Sunday, August 22, 2010

STARS ya kuivaa Al-geria yatangazwa

Kocha mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars JAN POULSEN anatangaza kikosi cha timu hiyo jijini Arusha hii leo kitakacho ivaa Algeria ugenini Septemba 4.

Kikosi hicho kitaingia kambini jijini DSM kesho tayari kwa mazoezi ya kujiweka sawa kwa ajili ya mchezo huo.

Katika kikosi kitakacho tangazwa leo haitarajiwi kama kocha huyo atafanya mabadiliko makubwa licha ya kushuhudia michezo miwili,mchezo kati ya watani wa jadi Simba na Yanga uliopingwa siku ya jumatano kwania Ngao ya Hisani uliochezwa katika uwanja wa Taifa jijini DSM na ule wa jana uliopingwa katika uwanja wa Shekhe Amur Abed kati ya AFC na Azam FC.

Wachambuzi wa mambo ya michezo wanasema kocha atarudisha wachezaji wale wale aliowaita kwa ajili ya mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Harambee Stars mchezo ulipingwa AUGOSTI 11 katika uwanja wa Taifa jijini DSM na timu hizo kufungana bao moja kwa moja.

Pia POULSEN anatarajiwa kuwateua katika timu yake wachezaji wanosukuama soka ya kulipwa ambao ni Nizar Khalifan anayekipinga katika timu ya Vacouvor White Camps ya Canada,Henry Josophy anayecheza Sweeden na mshambuliaji wa timu hiyo Danny Mrwanda anayecheza Veitnam na Idrisa Rajabu wa Sofapaka ya Kenya.

Star ikishashuka dimbani dhidi ya Algeria ugenini Septemba 4 itakabiliwa na mtihani mwingine mgumu nyumbani dhidi ya timu ngumu ya MORROCCO Octoba 9.

Timu ya taifa ya Tanzania,Taifa Stars imepangwa katika kundi lenye timu za Jamhuri ya Afrika ya Kati,Morocco na Algeria.

No comments:

Post a Comment