwingine wa kundi B, RWANDA wakaichapa wababe kutoka Afrika ya Magharibi IVORY COAST kwa mabao MAWILI kwa MOJA.

BURUNDI ilitoke kifua mbele baada ya kuifunga SOMALIA kwa mabao MAWILI kwa BILA.

katika mchezo wa kiporo wa kundi la A, ulichezwa jana katika dimba la KARUME,

===

Chelsea na LIVERPOOL zashindwa kutamba ligi kuu ya ENGLAND

Mabingwa watetezi wa ligi kuu ya ENGELAND CHELSEA jana walishindwa kurundi kileleni mwa ligi hiyo baada ya kulazimisha sare ya kufungana bao moja kwa moja na NEWCASTLE UNITED katika uwanja wa ST JAMES PARK.

NEWCASTLE UNITED ndio walionza kuzifumania nyavu za CHELSEA kupitia kwa mshambuliaji chipukizi wa klabu hiyo ANDY CARROLL baada ya kuuwahi mpira uliorejeshwa na mabaki wa CHELSEA kwa kipa wao PETER CHEKI.

Bao la CHELSEA likapachikwa wavuni na Salomon Kalou kufuatia kazi nzuri iliyofanywa na MFARANSA FLORENT MALOUDA.

LIVERPOOL nao wakaendelea kuchechemea baada ya kukubali kichapo cha mabao MAWALI kwa MOJA kutoka kwa mahasimu wao TOTTENHAM HOTSPUR mchezo ulichezwa kwenye dimba la WHITE HART LANE.

Goli lililozima ndoto za LIVERPOOL za kuondoka na angalao na Alama moja ugenini lilikwamishwa wavuni ni chipukizi AARON LENNON katika dakika za nyongeza baada ya kuwazidi mbio mabeki wa LIVERPOOL na kuutumbukiza mpira wavuni.

MANCHESTR UNITED wapo kileleni mwa ligi hiyo wakiwa na Alama 31 baada ya kuichapa BLACKBURN ROVERS mabao 7-1 mwishoni mwa wiki.

CHELSEA wapo katika nafasi ya pili ikiwa na ALAMA 29 sawa na ARSENAL, lakini ARSENAL wanashika nafasi ya tatu kutokana na tofauti ya mabao ya kufunga.

Manchester City wapo katika nafasi ya nne ya msimamo wa ligi hiyo wakiwa na ALAMA 26 baada ya kulazimishwa sare ya kufungana bao MOJA kwa MOJA Stoke City wakati SPURS wapo katika nafasi ya tano wakiwa na ALAMA 25.

===

BARCELONA uso kwa uso na REAL MADRID LA LIGA.

Leo ni leo katika ligi kuu ya HISPANIA maarufu kama LA LIGA wakati REAL MADRID watakapomenyana na BARCELONA katika mchezo unaitwa EL-CLASICO mchezo utakaopigwa kwenye dimba la Nou Camp.

Kocha wa REAL MADRID MRENO JOSE MOURINHO anajivunia kurejea kwa wachezaji wake kutoka kwenye majeruhi GONZALO HIGUAIN na SAMI KHEDIRA baada ya kuumia katika mchezo wa ligi hiyo dhidi ya ATHLETIC BILBAO wiki iliyopita.

REAL MADRID haijapoteza mchezo wowote katika michuano mbalimbali na katika LA LIGA imeshinda michezo KUMI na kutoka sare MARA MBILI katika msimu huu.

Mechi mbili za msimu kati ya REAL MADRID na BARCELONA ndiyo zinategemewa kuamua ni nani bingwa kwatika ligi hiyo ya HISPANIA LA LIGA na timu itakaoshinda mechi ya leo itakuwa kwenye nafasi nzuri ya kutwaa ubingwa wa LA LIGA mwishoni mwa msimu.

Katika mchezo wa leo safu za ushambuliaji za timu zote mbili ndio zitaumua timu ipi itaondoka na ushindi.

REAL MADRID inawategemea washambuliaji wake Cristiano Ronaldo, Higuain, Ozil na Angel Di Maria,wakati mabingwa watetezi BARCELONA wao watawategemea zaidi Lionel Messi, David Villa, Pedro na Andres Iniesta.

== ==

Valencia yashinda LA LIGA

Katika michezo ya ligi kuu ya HISPANIA LA LIGA iliyochezwa jana VALENCIA imeibuka kidedea baada ya kuifunga ALMERIA kwa mabao MAWILI kwa MOJA.

Mabao ya VALENCIA yakipachikwa wavuni na ROBERTO SOLDADO,katika mchezo mwingine ulipigwa jana ESPANYOL imepaa hadi nafasi ya nne baada ya hiyo jana kuifunga ATLETICO MADRID mabao MATATU kwa MAWILI.

VILLARREAL nao wameibuka kidedea baada ya kuwafunga REAL ZARAGOZA kwa mabao MATATU kwa BILA wakati . ATHLETIC BILBAO wao wakiibuka na ushinmdi wa bao MOJA kwa BILA dhidi ya OSASUNA.

Msimamo wa ligi hiyo unaonyesha kwamba REAL MADRID inaongoza wakiwa na ALAMA 32, BARECELONA wapo katika nafasi ya pili wakiwa na ALAMA 31, VILLARREAL wapo katika nafasi ya TATU wakiwa na ALAMA 27, wakati ESPANYOL wapo katika nafasi ya NNE wakiwa na ALAMA 25.

===

LIVERPOOL kumenyana na MAN UNITED FA CUP

MANCHESTER UNITED itaikabili LIVERPOOL katika mchezo wa kuwania ubingwa kombe la FA mzunguko wa tatu, mchezo utakaopigwa kwenye dimba la OLD TRAFFORD JANURY mwakani.

ARSENAL wao wamepangiwa vibonde LEEDS UNITED huku CHELSEA wakicheza na IPSWICH.

STEVENAGE itaikabili NEWCASTLE, vijana WA SVEN-GORAN ERIKSSON timu ya LEICESTER wao watakua na kazi ngumu ya kuikabili timu iliwahi kufundishwa na Eriksson, Manchester City.

Michezo hiyo ya kuwania KOMBE LA FA mzunguko wa tatu itachezwa mwezi JANUARY mwakani kati ya tarehe nane na tisa huku mchezo ukaovuta hisia za mashabiki wengi wa soka duniani ukiwa kati ya MAN UNITED na LIVERPOOL.

==

Roger Federer anyakua ubingwa wa ATP World Tour

Katika tenesi mchezaji namba mbili kwa ubora wa tenesi dunia ROGER FEDERER amefanikiwa kunyakua ubingwa wa ATP WORLD TOUR baada ya kuchapa RAFAEL NADAL kwa seti mbili kwa moja ya ushindi wa 6-3, 3-6, 6-1 mchezo uliopigwa kwenye uwanja wa O2 ARENA jijini LONDON.

FEDERER amenyakua ubingwa huo katika mchezo ulidumu kwa muda wa saa moja na dakika thelathini na SABA dhidi ya mpizani wake Rafael Nadal.

Huu utakua ni ushindi wa pili mkubwa kwa FEDERER kwa mwaka huu baada ya kunyakua taji la AUSTRALIAN OPEN mwezi January mwaka huu na sasa amenyakua taji la ATP World Tour katika fainali iliyokua inashirikisha wachezaji NANE nyota duniani kwa upande wa wanaume.

Katika michezo ya nusu fainali NADAL alimufunga ANDY MURRAY huku FEDERER akimchapa NOVAK DJOKOVIC.

===

No comments:

Post a Comment