Tuesday, August 31, 2010

TWIGA STARS Kambini

Timu ya taifa ya soka ya wanawake TWIGA STARS itacheza michezo minne ya kimataifa dhidi ya timu ya taifaya AFRIKA YA KUSINI Banyana Banyana na ZIMBABWE mwezi ujao kujiweka sawa na fainali za kombe la matifa ya Afrika kwa wanawake yanayotarajiwa kufanyika mwezi OCTOBA nchini Afrika ya kusini.
Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kutangaza kikosi cha wachezaji 25 wa timu hiyo wanaoanza kambi kesho, Kocha mkuu wa TWIGA STARS, CHARLESE MKWASA, amesema wameamua kuanza kambi mapema igawa hawajui tarehe ya kuanza kwa mashindano hayo ya Afrika kwa wanawake.
Mkwasa amesema TWIGA STARS,itacheza na Banyana Banyana septemba 29 na Oktoba 2 na pia itacheza dhidi ya ZIMBABWE Octoba 6 na 10 kwa lego la kuiweka sawa timu hiyo kabla ya mashindano hayo makubwa barani Afrika kwa wanawake na kwamba michezo hiyo itachezwa jijini DSM.Fainali za soka kwa mataifa ya Afrika kwa wanawake yatazishirikisha timu za taifa za Algeria,Ghana,Tunisia,Equitoria Gine,Tanzania,Cameroon na wenyeji Afrika ya Kusini na yanatarajiwa kutimua vumbi mwezi Okatoba

No comments:

Post a Comment